Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Tuambie, Mambo Haya Yatakuwa Wakati Gani?”

“Tuambie, Mambo Haya Yatakuwa Wakati Gani?”

‘Ni nini itakayokuwa ishara [alama] ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mufumo wa mambo?’​—MT. 24:3.

1. Kama mitume, sisi pia tunatamani sana kujua nini?

 KAZI ya Yesu ya kuhubiri ilipokuwa karibu kumalizika, wanafunzi wake walitamani sana kujua mambo ambayo yangetokea wakati ujao. Kwa hiyo, siku chache tu mbele ya kifo chake, mitume wake wane walimuuliza hivi: ‘Mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mufumo wa mambo?’ (Mt. 24:3; Mk. 13:3) Yesu aliwajibu kwa kuwatolea unabii ambao ungetimia kwa kiasi kikubwa, unabii unaopatikana katika sura ya 24 na 25 ya kitabu cha Mathayo. Katika unabii huo, Yesu alizungumuzia matukio mengi makubwa ya wakati ujao. Unabii wake ni wa maana sana kwetu kwa sababu sisi pia tunatamani sana kujua mambo yatakayotukia wakati ujao.

2. (a) Kwa miaka mingi, tumetafuta kuelewa vizuri zaidi jambo gani? (b) Tutazungumuzia maulizo gani matatu?

2 Kwa miaka mingi, watumishi wa Yehova wamejifunza na kusali ili kuelewa unabii wa Yesu kuhusu siku za mwisho. Wametafuta kuelewa vizuri zaidi wakati unabii huo ungetimia. Ili kujua namna gani tumefikia kuelewa vizuri zaidi unabii huo, acheni tuzungumuzie maulizo matatu yanayohusu wakati unabii huo ungetimia. ‘Ziki kubwa’ itaanza wakati gani? Yesu atahukumu “kondoo” na “mbuzi” wakati gani? Yesu ‘atafika’ ao kuja wakati gani?​—Mt. 24:21; 25:31-33.

ZIKI KUBWA ITAANZA WAKATI GANI?

3. Zamani, tulifikiri ziki kubwa ingekuwa na sehemu gani tatu?

3 Kwa miaka fulani, tulifikiri kwamba ziki kubwa ilianza na Vita ya Kwanza ya Ulimwengu katika 1914 na kwamba ‘siku hizo zilifupishwa’ na Yehova katika 1918 wakati vita hiyo ilimalizika ili mabaki ya watiwa-mafuta wapate nafasi ya kuhubiri habari njema katika mataifa yote. (Mt. 24:21, 22) Tulifikiri kwamba kisha kazi hiyo kutimizwa, ulimwengu wa Shetani ungeharibiwa. Kwa hiyo, tulifikiri kwamba ziki kubwa ingekuwa na sehemu tatu: Ingeanza katika (1914-1918), ingekatizwa (kuanzia mwaka wa 1918 na kuendelea), na ingefikia mwisho kwenye Har-magedoni.

4. Ni uvumbuzi gani ambao umetusaidia kuelewa vizuri zaidi unabii wa Yesu kuhusu siku za mwisho?

4 Hata hivyo, kisha kuchunguza tena unabii wa Yesu, tulivumbua kwamba sehemu moja ya unabii wake kuhusu siku za mwisho inatimia mara mbili. (Mt. 24:4-22) Ilitimia kwa mara ya kwanza huko Yudea wakati wa mitume, na kisha kungekuwa utimizo wa ulimwenguni pote katika siku zetu. Kuvumbua jambo hilo kumetuongoza kwenye mafasirio mapya ya unabii huo. *

5. (a) Ni kipindi gani kigumu kilichoanza katika 1914? (b) Kipindi hicho cha taabu kinalingana na kipindi gani cha wakati wa mitume?

5 Tulielewa pia kwamba sehemu ya kwanza ya ziki kubwa haikuanza katika 1914. Sababu gani? Kwa sababu unabii wa Biblia unaonyesha kwamba ziki kubwa itaanza na kushambuliwa kwa dini ya uongo, haitaanza na vita kati ya mataifa. Kwa hiyo, matukio yaliyoanza katika 1914 hayakuwa mwanzo wa ziki kubwa, lakini yalikuwa “mwanzo wa maumivu ya taabu.” (Mt. 24:8) Hayo “maumivu ya taabu” yanalingana na yale yaliyotokea katika Yerusalemu na Yudea kuanzia mwaka wa 33 mupaka 66 kisha Yesu.

