Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MASIMULIZI KUHUSU MAISHA YA WATU

Maisha Yetu Yamekuwa na Kusudi Nzuri

Maisha Yetu Yamekuwa na Kusudi Nzuri

KISHA tu mwana wangu Gary kuzaliwa katika mwaka wa 1958, nilitambua kwamba alikuwa na tatizo fulani la afya. Hata hivyo, ilichukua miezi kumi ili waganga wavumbue ugonjwa wake na miaka mingine mitano ili waganga wa Londres wahakikishe kwamba ana ugonjwa. Nilihuzunika sana wakati binti wangu Louise, aliyezaliwa miaka kenda kisha kuzaliwa kwa Gary, alioonyesha alama nyingi za ugonjwa huo kuliko Gary.

Waganga waliniambia hivi kwa utulivu: “Watoto wako wote wawili wana ugonjwa wa LMBB, * na ugonjwa huo hauna dawa kwa sasa.” Wakati huo, waganga hawakujua mengi kuhusu ugonjwa huo wa chembe za uriti. Alama za ugonjwa huo ni matatizo ya kuona yanayoweza kumufanya mutu awe kipofu, kunenepa sana, kuwa na vidole vingi vya mukono ao muguu, kukomaa polepole, viungo vya mwili havifanye kazi kwa upatano, diabete, ugonjwa wa mifupa kwa sababu ya kukosa maji katika maunganisho na ugonjwa wa figo. Kwa hiyo, haikuwa rahisi kwangu kushugulikia watoto wangu. Utafiti fulani wa hivi karibuni, unaonyesha kama mutu mumoja kati ya watu 125 000 katika Grande-Bretagne ana ugonjwa huo, lakini wengine wanaweza kuwa na ugonjwa huo katika njia isiyoonekana wazi.

YEHOVA ANAKUWA “KILELE CHETU SALAMA”

Kisha tu kuolewa, nilizungumuza na dada mumoja, na mara moja nikavumbua kwamba Mashahidi wa Yehova wanafundisha kweli. Lakini bwana yangu hakupendezwa na jambo hilo hata kidogo. Kwa sababu ya kazi yake, tulikuwa tukihama-hama, kwa hiyo, sikubaki hata katika kutaniko moja. Lakini, niliendelea kusoma Biblia na kusali kwa Yehova. Nilifarijiwa sana niliposoma kwamba ‘Yehova atakuwa kilele salama kwa ajili ya mutu yeyote aliyekandamizwa, kilele salama wakati wa taabu’ na kwamba ‘hakika hatawaacha wale wanaomutafuta.’​—Zab. 9:9, 10.

Gary hakuwa naona vizuri, kwa hiyo alipokuwa na miaka sita, tulimutuma kwenye masomo ambako wanafunzi wanaishi kusini mwa Angleterre ili apate mafunzo ya pekee. Alikuwa akiniita kwa ukawaida kupitia telefone ili kunielezea matatizo yake, na nilimusaidia kuelewa namna anavyoweza kutumia kanuni za musingi za Biblia. Miaka kidogo baadaye Louise, alizaliwa; mimi mwenyewe nilipata magonjwa ya neva ao mishipa ya ubongo na ugonjwa unaofanya maunganisho ya mwili yakose maji unaoitwa fibromyalgie. Gary alirudi nyumbani alipokuwa na miaka 16. Lakini uwezo wake wa kuona uliendelea kupunguka, na katika mwaka wa 1975 alikuwa kipofu. Katika mwaka wa 1977, bwana yangu alituacha na kututupilia.

Muda kidogo tu kisha Gary kurudi, tulijitoa sana katika utendaji mbalimbali wa kutaniko moja ambamo mulikuwa ndugu na dada waliotupenda, na katika mwaka wa 1974 nilibatizwa. Nilishukuru sana wakati muzee mumoja wa kutaniko alimusaidia Gary kupambana na mabadiliko yake ya miaka ya ujana. Ndugu na dada wengine walinisaidia kufanya kazi za nyumbani, na shirika moja la ulimwengu linalowasaidia watu liliwalipa Mashahidi watano ili watusaidie nyumbani. Tulibarikiwa kabisa!

Gary aliendelea vizuri katika kweli na alibatizwa katika mwaka wa 1982. Alipenda sana kuwa painia musaidizi. Kwa hiyo, niliamua kufanya kazi hiyo pamoja naye na tuliifanya kwa miaka mingi. Mwana wangu alifurahi sana wakati mwangalizi wetu wa muzunguko alimuuliza hivi: “Gary, kwa nini haujakuwa painia wa kawaida?” Maneno hayo yalikuwa kitia moyo ambacho Gary alihitaji, na alianza kazi ya upainia wa kawaida katika 1990.

