Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inabadilisha Maisha Ya Watu

Biblia Inabadilisha Maisha Ya Watu

Biblia Inabadilisha Maisha Ya Watu

NI NINI kilichomusaidia mwanamuke mumoja kijana, ambaye hakupendezwa na Mungu na ambaye alikuwa na kazi nzuri sana, apate kusudi katika maisha? Kijana mumoja Mukatoliki alijifunza mambo gani juu ya kifo ambayo yalimusaidia kubadilisha maisha yake? Na ni nini kilichomusaidia kijana mumoja aliyechoshwa na maisha kujifunza juu ya Mungu na kumuchochea kuwa muhudumu Mukristo? Usome mambo ambayo watu hao wanaeleza.

“Kwa miaka mingi nilijiuliza, ‘Sababu gani tunaishi?’”​—ROSALIND JOHN

ALIZALIWA MWAKA WA 1963

ALIZALIWA KATIKA INCHI YA GRANDE-BRETAGNE

ALIKUWA NA KAZI YENYE MUSHAHARA MUZURI SANA

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilizaliwa katika muji wa Croydon, Kusini mwa Londres, niko mutoto wa 6 katika familia ya watoto 9. Wazazi wangu walizaliwa katika kisiwa cha Caraïbes ya Saint Vincent. Mama alikuwa katika kanisa la Metodiste. Hata kama nilikuwa na tamaa ya kujua mambo mengi, sikupenda kujifunza juu ya Mungu. Mara nyingi nilikuwa ninapitisha wakati wa mapumuziko ya masomo kwenye bahari iliyo katika eneo letu, nikisoma vitabu vingi ambavyo nilikuwa ninakopa mahali fulani pa kuchungia vitabu.

Miaka fulani kisha kumaliza masomo ya segondere, nilitambua kama nilitamani kusaidia watu wa hali ya chini. Nilianza kusaidia watu wasio na makao, walemavu na watu walio na matatizo ya kujifunza. Kwa hiyo, nilienda kwenye université ili kujifunza mambo ya kiganga. Nilipomaliza masomo hayo, niliendelea kupata kazi nyingi zenye mushahara muzuri na maisha yangu yakaendelea kuwa mazuri sana. Wakati fulani nilikuwa mushauri musimamizi na mutafiti katika mambo ya kijamii, wakati huo nilihitaji tu ordinatere ndogo na kutumia Internete ili kufanya kazi yangu. Nilikuwa ninasafiri kwa avion katika inchi za kigeni kwa majuma fulani, nilikaa katika hoteli niliyofurahia zaidi, nilifurahia mazingira mazuri, na nilienda katika vyumba vya mazoezi ili nisinenepe. Nilifurahia maisha kabisa. Lakini niliendelea kuhangaikia watu wa hali ya chini.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Kwa miaka mingi nilijiuliza, ‘Sababu gani tunaishi, na maisha yana kusudi gani?’ Lakini sikujaribu kutafuta majibu ya maulizo hayo katika Biblia. Siku moja katika mwaka wa 1999, Margaret, dada yangu mudogo, aliyekuwa Shahidi wa Yehova alinitembelea pamoja na rafiki yake aliyekuwa pia Shahidi. Shahidi huyo alipendezwa kabisa nami. Nilikubali kujifunza naye Biblia, lakini sikufanya maendeleo haraka kwa sababu kazi zangu na namna yangu ya kuishi vilinichukua wakati mwingi.

Katika mwaka wa 2002, nilihamia kusini mangaribi mwa Angleterre. Huko, nilienda tena kwenye université ili kuongeza masomo ya utafiti katika mambo ya kijamii, nilikuwa na kusudi la kupata diplome ya doktora. Nilianza kuhuzuria mikutano kwa ukawaida kwenye Jumba la Ufalme pamoja na mutoto wangu mudogo. Hata kama nilisoma sana, kujifunza Biblia kulianza kunisaidia kuelewa sababu gani tuna matatizo katika maisha na namna matatizo hayo yatamalizika. Niliona kama maneno ya Mathayo 6:24 ni ya kweli, andiko hilo linaonyesha kama hakuna mutu anayeweza kutumikia mabwana wawili. Nilipaswa kutumikia Mungu ao utajiri. Nilijua kama nilipaswa kuchagua mambo ya kutia pa nafasi ya kwanza katika maisha yangu.

