Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tumia Neno la Mungu Ili Kujisaidia na Kuwasaidia Wengine

Tumia Neno la Mungu Ili Kujisaidia na Kuwasaidia Wengine

“Nimeyaona maagizo yote juu ya mambo yote kuwa ni sawa.”​—ZAB. 119:128.

1. Sababu gani tunapaswa kutumaini kabisa Neno la Mungu?

 WAZEE wanapochunguza ikiwa mwanafunzi fulani wa Biblia anastahili kuwa muhubiri, wanajiuliza hivi: ‘Je, maelezo yake yanaonyesha kama anaamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu lililoongozwa na roho?’ * Watumishi wote wa Mungu wanaamini hivyo, na yule anayetaka kuwa muhubiri wa Ufalme anapaswa kuamini hivyo. Sababu gani? Ikiwa tunatumaini kabisa Neno la Mungu na kulitumia kwa ufundi katika mahubiri, mambo hayo yatatuwezesha kuwasaidia wengine wamujue Yehova na kuweza kuokolewa.

2. Sababu gani tunapaswa ‘kuendelea katika mambo tuliyojifunza’?

2 Mutume Paulo alikazia umaana wa Neno la Mungu alipomuandikia Timotheo hivi: “Endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini.” “Mambo” ambayo mutume Paulo alizungumuzia hapa ni mafundisho ya Biblia yaliyomufanya Timotheo aamini habari njema. Mafundisho hayo yametusaidia sisi pia leo, na yanaendelea kutusaidia tuwe wenye “hekima kwa ajili ya wokovu.” (2 Tim. 3:14, 15) Tunatumia kila mara maneno ambayo Paulo alisema katika mustari unaofuata ili kuwaonyesha wengine kwamba Biblia ni Neno la Mungu, lakini sisi wenyewe tunaweza kupata faida katika maneno hayo yanayopatikana kwenye 2 Timotheo 3:16. (Soma.) Acheni tuzungumuzie andiko hilo kwa urefu. Kufanya hivyo kutatia nguvu tumaini letu kwamba mafundisho yote ya Yehova ni “sawa.”​—Zab. 119:128.

“LENYE FAIDA KWA KUFUNDISHA”

3-5. (a) Watu wengi walifanya nini waliposikia hotuba ya mutume Petro kwenye Pentekoste, na sababu gani? (b) Sababu gani watu wengi walikubali kweli huko Thesalonika? (c) Ni jambo gani linalowashangaza watu wengi tunapowahubiria?

3 Yesu aliwaambia Waisraeli hivi: “Ninatuma kwenu manabii na watu wenye hekima na wafundishaji wa watu wote.” (Mt. 23:34) Yesu alikuwa akizungumuzia wanafunzi wake, ambao alifundisha kutumia Maandiko katika mahubiri. Mutume Petro, aliyekuwa mumoja wa hao “wafundishaji wa watu wote,” alitaja maandiko mengi ya Kiebrania katika hotuba ambayo alitolea watu wengi kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33. Wasikilizaji wengi “walichomwa moyoni” waliposikia namna Petro alivyofasiria maandiko hayo. Kwa hiyo, walitubu zambi zao. Watu elfu tatu hivi kati yao walitafuta musamaha wa Mungu na wakawa Wakristo.​—Mdo. 2:37-41.

4 Mutume Paulo, aliyekuwa mufundishaji mwingine wa watu wote, alihubiri habari njema katika miji iliyokuwa mbali na Yerusalemu. Kwa mufano, aliwahubiria wale waliokuwa wakiabudu katika sinagogi moja la muji wa Thesalonika, huko Makedonia. Kwa Sabato tatu, Paulo ‘alijadiliana nao kwa kutumia Maandiko, akieleza na kusibitisha kwa marejeo kwamba ilikuwa lazima Kristo ateseke na kufufuliwa kutoka kwa wafu.’ Matokeo yalikuwa nini? ‘Baazi yao [Wayahudi] wakawa waamini,’ vilevile ‘umati mukubwa kati ya Wagiriki.’​—Mdo. 17:1-4.