6. Ni nini itakayoonyesha kwamba ziki kubwa imeanza?

 6 Ni nini itakayoonyesha kwamba ziki kubwa imeanza? Yesu alitabiri hivi: ‘Kwa hiyo, mutakapoona lile chukizo linalosababisha ukiwa, kama vile lilivyosemwa kupitia nabii Danieli, likiwa limesimama katika mahali patakatifu, (musomaji na atumie utambuzi,) ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani.’ (Mt. 24:15, 16) Katika siku za mitume, “lile chukizo,” ni kusema, jeshi la Roma, ‘lilisimama mahali patakatifu’ katika mwaka wa 66 wakati jeshi hilo lilishambulia muji wa Yerusalemu na hekalu lake (ambalo Wayahudi waliona kuwa takatifu). Katika utimizo mukubwa zaidi, Umoja wa Mataifa (ambao ndio “chukizo” la siku zetu) ‘utasimama’ mahali patakatifu wakati utashambulia dini zinazojidai kuwa za Kikristo (ambazo waamini wazo wanaziona kuwa takatifu) na dini zingine za Babiloni Mukubwa. Shambulio hilo linazungumuziwa katika Ufunuo 17:16-18. Tukio hilo litaonyesha kwamba ziki kubwa imeanza.

7. (a) Namna gani ‘mwili uliokolewa’ wakati wa mitume? (b) Tunaweza kutazamia nini katika siku zinazokuja?

 7 Yesu alitabiri pia hivi: “Siku hizo zitafupishwa.” Katika utimizo wa kwanza wa unabii huo, jambo hilo lilitimia katika mwaka wa 66 wakati jeshi la Roma ‘lilifupisha’ shambulio lake. Kisha, Wakristo watiwa​-mafuta wa Yerusalemu na Yudea walikimbia ili ‘mwili, ao uzima wao uokolewe.’ (Soma Mathayo 24:22; Mal. 3:17) Kwa hiyo basi, tunaweza kutazamia nini wakati wa ziki kubwa inayokuja? Yehova ‘atafupisha’ shambulio la Umoja wa Mataifa juu ya dini za uongo na hataruhusu dini ya kweli iharibiwe pamoja na dini za uongo. Hilo litawatolea watumishi wa Mungu nafasi ya kuokolewa.

8. (a) Ni mambo gani yatakayotokea kisha sehemu ya kwanza ya ziki kubwa? (b) Inaonekana mutiwa-mafuta wa mwisho wa wale 144 000 atainuliwa kwenda mbinguni wakati gani? (Ona maelezo ya kumalizia.)

  8 Ni jambo gani litakalotokea kisha sehemu ya kwanza ya ziki kubwa? Maneno ya Yesu yanaonyesha kwamba kutakuwa kipindi cha wakati ambacho kitaendelea mupaka mwanzo wa Har-magedoni. Ni mambo gani yatakayotokea muda wa kipindi hicho? Jibu linapatikana katika Ezekieli 38:14-16 na Mathayo 24:29-31. (Soma.) * Kisha mambo hayo, vita ya Har-magedoni ambayo ni sehemu ya mwisho kabisa ya ziki kubwa itaanza, vita hiyo inalingana na uharibifu wa Yerusalemu katika mwaka wa 70. (Mal. 4:1) Ziki kubwa itakayofikia mwisho wake kwenye vita ya Har-magedoni itakuwa tukio la pekee la ‘namna ambayo halijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu.’ (Mt. 24:21) Kisha Har-magedoni, Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo utaanza.

9. Unabii wa Yesu kuhusu ziki kubwa unatutia nguvu namna gani?

9 Unabii huo kuhusu ziki kubwa unatutia nguvu. Sababu gani? Kwa sababu unatuhakikishia kwamba hata wapambane na matatizo ya namna gani, watu wa Yehova kwa ujumla, wataokoka ziki kubwa. (Ufu. 7:9, 14) Zaidi ya yote, tunafurahi kwa kuwa kwenye Har-magedoni, Yehova atatetea mamlaka yake na atalitakasa jina lake takatifu.​—Zab. 83:18; Eze. 38:23.

YESU ATAHUKUMU KONDOO NA MBUZI WAKATI GANI?

