Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA: JE, KUNA DINI YOYOTE AMBAYO UNAWEZA KUTUMAINIA?

Sababu Gani Unapaswa Kuichunguza Dini Yako?

Sababu Gani Unapaswa Kuichunguza Dini Yako?

Wazia unahitaji kupasuliwa kwa sababu una ugonjwa ambao unahatarisha maisha yako. Utapenda kupata muganga mupasuaji mwenye kutumainika sana kwa sababu maisha yako yatakuwa katika mikono yake. Litakuwa jambo la hekima kuchunguza ikiwa kwa kweli anajua vizuri kazi yake ya upasuaji, sivyo?

Vivyo hivyo, ni jambo la hekima kuchunguza dini yako kwa uangalifu. Ikiwa wewe ni muamini wa dini fulani, kwa kweli unatia uzima wako wa kiroho katika mikono ya dini hiyo. Hilo linatia ndani tumaini lako la kupata uzima wa milele.

Yesu alitoa kanuni inayotusaidia kuchunguza kwa uangalifu dini yetu. Alisema hivi: ‘Kila muti unajulikana kwa matunda yake.’ (Luka 6:44) Kwa mufano, wakati tunachunguza dini fulani, tunapaswa kujiuliza, inazaa matunda gani? Je, viongozi wa dini hiyo wanakaza sana watu kutoa feza? Je, washiriki wa dini hiyo wanafuata kanuni za Biblia kuhusu vita na mwenendo muzuri? Mwishowe, je, kuna dini yoyote ambayo unaweza kutumainia? Tunakuomba uchunguze habari zinazofuata.

‘Kila muti unajulikana kwa matunda yake.’​—Luka 6:44