Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo juu ya habari za Biblia yanajibiwa

Maulizo juu ya habari za Biblia yanajibiwa

Sababu Gani Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?

Mungu hana bibi ao muke halisi ambaye alizaa naye watoto. Yeye ni Muumbaji wa viumbe vyote vyenye uzima. Wanadamu waliumbwa wakiwa na uwezo wa kuiga sifa za Mungu. Ndiyo sababu Adamu, mutu wa kwanza ambaye Mungu aliumba, anaitwa “mwana wa Mungu.” Vivyo hivyo, Yesu anaitwa “Mwana wa Mungu” kwa sababu aliumbwa akiwa na sifa kama zile za Baba yake.​—Soma Luka 3:38; Yohana 1:14, 49.

Yesu aliumbwa wakati gani?

Mungu alimuumba Yesu mbele ya kumuumba Adamu. Kwa kweli, Mungu alimuumba Yesu na kisha akamutumia ili kuumba vitu vingine vyote, kutia ndani malaika. Ndiyo sababu Biblia inamuita Yesu ‘muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote’ vya Mungu.​—Soma Wakolosai 1:15, 16.

Yesu aliishi mbinguni akiwa kiumbe wa roho mbele ya kuzaliwa huko Bethlehemu. Wakati ulipofika ili Yesu azaliwe kama mwanadamu, Mungu alihamisha uzima wa Yesu kutoka mbinguni na kuuweka ndani ya tumbo la uzazi la Maria.​—Soma Luka 1:30-32; Yohana 6:38; 8:23.

Sababu gani Mungu aliruhusu Yesu azaliwe kama mwanadamu duniani? Yesu alitimiza daraka gani la pekee? Unaweza kupata majibu kwa maulizo hayo katika Biblia, na majibu hayo yatakusaidia sana kuongeza ujuzi wako na shukurani yako juu ya mambo ambayo Mungu na Yesu wamefanya kwa ajili yako.