5 Wengi leo wanashangaa kuona namna watumishi wa Mungu wanavyotumia Biblia. Dada wawili huko Suisse walikuwa katika mahubiri. Mumoja wao alipomusomea mwenye-nyumba fulani andiko moja, mutu huyo aliuliza hivi: “Ninyi ni wa dini gani?” Dada yetu alijibu hivi: “Sisi ni Mashahidi wa Yehova.” Kisha mutu huyo alisema hivi: “Sikupaswa hata kuuliza. Isipokuwa Mashahidi wa Yehova, nani mwengine anaweza kuja nyumbani hivi na kunisomea Biblia?”

6, 7. (a) Namna gani wale wanaofundisha kutaniko wanaweza kutumia maandiko vizuri? (b) Sababu gani ni jambo la lazima kutumia maandiko vizuri tunapoongoza mafunzo ya Biblia?

6 Namna gani tunaweza kutumia Biblia zaidi tunapofundisha? Ikiwa una pendeleo la kufundisha kutaniko, tumia maandiko yanayopatana na mambo unayozungumuzia. Kuliko tu kutaja maneno ya andiko, ao kutumia maandiko yaliyoandikwa tayari kwenye karatasi, ao kusoma andiko kwenye chombo cha kielektroniki kama vile ordinatere, fungua Biblia na usome andiko, na uwatie moyo wasikilizaji kufanya hivyo. Zaidi ya hayo, chukua wakati ili kuonyesha wasikilizaji namna wanavyoweza kutumia maandiko hayo ili kumukaribia Yehova zaidi. Kuliko kutumia mifano isiyoeleweka ao mambo ambayo ndugu walikutana nayo ya kuchekesha tu, tumia wakati huo ili kufasiria Neno la Mungu.

7 Tunapaswa kukumbuka nini tunapoongoza mafunzo ya Biblia? Tunaposoma vichapo vinavyotegemea Biblia, tunapaswa kusoma maandiko yote yanayoonyeshwa. Tunapaswa kumutia moyo mwanafunzi asome maandiko yanayotajwa na kumusaidia ayaelewe. Namna gani? Si kwa kutoa mafasiriyo marefu kama mutu anayetoa hotuba, lakini kwa kumutia moyo atoe maoni yake. Kuliko kumuambia mambo anayopaswa kuamini ao namna anavyopaswa kutenda, tunapaswa kumuuliza maulizo yanayomufanya mutu afikiri na ambayo yatamusaidia achukue maamuzi yanayofaa. *

“LENYE FAIDA . . . KWA KUKARIPIA”

8. Mutume Paulo alipambana na nini katika viungo vyake?

8 Wengi wanafikiri kwamba “kukaripia” ni daraka la wazee wa kutaniko tu. Bila shaka, wazee wana daraka la ‘kukaripia wale wanaofanya zambi.’ (1 Tim. 5:20; Tito 1:13) Lakini, sisi wenyewe tunapaswa pia kujikaripia. Mutume Paulo alikuwa Mukristo aliyekuwa na zamiri safi. (2 Tim. 1:3) Hata hivyo, aliandika hivi: ‘Ninaona ndani ya viungo vyangu sheria nyingine ikipigana na sheria ya akili yangu na kunichukua mateka kwa sheria ya zambi.’ Ikiwa tunajifunza sababu zilizomusukuma kuandika maneno hayo, tutaelewa vizuri zaidi vita ambayo Paulo alipaswa kupigana ili kuzuia tamaa ya mwili wake wenye zambi.​—Soma Waroma 7:21-25.

9, 10. (a) Inawezekana mutume Paulo alipambana na uzaifu gani? (b) Labda mutume Paulo alipambana na hali yake ya kutokamilika namna gani?

