Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
Je, inawezekana kuelewa Biblia?
Biblia ni Neno la Mungu. Ni kama barua inayotoka kwa baba mwenye upendo. (2 Timotheo 3:16) Katika Biblia, Mungu anaeleza namna tunavyoweza kumupendeza, sababu gani anaacha mambo mabaya, na mambo ambayo atawafanyia watu wakati unaokuja. Lakini walimu wa dini wamegeuza mafundisho ya Biblia; na hilo linafanya watu wengi wawaze kwamba hawawezi hata kidogo kuielewa.—Matendo 20:29, 30.
Yehova Mungu anataka tujue kweli juu yake. Ndiyo sababu ametupatia kitabu ambacho tunaweza kuelewa.—Soma 1 Timotheo 2:3, 4.
Namna gani unaweza kuelewa Biblia?
Zaidi ya kutupatia Biblia, Yehova anatutolea musaada ili kuielewa. Alimutuma Yesu ili kutufundisha. (Luka 4:16-21) Yesu aliwasaidia wasikilizaji wake kuelewa Maandiko, alikuwa anataja andiko baada ya lingine.—Soma Luka 24:27, 32, 45.
Yesu alianzisha kutaniko la Kikristo ili kazi aliyokuwa ameanzisha iendelee. (Mathayo 28:19, 20) Leo, wafuasi wa kweli wa Yesu wanasaidia watu kuelewa yale ambayo Biblia inafundisha juu ya Mungu. Ikiwa unapenda kuelewa Biblia, Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia.—Soma Matendo 8:30, 31.