Mwaka uliopita, nilikuwa ninahuzuria mara kwa mara funzo la Biblia ambalo Mashahidi wa Yehova walikuwa wanafanya nyumbani; wakati huo walikuwa wanajifunza kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? * Nilisadikishwa kama ni Yehova, muumbaji wetu tu, ndiye anaweza kumaliza matatizo ya watu. Lakini kwenye université, nilikuwa ninafundishwa kama si lazima kumuamini Muumbaji ili kuelewa kusudi la maisha. Hilo lilinikasirisha sana. Kisha miezi 2, niliacha masomo hayo na nikaamua kupitisha wakati mwingi katika mambo ya kiroho.

Andiko la Biblia lililonichochea kubadilisha maisha yangu ni Methali 3:5, 6. Andiko hilo linasema hivi: ‘Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Umutambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.’ Kujifunza juu ya Mungu wetu mwenye upendo kuliniletea faida nyingi ambazo utajiri ao masomo marefu havingeweza kuniletea. Nilipoendelea kujifunza juu ya kusudi la Yehova kuhusu dunia na daraka ambalo Yesu alitimiza kupitia kifo chake, nilitaka kujitoa kwa Muumbaji wetu. Nilibatizwa katika Mwezi wa 4, 2003. Kisha hapo, nikaanza hatua kwa hatua kubadilisha namna yangu ya kuishi.

FAIDA AMBAYO NIMEPATA: Urafiki ambao nimefanya pamoja na Yehova ni wa lazima sana. Kumujua Yehova kumeniletea amani ya moyoni na furaha. Kukusanyika pamoja na waabudu wa kweli wa Mungu kumeniletea pia furaha.

Mambo ninayojifunza katika Biblia na kwenye mikutano ya Kikristo yanaendelea kutosheleza tamaa yangu ya kujua mambo mengi. Ninafurahia sana kuwahubiria wengine mambo ninayoamini. Hiyo imekuwa kazi yangu, kazi hiyo ndiyo inaniwezesha kabisa kusaidia wengine wawe na maisha mazuri leo na tumaini nzuri la kuishi katika dunia mupya wakati unaokuja. Nimekuwa muhubiri wa wakati wote tangu Mwezi wa 6, 2008, na mimi ni mwenye furaha zaidi kuliko nilivyokuwa zamani. Sasa ninajua kusudi la maisha, na kwa hiyo ninamushukuru Yehova sana.

“Kifo cha rafiki yangu kiliniumiza sana moyoni.”​—ROMAN IRNESBERGER

ALIZALIWA MWAKA WA 1973

ALIZALIWA KATIKA INCHI YA AUTRICHE

ALIZOEA SANA MICHEZO YA FEZA

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilikomalia katika muji mudogo wa Braunau, huko Autriche. Watu walikuwa matajiri katika muji huo, na uvunjaji wa sheria haukuwa mwingi. Familia yangu ilikuwa ya Wakatoliki, kwa hiyo mimi pia nilikuwa Mukatoliki.

Jambo fulani lililotendeka nilipokuwa mutoto liliniumiza sana moyoni. Siku moja, katika mwaka wa 1984, nilipokuwa na miaka karibu 11, nilicheza kabumbu na mumoja wa marafiki wangu wa sana. Siku hiyohiyo, aliuawa katika aksida ya motokari. Kifo cha rafiki yangu kiliniumiza sana moyoni. Kwa muda wa miaka mingi kisha aksida hiyo, nilijiuliza mahali ambapo tunaenda wakati tunakufa.