9 Paulo alijikaza kushinda uzaifu gani? Hata ikiwa hakutaja uzaifu wake mbalimbali, alimuandikia Timotheo kwamba hapo zamani yeye alikuwa ‘mutu mwenye zarau.’ (1 Tim. 1:13) Mbele ya kuwa Mukristo, mutume Paulo aliwatesa kwa ukali Wakristo. Alisema hivi waziwazi kuhusu namna alivyowaona wanafunzi wa Yesu: ‘Niliwaonea hasira kama mwenye wazimu.’ (Mdo. 26:11Union Version) Mutume Paulo alijifunza kujizuia, hata ikiwa wakati fulani alishindwa kuzuia hasira na maneno yake. (Mdo. 15:36-39) Ni nini kilichomusaidia?

10 Katika barua yake kwa Wakristo wa Korintho, mutume Paulo alizungumuzia njia aliyotumia ili kujikaripia. (Soma 1 Wakorintho 9:26, 27.) Alijipigapiga ili kupambana na hali yake ya kukosa kukamilika. Bila shaka, alitafuta mashauri katika Maandiko, aliomba Yehova amusaidie kuyatumikisha, na alijikaza sana kufanya mabadiliko. * Mufano wake unaweza kutusaidia kwa sababu sisi pia tunapambana na hali yetu ya kukosa kukamilika.

11. Namna gani tunaweza ‘kuendelea kujijaribu’ wenyewe ili kuona ikiwa tunaendelea kutembea kabisa katika kweli?

11 Hatupaswe kujisikia kuwa tumetosheka. Lakini, tunapaswa ‘kuendelea kujijaribu’ ili kuona ikiwa tunaendelea kutembea kabisa katika kweli. (2 Kor. 13:5) Tunaposoma maandiko kama vile Wakolosai 3:5-10, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Je, ninafanya yangu yote ili kuua tamaa ao mwelekeo wangu wa zambi ao nimeanza kujiendesha vibaya? Picha chafu zinapojitokeza wakati ninatumia Internete, je, ninafunga adresi hiyo, ao ninatafuta kimakusudi adresi zinazoonyesha picha hizo?’ Kutumia mashauri ya Neno la Mungu katika njia hiyo kutatusaidia “tukae macho na kutunza akili zetu.”​—1 Thes. 5:6-8.

“LENYE FAIDA . . . KWA KUNYOOSHA MAMBO”

12, 13. (a) ‘Kunyoosha mambo’ kunapaswa kuwa na kusudi gani, na namna gani tunaweza kuiga Yesu tunapofanya hivyo? (b) Tunapaswa kuepuka maneno ya namna gani ‘tunaponyoosha mambo’ pamoja na wengine?

12 Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “kunyoosha mambo” linamaanisha “kutengeneza, kusahihisha, kurudisha katika hali nzuri.” Wakati fulani, tunapaswa kuchukua hatua ili kunyoosha mambo na wale wanaotuelewa vibaya ao kuelewa vibaya matendo yetu. Kwa mufano, viongozi wa dini ya Wayahudi walinungunika kwa kusema kwamba Yesu alikuwa rafiki ya ‘wakusanya​-kodi na watenda​-zambi.’ Yesu aliwajibu hivi: “Watu wenye afya hawahitaji tabibu [muganga], bali wenye kuugua ndio wanaomuhitaji. Nendeni, basi, mukajifunze maana ya jambo hili, ‘Ninataka rehema, wala si zabihu.’” (Mt. 9:11-13) Yesu aliwaelezea watu wote Neno la Mungu kwa upole na uvumilivu. Kwa hiyo, watu wanyenyekevu walianza kutambua kwamba Yehova ni ‘Mungu mwenye rehema na neema, si mwepesi wa hasira naye ni mwingi wa fazili zenye upendo na kweli.’ (Kut. 34:6) Kwa kuwa Mwana wa Mungu alijikaza ‘kunyoosha mambo,’ wengi walianza kuamini habari njema.

