Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Jina la Mungu ni nani?

Watu wote katika familia zetu wana majina ya kibinafsi. Hata wanyama wa kufugwa wana majina! Je, si jambo linalopatana na akili kwa Mungu kuwa na jina? Katika Biblia, Mungu ana majina mengi ya cheo, kama vile, Mungu Mweza-Yote, Bwana Mwenye Enzi Kuu, na Muumba, lakini pia ana jina la kibinafsi.—Soma Isaya 42:8.

Tafsiri nyingi za Biblia zina jina la kibinafsi la Mungu kwenye Zaburi 83:18. Kwa mfano, kwenye Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, andiko hilo linasema: “Ili watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”

Kwa nini tunapaswa kulitumia jina la Mungu?

Mungu anataka tulitumie jina lake la kibinafsi. Tunatumia majina ya kibinafsi tunapozungumza na watu tunaowapenda, kama vile rafiki zetu wa karibu, hasa wanapotuomba tutumie majina yao. Je, haipaswi kuwa hivyo pia tunapozungumza na Mungu? Zaidi ya hayo, Yesu Kristo aliwatia moyo watu watumie jina la Mungu.—Soma Mathayo 6:9; Yohana 17:26.

Hata hivyo, ili tuwe rafiki za Mungu, tunapaswa kujua mengi zaidi kumhusu mbali tu na kujua jina lake. Kwa mfano, Mungu ana mwili wa aina gani? Je, kweli inawezekana kumkaribia Mungu? Unaweza kupata majibu ya maswali hayo katika Biblia.