Nilipomaliza masomo, nikakuwa fundi wa umeme (courant). Hata ikiwa nilizoea michezo ya feza na nilikuwa ninachezea feza nyingi sana, sikuwa na matatizo ya feza. Nilipitisha pia wakati mwingi katika michezo mingine na nilipenda miziki yenye mudundo mukali. Maisha yangu yalikuwa tu kujifurahisha na kuenda kwenye bare ili kunywa pombe na kucheza. Nilikuwa ninaishi maisha machafu, na ya kutafuta raha tu lakini sikuwa na kusudi katika maisha.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Katika mwaka wa 1995, Shahidi wa Yehova mumoja aliyezeeka alinitembelea na akanipatia kitabu kilichojibia ulizo, Mutu anapokufa, anaenda wapi? Nilichukua kitabu hicho kwa sababu kifo cha rafiki yangu kiliendelea kuniumiza sana moyoni. Nilisoma sura inayozungumuzia kifo na kisha nikasoma kitabu chote.

Mambo niliyosoma yalijibia maulizo yangu juu ya kifo. Lakini nilijifunza mambo mengi zaidi. Kwa sababu nilikomalia katika dini ya Katoliki, imani yangu ilitegemea Yesu tu. Lakini, kujifunza Biblia kwa uangalifu kulinisaidia kufanya urafiki na Yehova Mungu, Baba wa Yesu. Nilishangaa kujua kama Yehova anatuhangaikia na kama anatutia moyo tumujue. (Mathayo 7:7-11) Nilijifunza kama Yehova anaweza kufurahi ao kuhuzunika. Tena nilijifunza kama anatimiza neno lake sikuzote. Hilo lilinichochea nipendezwe zaidi na unabii mbalimbali wa Biblia na kuchunguza namna ulivyotimizwa. Mambo niliyojifunza yalinifanya nimuamini Mungu zaidi.

Nilielewa haraka kama ni Mashahidi wa Yehova tu ndio wanaopendezwa kabisa na kusaidia watu kuelewa Biblia. Niliandika maandiko yaliyokuwa katika vitabu vyao na kisha nilisoma maandiko hayo katika Biblia yangu ya Katoliki. Nilipoendelea kujifunza, nilitambua kama nilikuwa nimepata kweli.

Kujifunza Biblia kulinisaidia kujua kama Yehova anapenda niishi kulingana na kanuni zake. Niliposoma andiko la Waefeso 4:22-24, niliona kama nilipaswa kuvua “utu wa zamani,” unaolingana na ‘mwenendo wangu wa kwanza’ na ‘kuvaa utu mupya ulioumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu.’ Kwa hiyo, niliacha maisha yangu machafu. Tena niliona kama nilipaswa kuacha michezo ya feza, kwa sababu tabia hiyo inamuchochea mutu apende vitu vya kimwili na awe na tamaa mbaya. (1 Wakorintho 6:9, 10) Nilijua kama ili kufanya mabadiliko hayo, nilipaswa kuachana na marafiki wangu wa zamani na kutafuta marafiki wapya wanaoshika kanuni za Biblia.

Haikuwa vyepesi kwangu kufanya mabadiliko hayo. Lakini nilianza kuhuzuria mikutano pamoja na Mashahidi wa Yehova kwenye Jumba la Ufalme, na nilianza kupata marafiki wapya katika kutaniko letu. Tena niliendelea kujifunza Biblia kwa uangalifu mimi mwenyewe. Kufanya hivyo kulinisaidia kuacha kusikiliza miziki isiyofaa, kubadilisha miradi yangu maishani, na namna yangu ya kuvaa na kukata nywele. Katika mwaka huohuo wa 1995, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova.

