Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Je, maneno ya Yesu katika Mathayo 19:10-12 yanaonyesha kama wale wanaochagua kubaki bila kuoa ao kuolewa wamepata zawadi hiyo kwa njia fulani ya kimuujiza?

▪ Fikiria mambo yaliyomufanya Yesu aseme maneno hayo. Mafarisayo walipokuja mbele yake na kumuuliza kuhusu kuvunja ndoa, Yesu aliwafunulia waziwazi kanuni ya Mungu kuhusu ndoa. Hata ikiwa Sheria ilimuruhusu mwanaume kuandikia bibi yake cheti cha kuvunja ndoa kwa sababu amepata “kitu fulani kisichofaa” katika bibi yake, mambo hayakuwa hivyo tangu mwanzo. (Kum. 24:1, 2) Kwa hiyo Yesu alisema hivi: ‘Mutu yeyote anayemutaliki muke wake na kumuoa mwingine, ila kwa sababu ya uasherati, anafanya uzinzi.’​—Mt. 19:3-9.

Waliposikia maneno hayo, wanafunzi walisema hivi: “Ikiwa hivyo ndivyo ilivyo kati ya mwanamume na muke wake, ni afazali kutooa.” Lakini, Yesu aliwajibu hivi: “Si watu wote wanaolipa nafasi neno hilo, ila tu wale walio na hiyo zawadi. Kwa maana kuna matowashi waliozaliwa namna hiyo kutoka katika tumbo la uzazi la mama yao, na kuna matowashi waliofanywa matowashi na watu, na kuna matowashi ambao wamejifanya wenyewe matowashi kwa sababu ya ufalme wa mbinguni. Yule anayeweza kulipa nafasi na alipe nafasi.”​—Mt. 19:10-12.

Matowashi wa kimwili ni wale waliozaliwa hivyo kwa sababu ya kasoro fulani ao labda wamekuwa katika hali hiyo kwa sababu ya aksida ao kwa sababu ya kuharibiwa kwa viungo vyao vya uzazi. Hata hivyo, kuna wale waliojifanya wenyewe matowashi. Hata ikiwa wangeweza kufunga ndoa, wanaendelea kujizuia na wanabaki pasipo kuoa ao kuolewa “kwa sababu ya ufalme wa mbinguni.” Kama Yesu, wanachagua kutumia hali yao ya kutokuoa ao kutokuolewa ili kufanya mengi katika kazi ya Ufalme. Hawakuzaliwa na zawadi hiyo wala hawakuipata kwa njia fulani ya kimuujiza. Waliamua tu kubaki bila kuoa ao kuolewa.

Paulo alijua mambo ambayo Yesu alisema, kwa hiyo alisema kwamba ijapokuwa Wakristo wote, iwe wamefunga ndoa ao hapana, wanaweza kumutumikia Mungu kwa njia anayokubali, wale ambao ‘wametulia moyoni mwao’ ili kubaki hivyo ‘wanafanya vema zaidi.’ Namna gani? Yule aliyefunga ndoa anagawa wakati wake ao nguvu zake ili kutunza bibi ao bwana yake. Lakini, Wakristo ambao hawajafunga ndoa wanaweza kutumia wakati na nguvu zao ili kufanya kazi ya Bwana bila kukengeushwa. Wakristo hao wanaona hali yao kuwa “zawadi” kutoka kwa Mungu.​—1 Kor. 7:7, 32-38.

Kwa hiyo, Maandiko yanaonyesha kwamba Mukristo hapokei zawadi hiyo kwa njia ya kimuujiza. Lakini, anaweza kuamua kubaki hivyo ili kuendeleza faida za Ufalme bila kukengeushwa. Wengi leo wameamua moyoni mwao kubaki bila kuoa ao kuolewa, kwa hiyo Wakristo wengine wanapaswa kuwatia moyo.