Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Ujumbe Ambao Watu Walikuwa Hawajasikia’

‘Ujumbe Ambao Watu Walikuwa Hawajasikia’

Vitu vya Maana Sana vya Historia Yetu

‘Ujumbe Ambao Watu Walikuwa Hawajasikia’

“MITI yote hii ina kazi gani?” George Naish aliuliza ulizo hilo akionyesha rundo lenye urefu wa metre 18 la miti iliyokuwa mahali vitu viliwekwa wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu katika muji wa Saskatoon, Saskatchewan, Canada. Aliambiwa kama miti hiyo ilitumiwa wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ili kujenga minara ya walinzi. Baadaye Ndugu Naish alisema hivi: “Nilifikiri kwamba tunaweza kutumia miti hiyo ili kujenga kituo cha radio, na hivyo ndivyo tulivyoanza kufikiria kufungua kituo cha radio ili kuhubiri habari njema.” Mwaka mumoja baadaye, katika 1924, kituo cha radio kilichoitwa CHUC kilianza kutangaza programe zake. Hiyo ilikuwa moja ya stesheni za radio za kwanza kutangaza habari za Biblia katika Canada.

Kuhubiri kwa njia ya radio kulifaa kabisa katika Canada sababu ni inchi kubwa karibu sawa na Ulaya. Dada Florence Johnson, aliyetumika kwenye kituo cha radio katika muji wa Saskatoon, alisema hivi: “Kupitia radio yetu, watu wengi ambao hatungeweza kuzungumuza nao nyumbani kwao walisikia kweli. Kwa kuwa radio ilikuwa jambo jipya, watu wengi walikuwa na hamu ya kusikiliza jambo lolote lililotangazwa kwenye radio.” Mwishoni mwa 1926, Wanafunzi wa Biblia (jina la zamani la Mashahidi wa Yehova) walikuwa wakitangaza habari njema katika miji ine ya Canada kupitia vituo vyao vya radio. *

Ikiwa ungefungua radio yako na kusikiliza moja ya radio hizo, ungesikia nini? Waimbaji kutoka makutaniko ya karibu waliimba mara kwa mara nyimbo wakifuatana na vyombo vya muziki na hata vikundi vidogo vya wanamuziki. Zaidi ya hayo, ndugu walitoa hotuba na kuwa na mazungumuzo ya Biblia. Ndugu Amy Jones, aliyeshiriki katika mazungumuzo hayo, anakumbuka hivi: “Wakati fulani nilipojitambulisha katika mahubiri, mwenye-nyumba aliniambia, ‘Oh, nakumbuka, nilikusikia kwenye radio.’”

Wanafunzi wa Biblia katika Halifax, Nouvelle​-Écosse, walitumia njia nyingine mupya wakati huo, ni kusema, waliwaalika wasikilizaji waite na kuuliza maulizo ya Biblia kwa kutumia telefone. Ndugu mumoja aliandika hivi: “Watu wengi walifurahia sana programe hiyo. Haikuwezekana kujibu maulizo yote sababu watu wengi sana waliita.”

Kama ilivyotokea kwa mutume Paulo, watu waliitikia ujumbe wa Wanafunzi wa Biblia kwa njia mbalimbali. (Mdo. 17:1-5) Watu fulani walifurahia ujumbe wa Biblia. Kwa mufano, Hector Marshall aliomba mabuku sita ya Études des Ecritures wakati alisikia Wanafunzi wa Biblia wakizungumuzia vitabu hivyo kwenye radio. Baadaye aliandika hivi: “Nilifikiri kama ningetumia vitabu hivyo ili kufundisha Misa ya Watoto ya Siku ya Yenga.” Lakini wakati alimaliza Buku la 1, Hector aliamua kutoka katika dini yake. Alianza kuhubiri kwa bidii, na mupaka kifo chake katika mwaka wa 1998, alikuwa akimutumikia Yehova kwa uaminifu. Kisha kusikiliza hotuba yenye kichwa “Ufalme, Tumaini la Ulimwengu” kwenye radio J. A. MacDonald aliyekuwa mukubwa wa jeshi mashariki mwa muji wa Nouvelle-Écosse, alimuambia ndugu mumoja hivi: “Wakaaji wa Cap-Breton Island walisikia jana ujumbe muzuri sana. Huo ulikuwa ujumbe muzuri sana ambao watu walikuwa hawajasikia katika sehemu hii ya ulimwengu.”

Lakini, viongozi wa makanisa walikasirika. Wakatoliki fulani katika muji wa Halifax walisema kwamba wataharibu kituo cha radio kinachotangaza programe za Wanafunzi wa Biblia. Serikali ilichochewa na viongozi wa kidini, na kwa sababu hiyo katika mwaka wa 1928 ilitangaza kwa gafula kama haitaruhusu tena vituo vya radio ambavyo Wanafunzi wa Biblia wanatumia, viendelee kutangaza programe zao. Kwa hiyo, ndugu na dada waligawanya vikaratasi viliyokuwa na ujumbe unaopinga tendo hilo la kukosa haki. Vikaratasi hivyo vilikuwa na kichwa Anga Ni la Nani? Hata hivyo, serikali ilikataa kuwapa Wanafunzi wa Biblia ruhusa ya kutangaza programe zao.

Je, hilo lilivunja moyo kikundi kidogo cha Mashahidi wa Yehova wa Canada? Dada Isabel Wainwright alisema hivi: “Mwanzoni, ilionekana kwamba adui wetu wameshinda. Lakini ikiwa Yehova alitaka tuendelee kuhubiri kwa njia ya radio, basi yeye hangeruhusu jambo hilo. Kwa hiyo, hilo lilimaanisha kama tulipaswa kutafuta njia nyingine nzuri zaidi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme.” Kuliko kutegemea sana radio ili kuhubiri, Wanafunzi wa Biblia katika Canada walijikaza kuwatembelea watu nyumbani kwao. Kwa kweli, radio ilisaidia wakati fulani kutangaza ‘ujumbe ambao watu walikuwa hawajasikia.’​—Vitu vya Maana Sana vya Historia Yetu kutoka Canada.

[Maelezo ya chini]

^ Ndugu walilipa feza ili kutumia vituo vingine vya radio vya kibiashara ili kutangaza ujumbe wa Biblia.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 32]

“Haikuwezekana kujibu maulizo yote sababu watu wengi sana waliiita”

[Picha katika ukurasa wa 32]

(1) Kituo cha radio katika muji wa Edmonton, Alberta (2) Ndugu anatia kitu kinachoingiza moto katika mashine ya kutangaza habari katika muji wa Toronto, Ontario (3) Kituo cha radio CHUC katika muji wa Saskatoon, Saskatchewan