FAIDA AMBAYO NIMEPATA: Sasa nina maoni yenye kufaa juu ya feza na vitu vya kimwili. Zamani nilikuwa mutu mwenye hasira sana, lakini sasa mimi ni mutu mwenye kutulia. Na sihangaikie tena sana wakati unaokuja.

Ninafurahi kuwa katika familia ya watu wa mataifa yote wanaomutumikia Yehova. Kati yao ninaona watu wanaopambana na matatizo, lakini wanaendelea kumutumikia Mungu kwa uaminifu. Ninafurahi sana kwa sababu sasa ninatumia wakati wangu wote na nguvu zangu zote ili kumuabudu Yehova na kuwatendea watu wengine mambo mema, sivitumie tena ili kutosheleza tamaa zangu mwenyewe.

“Mwishowe, maisha yangu yana kusudi.”​—IAN KING

ALIZALIWA MWAKA WA 1963

ALIZALIWA KATIKA INCHI YA ANGLETERRE

ALIKUWA MWENYE KUCHOSHWA NA MAISHA

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilizaliwa huko Angleterre, lakini nilipokuwa na miaka karibu 7, familia yangu ilihamia huko Australie. Tuliishi katika eneo la Gold Coast, mahali panapotembelewa sana na wageni huko Queensland, Australie. Hata ikiwa familia yetu haikuwa tajiri, sikuzote tulipata vitu tulivyohitaji.

Ijapokuwa wazazi wangu walinilea vizuri, sikuwa mwenye furaha hata kidogo. Nilikuwa mwenye kuchoshwa na maisha. Baba yangu alikuwa mulevi sana. Sikumupenda hata kidogo, zaidi sana kwa sababu ya ulevi wake na namna alivyokuwa anamutendea mama yangu. Baadaye, nilijua mambo aliyopitia maishani mwake alipokuwa askari huko Malaya, na hivyo nikaanza kuelewa sababu gani alikuwa anatenda kwa njia hiyo.

Nilipokuwa kwenye masomo ya segondere, nilianza kulewa sana na nilipofikia miaka 16, niliacha masomo na kujiunga na kikundi cha askari wa majini. Nilianza kutumia dawa za kulewesha na nikakuwa muvutaji mukubwa wa tumbaku. Tena, nikaanza kunywa pombe sana. Sasa nilianza kunywa pombe nyingi si mwisho wa juma tu lakini kila siku.

Nilipokuwa na miaka 18 ao 19 hivi mupaka 20 na kitu, nilianza kuwa na mashaka juu ya kuwapo kwa Mungu. Niliwaza hivi: ‘Ikiwa Mungu iko, sababu gani anawaacha watu wateseke na kufa?’ Niliandika hata habari fulani za kumulaumu kwa sababu ya mambo yote mabaya yanayotendeka duniani.

Nilipofikia miaka 23, niliachana na kikundi cha askari wa majini. Kisha hapo, nilifanya kazi mbalimbali na hata nilisafiri katika inchi za kigeni kwa muda wa mwaka mumoja, lakini hakuna kitu kilinisaidia kuwa mwenye furaha. Sikuwa hata na tamaa ya kujiwekea miradi fulani ao kutimiza jambo lolote. Sikupendezwa kabisa na kitu chochote maishani mwangu. Matumaini ya kupata nyumba, kuwa na kazi nzuri, na kupata cheo, yote hayo niliyaona kuwa mambo ya bure. Kunywa pombe na kusikiliza muziki ndiyo mambo tu yaliyonituliza.

Ninakumbuka kabisa wakati nilitamani sana kuwa na kusudi katika maisha. Nilipokuwa huko Polonye, nilitembelea kambi ya mateso ya Auschwitz. Mbele ya hapo, nilisoma juu ya namna watu walivyoteswa katika kambi hiyo. Lakini niliposimama hapo na kuona ukubwa wa kambi hiyo, niliumia sana moyoni. Singeweza kuelewa sababu gani wanadamu wangeweza kuwatesa vikali hivyo wanadamu wenzao. Ninakumbuka nilipotembea katika kambi hiyo nikiwa mwenye kutokwa na machozi na kujiuliza, ‘Sababu gani?’