13 Mufano wa Yesu unatufundisha namna tunavyoweza kuwasaidia wengine. Mutu fulani mwenye hasira anaweza kusema hivi kwa ukali, ‘Ninataka tumalize matatizo yetu sasa hivi.’ Lakini kufanya hivyo hakupatane na andiko la 2 Timotheo 3:16. “Kila andiko” halituruhusu kuongea na wengine kwa ukali. Kama “upanga unaochoma,” maneno ya ukali yanaumiza sana na hayana faida hata moja.​—Met. 12:18.

14-16. (a) Namna gani wazee wanaweza ‘kunyoosha mambo’ katika njia itakayowasaidia wengine watatue matatizo yao? (b) Sababu gani ‘kunyoosha mambo’ kama inavyoombwa na Maandiko ni kwa lazima sana wakati wazazi wanapolea watoto wao?

14 Kwa hiyo, namna gani tunaweza kuonyesha uvumilivu na upole ‘tunaponyoosha mambo’? Wazia bibi na bwana wanaomuomba muzee wa kutaniko mashauri ili kumaliza mabishano yao ya kila siku. Muzee huyo anaweza kufanya nini? Bila kupendelea upande fulani, anaweza kufikiri nao kuhusu kanuni za Biblia, labda kwa kutumia kanuni zinazopatikana katika sura ya 3 ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Muzee anapoongea nao, kila mumoja wao anaweza kutambua ni shauri gani atakalotumikisha vizuri zaidi. Katika siku zinazofuata, muzee huyo anaweza kuwauliza kama mambo yanaendelea namna gani katika familia yao na kuwatolea musaada mwingine ikiwa wanauhitaji.

 15 Namna gani wazazi wanaweza ‘kunyoosha mambo’ katika njia itakayofanya watoto wao wawe nguvu kiroho? Wazia kwamba unataka kumusaidia binti yako aepuke marafiki wabaya. Kwanza, unapaswa kuwajua marafiki wake. Kisha, ikiwa ana marafiki wabaya, unaweza kuongea naye, labda kwa kutumia mawazo ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2. Katika siku zinazofuata, unaweza kupitisha wakati mwingi pamoja naye. Unaweza pia kutazama hali yake anapohubiri na anapojifurahisha na washiriki wengine wa familia. Ikiwa unatenda kwa uvumilivu na upole, binti yako atatambua kwamba unamupenda kabisa. Labda hilo litamusaidia atumikishe mashauri yako ili kuepuka mambo yanayoweza kumuletea matatizo katika maisha.

Ikiwa wazazi wanatumia Biblia kwa upole ili ‘kunyoosha mambo’ wanapolea watoto wao, hilo linaweza kuwasaidia watoto waepuke matatizo mengi

16 Tunapaswa pia kutenda kwa uvumilivu na upole tunapowatia moyo wale wanaopambana na magonjwa, wale waliovunjika moyo kisha kupoteza kazi, ao wale walio na mashaka kuhusu fundisho fulani la Maandiko. Kutumia Neno la Mungu ili ‘kunyoosha mambo’ kunatuletea faida nyingi.

‘LENYE FAIDA . . . KWA KUTIA NIZAMU KATIKA UADILIFU’

17. Sababu gani tunapaswa kufurahia nizamu?

17 ‘Hakuna nizamu inayoonekana kwa sasa kuwa yenye shangwe.’ Hata hivyo, “baadaye kwa wale ambao wamezoezwa nayo hiyo huzaa tunda lenye kufanya amani.” (Ebr. 12:11) Wakristo wengi ambao wamekuwa watu wazima sasa wanakubali kwamba nizamu waliyopewa na wazazi wao Wakristo imewasaidia. Pia, kukubali nizamu ambayo Yehova anatutolea kupitia wazee kunatusaidia kubaki katika barabara inayoongoza kwenye uzima.​—Met. 4:13.

18, 19. (a) Sababu gani tunapaswa kufuata shauri la Methali 18:13 ili ‘kutia nizamu katika uadilifu’? (b) Mambo yanakuwa namna gani wakati wazee wanawatendea kwa upole na upendo wale ambao wamefanya zambi nzito?

