Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Ni Mukarimu na Mwenye Usawaziko

Yehova Ni Mukarimu na Mwenye Usawaziko

“Yehova ni mwema kwa wote, Na rehema zake ziko juu ya kazi zake zote.”​—ZAB. 145:9.

1, 2. Marafiki wa Yehova watakuwa na nafasi gani?

 DADA Monika ambaye amefanya miaka 35 hivi katika ndoa anasema hivi: “Mimi na bwana yangu tunajuana vizuri sana. Lakini, hata kisha miaka hiyo, kila mumoja wetu angali anavumbua juu ya mwenzake mambo fulani ambayo hakujua hapo mbele.” Bila shaka, wengi wanaweza kusema hivyo kuhusu bibi, bwana, ao rafiki yao.

2 Tunataka kuwajua vizuri wale tunaowapenda. Tunaweza kuanzisha urafiki na watu wengi, hata hivyo, urafiki wetu na Yehova ndio wa maana zaidi. Hakuna hata siku moja ambayo tutajua mambo yote kumuhusu Yehova. (Rom. 11:33) Tutakapopata uzima wa milele, tutakuwa na nafasi ya kuendelea kujifunza mengi juu ya sifa za Yehova na tutaendelea kupendezwa sana na sifa hizo.​—Mhu. 3:11.

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Habari iliyotangulia ilitusaidia kupendezwa sana na sifa ya Yehova ya kukaribiwa kwa urahisi na kutokuwa na ubaguzi. Acheni sasa tuzungumuzie sifa zingine mbili za Yehova zenye kuvutia​—ukarimu na usawaziko wake. Kufanya hivyo kutatusaidia kutambua vizuri zaidi namna “Yehova ni mwema kwa wote na rehema zake ziko juu ya kazi zake zote.”​—Zab. 145:9.

YEHOVA NI MUKARIMU

4. Ukarimu wa kweli unamaanisha nini?

4 Kuwa mukarimu kunamaanisha nini? Maneno ya Yesu yanayopatikana katika Matendo 20:35 yanajibu ulizo hilo. “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” Kupitia maneno hayo rahisi, Yesu alitoa kabisa maana ya ukarimu wa kweli. Mutu mukarimu anatoa bila kulazimishwa wakati wake, nguvu, na mali yake ili kuwasaidia wengine, na anafanya hivyo kwa furaha. Bila shaka, ukarimu si kutoa zawadi kubwa ao nyingi, lakini ni kutoa kwa nia nzuri. (Soma 2 Wakorintho 9:7.) Yehova “Mungu mwenye furaha” ndiye mukarimu zaidi kuliko watu wote.​—1 Tim. 1:11.

5. Namna gani Yehova anaonyesha ukarimu?

5 Namna gani Yehova anaonyesha ukarimu ao sifa ya kutoa? Yehova anawatimizia wanadamu wote mahitaji yao, hata wale ambao hawajaanza kumuabudu. Bila shaka, “Yehova ni mwema kwa wote.” Yeye ‘analichomoza jua lake juu ya watu waovu na wema na ananyesha mvua juu ya watu waadilifu na wasio waadilifu.’ (Mt. 5:45) Kwa sababu alijua hivyo, mutume Paulo, aliwaambia wasioamini kwamba Yehova ‘alitenda mema, aliwapa mvua kutoka mbinguni na majira yenye kuzaa matunda, alijaza mioyo yao kikamili kwa chakula na uchangamfu.’ (Mdo. 14:17) Kwa kweli, Yehova anaonyesha wanadamu wote ukarimu.​—Lu. 6:35.

6, 7. (a) Yehova anafurahia zaidi sana kutimiza mahitaji ya nani? (b) Toa mufano unaoonyesha namna Yehova anavyowatunza waabudu wake waaminifu.

6 Yehova anafurahia zaidi sana kutimizia waabudu wake waaminifu mahitaji yao. Mufalme Daudi alisema hivi: ‘Nilikuwa kijana, pia nimezeeka, na bado sijamwona mutu yeyote mwadilifu akiwa ameachwa kabisa, wala uzao wake ukitafuta mukate.’ (Zab. 37:25) Wakristo wengi waaminifu wamejionea namna Yehova anavyowatunza watumishi wake. Fikiria mufano huu.