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Katika mwaka wa 1993, kisha kurudi nyumbani, nilianza kusoma Biblia ili kupata majibu. Muda kidogo kisha hapo, Mashahidi wa Yehova wawili waliokuwa wanahubiri nyumba kwa nyumba waligonga kwenye mulango wangu na wakanialika kuhuzuria mukusanyiko kwenye uwanja uliokuwa karibu na kwetu. Niliamua kuhuzuria mukusanyiko huo.

Miezi michache mbele ya hapo, nilikuwa kwenye uwanja huo kutazama muchezo wa kabumbu, lakini kulikuwa tofauti kubwa kati ya muchezo wa kabumbu na mukusanyiko huo. Mashahidi wa Yehova walikuwa wenye adabu na wenye kuvaa vizuri, na watoto wao walikuwa na mwenendo muzuri. Mambo niliyoona wakati wa chakula cha muchana yalinishangaza sana. Mamia ya Mashahidi wa Yehova walikaa chini kwenye uwanja huo ili kula chakula cha muchana, lakini waliporudi kwenye viti vyao, sikuona hata uchafu wowote chini! Zaidi ya yote, watu hao walionekana kuwa wenye furaha na amani​—jambo ambalo nilitamani sana. Sikumbuke hata hotuba moja iliyotolewa siku hiyo, lakini mwenendo wa Mashahidi hao ndilo jambo ambalo lilinivutia sana.

Mangaribi ya siku hiyo, niliwaza juu ya binamu yangu aliyesoma Biblia na kujifunza vitabu vingi juu ya dini mbalimbali. Miaka mingi mbele ya hapo, binamu huyo aliniambia kwamba Yesu alisema tunaweza kutambua dini ya kweli kupitia matunda yake. (Mathayo 7:15-20) Nilifikiri nilipaswa kuchunguza mambo yanayowafanya Mashahidi wa Yehova wawe tofauti sana na watu wengine. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilijisikia kuwa na mawazo mazuri na mwenye tumaini.

Juma lililofuata, wale Mashahidi wa Yehova wawili walionialika kwenye mukusanyiko walinitembelea tena. Waliniomba nijifunze nao Biblia, na nikakubali. Nikaanza pia kuhuzuria mikutano ya kutaniko pamoja nao.

Nilipoendelea kujifunza Biblia, mawazo yangu juu ya Mungu yalibadilika kabisa. Nilijifunza kama Mungu hatokeze mambo mabaya na mateso, na kama anaumia moyoni anapoona watu wanafanya mambo mabaya. (Mwanzo 6:6; Zaburi 78:40, 41) Nilikusudia kuepuka kabisa kufanya jambo lolote linaloweza kumuumiza Yehova moyoni. Nilitaka kufanya mambo yanayomufurahisha. (Methali 27:11) Niliacha kunywa pombe sana na kuvuta tumbaku, na niliachana na mwenendo muchafu. Mwezi wa 3, 1994, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova.

FAIDA AMBAYO NIMEPATA: Mimi ni mwenye furaha kabisa na mwenye kutosheka. Sikunywe tena pombe ili kujaribu kutatua matatizo yangu. Lakini, nimejifunza kumutupia Yehova mizigo yangu.​—Zaburi 55:22.

Kumepita miaka 10 tangu nilipomuoa Karen, mwanamuke mwenye sura nzuri ambaye ni Shahidi wa Yehova, na nina binti mwenye sura nzuri anayeitwa Nella ambaye Karen alizaa na mwanaume mwengine. Sisi watatu tunapitisha wakati mwingi katika kazi ya kuhubiri ili kuwasaidia wengine wajifunze kweli juu ya Mungu. Mwishowe, maisha yangu yana kusudi.

[Maelezo ya chini]

^ Kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.