18 Inaomba kuwa na ufundi fulani ili kutoa nizamu yenye matokeo. Yehova anawaomba Wakristo wafanye hivyo “katika uadilifu.” (2 Tim. 3:16) Kwa hiyo, inaomba kutumia kanuni za Biblia. Moja ya kanuni hizo inapatikana katika andiko la Methali 18:13: “Yeyote anapojibu jambo kabla ya kulisikia, huo ni upumbavu na aibu [ao haya] kwake.” Kwa hiyo, wazee wanapotaka kuzungumuza na mutu ambaye inasemekana kwamba amefanya zambi nzito, wanapaswa kufanya uchunguzi ili kujua mambo vizuri. (Kum. 13:14) Hilo litawasaidia kutoa nizamu “katika uadilifu.”

19 Zaidi ya hilo, Neno la Mungu linawaomba wazee wawashauri wengine “kwa upole.” (Soma 2 Timotheo 2:24-26.) Kwa kweli, mukosaji anaweza kulaumisha jina la Yehova na zambi yake inaweza kuwaumiza watu wasio na kosa. Hata hivyo, muzee hatamusaidia hata kidogo mukosaji kama huyo ikiwa anamutolea mashauri kwa ukali. Lakini, wazee wanaweza kumuchochea yule ambaye amefanya zambi nzito atubu ikiwa wanaiga ‘sifa ya fazili ya Mungu.’​—Rom. 2:4.

20. Wazazi wanapaswa kutumia kanuni gani wanapotolea watoto wao nizamu?

20 Wazazi wanapaswa kutumikisha kanuni za Biblia wanapowalea watoto wao ‘katika nizamu na muongozo wa akilini wa Yehova.’ (Efe. 6:4) Baba anapaswa kuepuka kutoa malipizi ikiwa hajasikia habari zote kuhusu kosa la mutoto. Na wazazi Wakristo hawapaswe kutenda kwa hasira kali. “Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema,” na wote walio na daraka la kutolea watoto nizamu wanapaswa kujikaza kuonyesha sifa hizo.​—Yak. 5:11.

YEHOVA AMETUPA ZAWADI NZURI SANA

21, 22. Ni maneno gani katika andiko la Zaburi 119:97-104 yanayoonyesha vizuri namna tunavyoliona Neno la Yehova?

21 Siku fulani, mwanaume mumoja mwenye kumuogopa Mungu alionyesha sababu gani aliipenda sheria ya Yehova. (Soma Zaburi 119:97-104.) Kwa kujifunza sheria hiyo, alipata hekima na ufahamu. Kutumikisha mashauri ya Mungu kulimuepusha na matendo mabaya yanayowaumiza wengine. Aliona kujifunza Maandiko kuwa jambo la kufurahisha na lenye kutosheleza. Aliazimia kutii maagizo ya Mungu ambayo yalikuwa yamemusaidia sana katika maisha yake.

22 Je, unaliona “kila Andiko” kuwa la maana? Kila andiko linatusaidia kuamini kabisa kwamba Mungu atatimiza kusudi lake. Mashauri yake yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanatulinda na matokeo mabaya ya kuzoea zambi. Na ikiwa tunatumia Biblia kwa ufundi tunapoifasiria watu, tunaweza kuwasaidia waione barabara inayoongoza kwenye uzima na kubaki ndani yake. Acheni tutumie zaidi “kila Andiko” tunapomutumikia Yehova, Mungu mwenye hekima yote na mwenye upendo.

^ Soma kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 80.

^ Alipokuwa akifundisha, Yesu alizoea kuwauliza wasikilizaji wake hivi: ‘Munaonaje?’ Kisha alisikiliza majibu yao.​—Mt. 18:12; 21:28; 22:42.

^ Barua za Paulo zina mashauri mengi yanayoweza kututia moyo ili kushinda tamaa ao mielekeo mbalimbali ya zambi. (Rom. 6:12; Gal. 5:16-18) Tunaweza kusema kwamba yeye mwenyewe alitumikisha mashauri aliyowatolea watu wengine.​—Rom. 2:21.

(Soma  kifungo cha 15)