7 Miaka fulani iliyopita, dada mumoja painia anayeitwa Nancy alikuwa na tatizo fulani. Anasema hivi: “Nilihitaji dola 66 ili kulipia nyumba, siku zangu za kukaa katika nyumba hiyo zingemalizika siku iliyofuata. Sikujua namna gani ningepata feza hizo. Nilisali kuhusu tatizo hilo, na kisha nilienda kazini; nilitumika mahali panapouzishwa chakula kilichopikwa. Sikutazamia kupata matabishi mingi mangaribi hiyo kwa sababu watu wengi hawaje kununua chakula siku hiyo. Jambo la kushangaza ni kwamba watu wengi walikuja kula usiku huo. Wakati ulipofika ili mufanyakazi mwengine aje kunigomboa, nilihesabu matabishi yote niliyopata, ilikuwa dola 66.” Nancy anaamini kwamba Yehova alimutolea tu kile alichohitaji.​—Mt. 6:33.

8. Ni zawadi gani iliyo kubwa kuliko zote ambayo Yehova amewatolea wanadamu?

8 Kila mutu anaweza kufaidika na zawadi iliyo kubwa kuliko zote ambayo Yehova amewatolea wanadamu. Ni zawadi gani hiyo? Ni zabihu ya ukombozi ya Mwana wake. Yesu alisema hivi: ‘Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.’ (Yoh. 3:16) Katika andiko hili, neno “ulimwengu” linamaanisha wanadamu wote. Bila shaka, zawadi hiyo kubwa ya Yehova inaweza kuwafaidi wote wanaochagua kuikubali. Wale wanaoonyesha imani katika Yesu watakuwa na uzima kwa wingi, ni kusema, wataishi milele. (Yoh. 10:10) Bila shaka, hiyo ndiyo zawadi kubwa kuliko zote inayoonyesha kwamba Yehova ni mukarimu, sivyo?

TUIGE UKARIMU WA YEHOVA

Waisraeli walitiwa moyo kuiga ukarimu wa Yehova (Ona  fungu la 9)

9. Namna gani tunaweza kuiga ukarimu wa Yehova?

 9 Namna gani tunaweza kuiga ukarimu wa Yehova? Yehova ‘anatupa sisi vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie; kwa hiyo, tunapaswa kuwa “tayari kushiriki” vitu vyetu pamoja na wengine ili wafurahi. (1 Tim. 6:17-19) Tunafurahia kutumia mali yetu ili kuwatolea wale tunaopenda zawadi na kusaidia wale walio katika uhitaji. (Soma Kumbukumbu la Torati 15:7.) Ni nini itatusaidia tusisahau kuonyesha ukarimu? Wakristo fulani wanatumia njia hii: Kila mara wanapopokea zawadi, wanakumbuka kwamba wao pia wanapaswa kumutolea mutu mwengine zawadi. Katika kutaniko la Kikristo tuna pendeleo la kuwa na ndugu na dada wengi walio na roho ya kutoa.

10. Ni njia gani moja nzuri zaidi ya kuonyesha ukarimu?

10 Njia moja nzuri zaidi ya kuonyesha ukarimu ni kujitoa ili kuwasaidia wengine kwa maneno na matendo. Namna gani? Kwa kutumia wakati na nguvu zetu ili kuwasaidia wengine na kuwatia moyo. (Gal. 6:10) Ili kujua ikiwa tunafanya hivyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Je, wengine wanaweza kusema kwamba niko tayari kujitoa kwa ajili yao na kusikiliza wanaponielezea shida zao? Ikiwa mutu fulani ananiomba nimusaidie kufanya kazi ao jambo fulani, je, ninamusaidia kadiri ninavyoweza? Je, unakumbuka kwa mara ya mwisho ulipomupongeza mushiriki wa familia yako ao mwamini mwenzako?’ Tunapokuwa na “mazoea ya kuwapa watu,” hilo litatusaidia tumukaribie zaidi Yehova na tutakuwa na uhusiano muzuri pamoja na marafiki wetu.​—Lu. 6:38; Met. 19:17.

11. Namna gani tunaweza kumuonyesha Yehova ukarimu?

 11 Tunaweza pia kumuonyesha Yehova ukarimu. Biblia inatushauri hivi: ‘Muheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye samani.’ (Met. 3:9) ‘Vitu [hivyo] vyenye samani’ vinatia ndani wakati wetu, nguvu, na mali yetu, tunayoweza kutumia bila kulazimishwa ili kufanya kazi yake. Hata watoto wadogo wanaweza kujifunza kumuonyesha Yehova ukarimu. Jason anasema hivi: “Familia yetu inapotoa michango, tunawapatia watoto wetu michango hiyo ili waitie katika kisanduku cha michango. Wanafurahia jambo hilo kwa sababu kwa kufanya hivyo ‘wanamutolea Yehova kitu fulani.’” Watoto wanaojifunza kumutolea Yehova wakiwa wangali wadogo wanaweza kuendelea kufanya hivyo watakapokomaa.​—Met. 22:6.

