Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA: INAWEZEKANA KUWA NA MAISHA YENYE MAANA

Je, Inawezekana Kabisa Kuwa na Maisha Yenye Maana?

Je, Inawezekana Kabisa Kuwa na Maisha Yenye Maana?

‘Jumla ya miaka yetu ndiyo makumi saba,​—tukiwa na afya njema, makumi munane. Na mingi ya hiyo ni taabu na shida.’​—Zaburi 90:10, Verbum Bible.

MANENO hayo ni ya kweli kabisa! Maisha katika dunia hii mara nyingi yanajaa “taabu na shida.” Labda umekwisha kujiuliza, ‘Je, inawezekana kweli kuwa na maisha yenye maana leo?’

Chukua mufano wa Maria. Sikuzote, alikuwa mutu mwenye bidii, lakini sasa akiwa na miaka 84, hawezi tena kujitosha nyumbani. Akili yake ingali inatumika vizuri, lakini hana tena nguvu za kimwili. Namna gani anaweza kuona kuwa maisha kama hayo yana maana?

Namna gani wewe? Inawezekana wakati fulani umekwisha kujiuliza ikiwa maisha yako yana maana. Labda unafanya kazi ile-ile na ni yenye kuchosha. Inawezekana watu wengine hawaone bidii ao kazi yako kuwa ya maana. Hata ikiwa unapata matokeo mazuri kwa njia fulani, unaweza kuwa na wasiwasi kuhusu wakati wako unaokuja. Wakati fulani, unaweza kujisikia kuwa peke yako ao mwenye kuvunjika moyo. Maisha ya familia yako yanaweza kuwa yenye kujaa magomvi na mabishano. Labda umefiwa na mutu uliyemupenda sana. Mwanaume mumoja anayeitwa André alikuwa anapendana sana na baba yake, ambaye aligonjwa mara moja na akakufa. Hilo lilikuwa pigo kubwa kwa André, na aliona kwamba hawezi kabisa kupambana na hali hiyo ngumu.

Hata iwe tunapambana na shida gani, jambo fulani la lazima ambalo tunahitaji kujua ni hili: Je, inawezekana kabisa kuwa na maisha yenye maana? Tunaweza kupata jibu kwa kuchunguza maisha ya mwanaume aliyeishi duniani kumepita miaka 2000 hivi, mwanaume huyo ni Yesu Kristo. Ijapokuwa alipambana na matatizo mengi, kwa kweli maisha yake yalikuwa yenye maana. Tukifuata mufano wake, maisha yetu pia yanaweza kuwa yenye maana.