Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Jina la Mungu Ni Nani?

Jina la Mungu Ni Nani?

Jina la Mungu Ni Nani?

Watu wote wa familia yetu wana majina ya pekee. Hata wanyama wa kufugwa wana majina. Je, hauone kama ni jambo lenye kupatana na akili kusema kama Mungu ana jina? Katika Biblia, Mungu ana majina mengi ya cheo, kama vile Mungu Mweza-Yote, Bwana Mutawala Mukubwa, na Muumbaji, lakini pia ana jina lake la pekee.​—Soma Isaya 42:8.

Tafsiri nyingi za Biblia zinaonyesha jina la Mungu la pekee katika Zaburi 83:18. Kwa mufano, katika Biblia Takatifu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, andiko hilo linasema hivi: “Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”

Sababu gani tunapaswa kutumia jina la Mungu?

Mungu anataka tutumie jina lake la pekee. Tunatumia majina ya pekee tunapozungumuza na watu tunaowapenda, kwa mufano marafiki ambao tunapendana nao sana, zaidi sana ikiwa wanatuomba tufanye hivyo. Je, hauone kama ni vizuri pia kutumia jina la pekee la Mungu tunapozungumuza naye? Zaidi ya hilo, Yesu Kristo alitutia moyo tutumie jina la pekee la Mungu.​—Soma Mathayo 6:9; Yohana 17:26.

Hata hivyo, ili tuwe marafiki wa Mungu, tunahitaji kujua mambo mengi juu yake kuliko tu kujua jina lake. Kwa mufano, Mungu ni mutu wa namna gani? Je, inawezekana kabisa kumukaribia? Unaweza kupata majibu ya maulizo hayo katika Biblia.