Gary alikuwa na vyombo viwili vya kutegemeza kiuno chake, chombo cha kwanza kilitiwa katika 1999 na chombo cha pili katika 2008, lakini afya ya Louise iliendelea kuharibika zaidi na zaidi. Yeye alizaliwa akiwa kipofu kabisa, na nilipoona kidole cha zaidi kwenye muguu wake, nilitambua kwamba yeye pia amezaliwa na ugonjwa wa LMBB. Uchunguzi wa afya ulionyesha kama alikuwa na matatizo mengi katika viungo vyake. Kwa miaka mingi, alifanyiwa aina mbalimbali za upasuaji, kutia ndani upasuaji tano wa figo. Kama Gary, yeye pia alikuwa na diabete.

Louise alijua kama upasuaji unatokeza matatizo mengi. Kwa hiyo, aliwaambia mbele ya wakati waganga wanaofanya upasuaji na wale wanaotia dawa inayopoteza ufahamu na wasimamizi wa hopitali, uamuzi wake kuhusu matunzo yasiyotumia damu. Kwa hiyo, alikuwa na uhusiano muzuri na wote waliohangaikia kwa njia nzuri afya yake.

MAISHA YENYE KUSUDI NZURI

Tunafanya mambo mengi katika nyumba yetu ili kumuabudu Yehova. Zamani, mbele ya sisi kuwa na vyombo vya kielektroniki niliwasomea Gary na Louise vitabu kwa saa nyingi. Kwa sasa CD, DVD, na mambo mengine tunayochukua kwenye www.pr418.com yanatusaidia sisi wote kuwa na programe nzuri ya kujifunza Biblia kila juma kwa wakati tofauti-tofauti, na hilo linatusaidia tutoe maelezo kwenye mikutano yetu.

Tunamushukuru sana Yehova kwa kututolea kweli zenye kupendeza sana katika Neno lake!

Wakati mwengine Gary anajikaza kuchunga katika akili majibu atakayotoa kwenye mikutano, na anapokuwa na hotuba katika Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi, anaweza kuitoa kwa kutumia maneno yake mwenyewe. Gary alikuwa mutumishi wa huduma katika 1995 na anaendelea kufanya mengi kwenye Jumba la Ufalme, anatumika kwenye ukaribishaji na anasaidia kutumia vyombo vya sauti.

Ndugu na dada wanamusindikiza Gary katika mahubiri, mara nyingi wakimusukuma kwenye kiti cha vilema anachotumia kwa sababu ya ugonjwa wake wa mifupa. Ndugu mumoja amemusaidia kuongoza funzo la Biblia na mwanaume mumoja aliyependezwa. Pia, Gary amemutia moyo dada mumoja ambaye alikuwa asiyetenda muda wa miaka 25. Mwanaume huyo aliyependezwa na dada huyo wanakusanyika sasa.

Louise alipokuwa na miaka kenda, tate ao nkambo yake mwanamuke alimufundisha kusuka nguo kwa kutumia uzi, na mumoja kati ya wale waliomutunza na mimi tulimufundisha kutia mapambo kwenye nguo. Kwa kuwa alifurahia sana kazi ya kusuka nguo, alisuka blangeti zenye kupambwa vizuri kwa ajili ya watoto na watu wenye kuzeeka walio katika kutaniko letu. Anatengeneza pia karte za salamu, akibandika picha kwenye karte hizo. Wale wanaopokea karte hizo wanazisamini sana. Katika ujana wake, Louise alijifunza kuandika na ordinatere bila kuona. Kwa Sasa anatumia ordinatere ya pekee inayotoa sauti, na anapashana habari na wenzake kupitia Internete. Louise alibatizwa alipokuwa na miaka 17. Wakati wa kampanye za pekee za mahubiri, mimi naye tunafanya upainia musaidizi. Kama Gary, Louise anajikaza kuweka katika akili maandiko anayoweza kutumia ili kuzungumuzia ahadi za Mungu kuhusu ulimwengu ambamo “macho ya vipofu yatafunguliwa” na ambamo “hakuna mukaaji atakayesema: ‘Mimi ni mugonjwa.’”​—Isa. 33:24; 35:5.

Tunamushukuru sana Yehova kwa kututolea kweli zenye kupendeza sana katika Neno lake! Mioyo yetu ni yenye shukrani sana tunapoona namna kutaniko linavyotutegemeza kabisa, kwa sababu bila musaada huo, hatungeweza kufanya mengi tunayofanya leo. Maisha yetu yamekuwa na kusudi nzuri zaidi sana kwa sababu ya musaada wa Yehova.

^ Jina la ugonjwa wa LMBB lilitokana na majina ya waganga wane, Laurence​-Moon-​Bardet-​Biedl, waliovumbua ugonjwa huo wa chembe za uriti, ambao mutu anariti wakati wazazi wake wawili wana chembe za ugonjwa huo. Leo, unaitwa ugonjwa wa Bardet-Biedl, na hauna dawa.