Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

“Wana wa Mungu wa kweli” walioishi duniani mbele ya Garika, kulingana na Mwanzo 6:2, 4, walikuwa nani?

Ni sababu gani hizo?

Mistari ya kwanza ya andiko hilo inasema hivi: “Wana wa Mungu wa kweli wakaanza kuwaona mabinti wa wanadamu, kwamba ni wenye sura ya kupendeza; nao wakajichukulia wake, yaani, wote waliowachagua.”​—Mwa. 6:2.

Katika Maandiko ya Kiebrania, maneno “wana wa Mungu wa kweli” na “wana wa Mungu” yanapatikana katika Mwanzo 6:2, 4; Ayubu 1:6; 2:1; 38:7; na Zaburi 89:6. Maandiko hayo yanaonyesha nini kuhusu hao “wana wa Mungu”?

Bila shaka, “wana wa Mungu” wanaotajwa katika Ayubu 1:6 walikuwa viumbe wa kiroho ambao walikusanyika mbele za Mungu. Shetani aliyekuwa ‘akizurura huku na huku duniani’ alikuwa kati ya viumbe hao wa kiroho. (Ayu. 1:7; 2:1, 2) Vivyo hivyo, katika Ayubu 38:4-7, tunasoma kuhusu “wana wa Mungu” ambao ‘walipaaza sauti kwa kushangilia’ wakati Mungu ‘aliweka jiwe la pembeni’ la dunia. Wana hao walikuwa malaika, kwa sababu wakati huo, wanadamu walikuwa bado hawajaumbwa. Bila shaka, “wana wa Mungu” wanaotajwa katika Zaburi 89:6 ni malaika wanaoishi mbinguni pamoja na Mungu, wala si wanadamu.

Kwa hiyo basi, “wana wa Mungu wa kweli” wanaotajwa katika masimulizi ya Mwanzo 6:2, 4 ni nani? Kulingana na habari za Biblia zilizo hapo juu, ni jambo la akili kusema kwamba masimulizi hayo yanahusu malaika waliokuja duniani.

Inaweza kuwa vigumu kwa watu fulani kukubali kwamba malaika wanaweza kutamani kufanya kitendo cha ndoa. Maneno ya Yesu katika andiko la Mathayo 22:30 yanaonyesha kwamba huko mbinguni malaika hawafunge ndoa ao kufanya ngono. Lakini, wakati fulani malaika walivaa miili ya kibinadamu, hata walikula na kunywa pamoja na wanadamu. (Mwa. 18:1-8; 19:1-3) Kwa hiyo, ni jambo la akili kusema kwamba kisha kuvaa miili ya kibinadamu, malaika waliweza kulala na wanawake.

Biblia inatoa sababu zinazoonyesha kwamba malaika fulani walifanya hivyo kabisa. Andiko la Yuda 6, 7 linalinganisha zambi za watu wa Sodoma, ambao walifanya matendo ya mwili yasiyo ya asili, na matendo ya “malaika ambao hawakubaki mahali pao pa kwanza bali wakayaacha makao yao wenyewe yanayofaa.” Malaika hao na watu wa Sodoma, wote “walifanya uasherati kwa kuzidi mno na [walienda] kufuatilia mwili kwa ajili ya matumizi yasiyo ya asili.” Maneno kama hayo yanayopatikana katika 1 Petro 3:19, 20 yanataja malaika hao wasiotii yanapozungumuzia “siku za Noa.” (2 Pet. 2:4, 5) Kwa hiyo, matendo ya malaika hao wasiotii katika siku za Noa yanaweza kulinganishwa na zambi za Sodoma na Gomora.

Jambo hilo linaeleweka tunapotambua kwamba “wana wa Mungu wa kweli” wanaozungumuziwa katika Mwanzo 6:2, 4 walikuwa malaika waliovaa miili ya kibinadamu na waliofanya uasherati pamoja na wanawake.

Biblia inasema kwamba Yesu ‘aliwahubiria roho walio katika gereza.’ (1 Pet. 3:19) Maneno hayo yanamaanisha nini?

Bila shaka, Petro alikuwa akizungumuzia malaika waliochagua kujiunga na Shetani katika uasi. Yuda anataja malaika ambao “hawakubaki mahali pao pa kwanza bali wakaacha makao yao wenyewe yanayofaa,” anaposema kwamba Mungu ‘amewaweka akiba wakiwa na vifungo vya milele chini ya giza nzito kwa ajili ya hukumu ya ile siku kubwa.’​—Yuda 6.

Ni katika njia gani viumbe hao wa kiroho hawakutii katika siku za Noa? Mbele ya Garika, roho waovu hao walivaa miili ya kibinadamu​—jambo ambalo Mungu hakuwapangia. (Mwa. 6:2, 4) Zaidi ya hilo, malaika hao waliolala na wanawake walikuwa wakifanya jambo lisilo la asili. Mungu hakuwaumba malaika ili wafanye ngono pamoja na wanawake. (Mwa. 5:2) Mungu atawaharibu malaika hao waovu na wasiotii kwa wakati ambao ameweka. Lakini kwa sasa, kama vile Yuda anavyosema, malaika hao wako katika hali ya ‘giza nzito,’ ni kusema, gereza la kiroho.

Ni wakati gani na namna gani Yesu aliwahubiria hao “roho walio katika gereza”? Petro aliandika kwamba jambo hilo lilitukia kisha “Yesu kufanywa kuwa hai katika roho.” (1 Pet. 3:18, 19) Petro anasema tena kwamba Yesu ‘aliwahubiria.’ Petro anatumia wakati uliopita ili kuonyesha kwamba mahubiri hayo yalifanyika mbele aandike barua yake ya kwanza. Kwa hiyo, inaonekana kwamba, wakati fulani kisha kufufuliwa, Yesu aliwatangazia roho hao waovu hukumu ya haki ambayo wanastahili kupewa. Yesu hakuwatolea tumaini lolote. Mahubiri hayo yalikuwa ya hukumu. (Yona 1:1, 2) Kwa kuwa Yesu alikuwa ameonyesha imani na uaminifu mupaka kifo na baadaye alifufuliwa​—na kuonyesha hivyo kwamba Ibilisi hakuwa na uwezo juu yake, Yesu alikuwa na musingi muzuri wa kutangaza hukumu hiyo.​—Yoh. 14:30; 16:8-11.

Kwa wakati unaokuja, Yesu atamutupa Shetani na malaika hao katika abiso. (Lu. 8:30, 31; Ufu. 20:1-3) Mupaka wakati huo, roho hao wasiotii wataendelea kuwa katika giza nzito la kiroho, na mwishowe wataharibiwa bila shaka.​—Ufu. 20:7-10.