Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Je, inawezekana kuelewa Biblia?

Biblia ni Neno la Mungu. Ni kama barua inayotoka kwa baba mwenye upendo. (2 Timotheo 3:16) Katika Biblia, Mungu anaeleza namna tunavyoweza kumupendeza, sababu gani anaacha mambo mabaya, na mambo ambayo atawafanyia watu wakati unaokuja. Lakini walimu wa dini wamegeuza mafundisho ya Biblia; na hilo linafanya watu wengi wawaze kwamba hawawezi hata kidogo kuielewa.​—Matendo 20:29, 30.

Yehova Mungu anataka tujue kweli juu yake. Ndiyo sababu ametupatia kitabu ambacho tunaweza kuelewa.​—Soma 1 Timotheo 2:3, 4. 

Namna gani unaweza kuelewa Biblia?

Zaidi ya kutupatia Biblia, Yehova anatutolea musaada ili kuielewa. Alimutuma Yesu ili kutufundisha. (Luka 4:16-21) Yesu aliwasaidia wasikilizaji wake kuelewa Maandiko, alikuwa anataja andiko baada ya lingine.​—Soma Luka 24:27, 32, 45.

Yesu alianzisha kutaniko la Kikristo ili kazi aliyokuwa ameanzisha iendelee. (Mathayo 28:19, 20) Leo, wafuasi wa kweli wa Yesu wanasaidia watu kuelewa yale ambayo Biblia inafundisha juu ya Mungu. Ikiwa unapenda kuelewa Biblia, Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia.​—Soma Matendo 8:30, 31.