Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Kwa nini hakuna amani duniani?

Serikali inayoweza kubadili mioyo ya watu ndiyo tu inayoweza kuleta amani duniani

Biblia inataja sababu mbili kuu. Kwanza, ingawa wanadamu wametimiza mambo yenye kustaajabisha, hawakuumbwa wakiwa na uwezo wa kujiongoza. Pili, jitihada za wanadamu zimeshindwa kufanikiwa kwa sababu “ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu,” Shetani Ibilisi. Hivyo basi, jitihada za wanadamu zimeshindwa kuleta amani duniani.Soma Yeremia 10:23; 1 Yohana 5:19.

Pia, ubinafsi na kujitakia makuu kumefanya amani isipatikane duniani. Serikali ya duniani pote inayowafundisha watu kupenda mema na kuwa wenye kujali ndiyo tu inayoweza kuleta amani duniani.Soma Isaya 32:17; 48:18, 22.

Ni nani atakayeleta amani duniani?

Mungu Mweza-Yote ameahidi kuleta serikali moja itakayotawala wanadamu wote. Itachukua mahali pa serikali za kibinadamu. (Danieli 2:44) Yesu, Mwana wa Mungu, atatawala akiwa Mkuu wa Amani. Ataondoa uovu wote duniani na atawafundisha watu kuishi kwa amani.Soma Isaya 9:6, 7; 11:4, 9.

Tayari mamilioni ya watu ulimwenguni pote wanatii mwongozo wa Yesu na wanatumia Neno la Mungu, Biblia, kuwafundisha watu jinsi ya kuishi kwa amani. Hivi karibuni, kutakuwa na amani duniani kote.Soma Isaya 2:3, 4; 54:13.