YEHOVA NI MWENYE USAWAZIKO

12. Kuwa mwenye usawaziko kunamaanisha nini?

12 Usawaziko ni moja kati ya sifa za Yehova zenye kuvutia. Kuwa mwenye usawaziko kunamaanisha nini? Katika Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, mara nyingi neno la Kigiriki linalotafsiriwa “mwenye usawaziko” linamaanisha “mwenye kukubali maoni ya wengine.” (Tito 3:1, 2) Mutu aliye na usawaziko hafuatie kila mara mambo madogo-madogo ya sheria, wala hawalazimishe watu wafuate tu maoni yake, na si mukali. Badala yake, anajikaza kutendea wengine kwa upole, anabadilika kulingana na hali zao. Mutu mwenye usawaziko iko tayari kusikiliza wengine na, inapofaa anakubali maoni yao na kubadilika kulingana na hali.

13, 14. (a) Namna gani Yehova anaonyesha usawaziko? (b) Namna Yehova alivyomutendea Loti inatufundisha nini?

13 Namna gani Yehova anaonyesha usawaziko? Yehova anafikiria maoni ya watumishi wake, na kila mara iko tayari kubadili maoni yake ili akubali maoni yao. Fikiria kwa mufano namna Yehova alivyomutendea mwanaume mwadilifu Loti. Yehova alipoamua kwamba ataharibu miji ya Sodoma na Gomora, alimuagiza waziwazi Loti akimbilie milimani. Lakini, kwa sababu fulani, Loti alimulilia Yehova amuruhusu akimbilie mahali pengine. Jaribu kufikiria hili: Loti alimuomba Yehova abadili maagizo yake!​—Soma Mwanzo 19:17-20.

14 Inaweza kuwa rahisi kufikiri kwamba Loti alikuwa muzaifu ao alikosa utii. Bila shaka, Yehova angemulinda mahali popote. Kwa hiyo, Loti hakuwa na sababu ya kuogopa, sivyo? Labda kuna mambo fulani ambayo aliogopa​—hatujue aliwaza nini, lakini Yehova alikubali uamuzi wake. Alimuruhusu Loti akimbilie kwenye muji ambao alikuwa ameamua kuharibu. (Soma Mwanzo 19:21, 22.) Kwa kweli, Yehova si mukali na hawalazimishe watu wafuate maoni yake. Yeye anakubali maoni ya wengine na ni mwenye usawaziko.

15, 16. Namna gani Sheria ya Musa ilionyesha usawaziko wa Yehova? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

15 Mufano mwengine unaoonyesha usawaziko wa Yehova unaonekana katika Sheria ya Musa. Ikiwa Mwisraeli fulani alikuwa maskini sana na hangepata mwana-kondoo ao mbuzi ya kumutolea Yehova, angetoa njiwa tetere wawili ao njiwa wawili. Lakini ingekuwa namna gani ikiwa Mwisraeli alikuwa maskini sana hivi kwamba hawezi kupata hata njiwa wawili? Katika hali hiyo, Yehova aliruhusu Mwisraeli huyo maskini atoe unga kidogo. Hata hivyo, fikiria jambo hili la lazima: Unga huo haungekuwa wa hivi hivi, lakini “unga laini,” unga ambao Mwisraeli alipaswa kutumia alipokuwa na wageni wa heshima. (Mwa. 18:6) Sababu gani jambo hilo ni lenye kutia moyo?​—Soma Walawi 5:7, 11.

16 Fikiria ikiwa wewe ndiye Mwisraeli huyo maskini sana. Unafika kwenye tabenakulo ao hema ya ibada ukiwa na unga kidogo ili kutoa zabihu na kisha unawaona Waisraeli matajiri wakileta mifugo yao. Kwa hiyo, unasikilia haya zabihu yako ya unga. Kisha, unakumbuka kwamba Yehova anaona zabihu yako kuwa ya maana. Sababu gani? Kwa sababu Yehova aliagiza kwamba unga wa kumutolea unapaswa kuwa laini, wa hali ya juu. Kwa kweli, ni kama vile Yehova alikuwa akimuambia Mwisraeli aliyekuwa maskini sana hivi: ‘Ninajua kama hauwezi kutoa mengi kama wengine, lakini ninajua pia kama unatoa kulingana na uwezo wako.’ Kwa kweli, Yehova anaonyesha usawaziko kwa kufikiria uwezo na hali ya watumishi wake.​—Zab. 103:14.

17. Yehova anakubali utumishi wa namna gani?

 17 Ni jambo lenye kufariji kujua kwamba, kwa kuwa Yehova ni mwenye usawaziko, anakubali utumishi tunaomutolea kwa nafsi yetu yote. (Kol. 3:23) Constance, dada mwenye kuzeeka wa Italie, alisema hivi: “Kuzungumuza na wengine kuhusu Muumba wangu ndilo jambo ambalo nimependa sana kufanya siku zote. Hiyo ndiyo sababu ninaendelea kuhubiri na kuongoza mafunzo ya Biblia. Wakati fulani ninahuzunika kwa sababu siwezi kufanya mengi kwa sababu ya afya yangu. Lakini ninatambua kwamba Yehova anajua uwezo wangu, ananipenda na anapendezwa sana na yale ninayoweza kufanya.”

TUIGE USAWAZIKO WA YEHOVA

18. Namna gani wazazi wanaweza kumuiga Yehova?

18 Namna gani tunaweza kuiga usawaziko wa Yehova? Fikiria tena namna Yehova alivyomutendea Loti. Yehova alikuwa na mamlaka ya kumuambia Loti mahali pa kukimbilia; lakini kwa upole, alimusikiliza Loti alipotoa maoni yake. Na alimuruhusu aende mahali alipotaka. Ikiwa wewe ni muzazi, je, unaweza kumuiga Yehova? Je, unaweza kusikiliza maoni ya watoto wako na kubadilika kulingana na hali ikiwa maoni yao yanafaa? Kuhusiana na hilo, Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 9, 2007, ulionyesha kwamba wazazi fulani wanaweza kuwaalika watoto wao wanapozungumuzia sheria za kufuata katika familia. Kwa mufano, wazazi wakiamua kuweka wakati wa kurudi nyumbani, wana haki ya kuchagua saa fulani ambayo watoto wanapaswa kuwa nyumbani. Hata hivyo, wanapaswa kusikiliza maoni ya watoto wao kuhusu saa waliyochagua. Wakati mwingine, wazazi wanaweza kuamua kubadili saa waliyochagua kwa sababu kufanya hivyo hakuvunje kanuni za Biblia. Wazazi wataona kwamba wakati wanafikiria maoni ya watoto wao kuhusu sheria za nyumbani, watoto watakuwa tayari kuelewa sheria hizo na kuzitii.

19. Namna gani wazee wanaweza kujikaza kuiga usawaziko wa Yehova?

19 Wazee wa kutaniko wanajikaza kuiga usawaziko wa Yehova kwa kufikiria hali za waamini wenzao. Tukumbuke kwamba Yehova alipendezwa sana na zabihu hata za Waisraeli waliokuwa maskini sana. Vilevile, ndugu na dada fulani hawawezi kuhubiri sana, labda kwa sababu ya magonjwa ao uzee. Namna gani ikiwa ndugu na dada hao wapendwa wanavunjika moyo kwa sababu hawawezi tena kufanya mengi? Wazee wanaweza kuwahakikishia kwa upole kwamba Yehova anawapenda kwa sababu wanatoa kulingana na uwezo wao.​—Mk. 12:41-44.

20. Je, usawaziko unamaanisha kufanya mambo machache katika kazi ya Mungu? Eleza.

20 Bila shaka, hatupaswe hata kidogo kufikiri kwamba usawaziko unamaanisha kupunguza bidii yetu katika kazi ya Mungu ili tu kujitendea kwa fazili. (Mt. 16:22) Hatupendi kufanya mambo machache katika kazi ya Mungu ijapokuwa tuna uwezo wa kufanya mengi, na kujitetea kwamba huo ndio usawaziko. Tofauti na hilo, sisi wote, tunapaswa ‘kujitahidi sana’ ili kutegemeza faida za Ufalme. (Lu. 13:24) Kwa hiyo, tunapaswa kuwa na usawaziko katika mambo mawili. Kwanza tunapaswa kumutumikia Mungu kwa nguvu zetu zote. Jambo la pili, tukumbuke kwamba Yehova hatuombe yale ambayo hatuwezi kufanya. Tunapomutolea kile kinacholingana na uwezo wetu, tuwe hakika kwamba anafurahi sana. Je, hatuone kama ni jambo lenye kufurahisha kumutumikia Mungu kama huyo mwenye shukrani na mwenye usawaziko? Katika habari inayofuata, tutazungumuzia sifa zingine mbili zenye kuvutia za Yehova.​—Zab. 73:28.

‘Muheshimu Yehova kwa vitu vyako vyenye samani.’​—Met. 3:9 (Ona  fungu la 11)

‘Lolote munalofanya, lifanyeni kwa nafsi yote.’​—Kol. 3:23 (Ona  fungu la 17)