10. Zamani, tulifikiri kwamba kuhukumiwa kwa kondoo na mbuzi kungetokea wakati gani?

10 Tuzungumuzie sasa wakati ambapo sehemu nyingine ya unabii wa Yesu itatimia; sehemu hiyo ni mufano unaohusu kuhukumiwa kwa kondoo na mbuzi. (Mt. 25:31-46) Zamani, tulifikiri kwamba watu walio mufano wa kondoo na mbuzi wangehukumiwa katika kipindi chote cha siku za mwisho kilichoanza mwaka wa 1914 na kuendelea. Kwa hiyo, tuliamini kwamba wale waliokataa ujumbe wa Ufalme na ambao walikufa mbele ya ziki kubwa kuanza walifananisha mbuzi, na hawangekuwa na tumaini la kufufuliwa.

11. Sababu gani tunaweza kusema kwamba hukumu ya watu walio mufano wa kondoo ao mbuzi haikuanza katika 1914?

11 Katikati ya miaka ya 1990, gazeti Munara wa Mulinzi lilizungumuzia tena andiko la Mathayo 25:31, linalosema hivi: “Wakati Mwana wa binadamu atakapofika katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu.” Gazeti hilo lilionyesha kwamba Yesu alikuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu katika 1914, lakini wakati huo ‘hakuketi juu ya kiti chake cha Ufalme chenye utukufu’ ili kuhukumu “mataifa yote.” (Mt. 25:32; linganisha na Danieli 7:13.) Hata hivyo, mufano wa kondoo na mbuzi unaonyesha kwanza namna Yesu anavyohukumu mataifa. (Soma Mathayo 25:31-34, 41, 46.) Kwa kuwa Yesu hakuanza kuhukumu mataifa yote katika 1914, hilo linamaanisha kwamba hakuanza kuhukumu watu walio mufano wa kondoo ao mbuzi katika mwaka huo. * Kwa hiyo basi, hukumu hiyo itaanza wakati gani gani?

12. (a) Ni wakati gani Yesu atahukumu mataifa yote kwa mara ya kwanza? (b) Ni mambo gani yatakayotokea yanayozungumuziwa katika Mathayo 24:30, 31 na Mathayo 25:31-33, 46?

  12 Unabii wa Yesu kuhusu siku za mwisho unaonyesha kwamba Yesu atahukumu mataifa yote kwa mara ya kwanza kisha kuharibiwa kwa dini za uongo. Kama ilivyoonyeshwa katika  fungu la 8, mambo fulani yatakayotokea wakati huo yanazungumuziwa katika Mathayo 24:30, 31. Unapochunguza mistari hiyo, utaona kwamba mambo ambayo Yesu alitabiri kwamba yatatokea wakati huo yanafanana na yale anayozungumuzia katika mufano wake wa kondoo na mbuzi. Kwa mufano, Mwana wa binadamu anakuja katika utukufu pamoja na malaika; makabila yote na mataifa yote yanakusanyika mbele yake; wale walio mufano wa kondoo ‘wanainua vichwa vyao’ kwa sababu watapata uzima wa milele. * Wale walio mufano wa mbuzi ‘wanajipiga-piga wenyewe kwa kuomboleza,’ kwa sababu wanatambua kwamba “watakatiliwa mbali milele.”​—Mt. 25:31-33, 46.

13. (a) Yesu atahukumu watu walio mufano wa kondoo ao mbuzi wakati gani? (b) Kujua hivyo kunatusaidia tutambue nini kuhusu kazi yetu ya kuhubiri?

 13 Kwa hiyo basi, tunaweza kusema nini? Yesu atahukumu watu wa mataifa yote walio mufano wa kondoo ao mbuzi atakapokuja wakati wa ziki kubwa. Kisha, kwenye Har-magedoni, ambayo ni sehemu ya mwisho ya ziki kubwa, watu walio mufano wa mbuzi “watakatiliwa mbali milele.” Kujua hivyo kunapaswa kutufanya tuone kazi yetu ya kuhubiri namna gani? Kunatusaidia kutambua kwamba kazi ya kuhubiri ni ya maana sana. Mbele ya ziki kubwa kuanza, watu wangali na nafasi ya kubadili maoni yao na kuanza kutembea katika barabara nyembamba “inayoongoza kwenye uzima.” (Mt. 7:13, 14) Bila shaka, leo watu wanaweza kuonyesha kwamba wao ni kondoo ao mbuzi. Hata hivyo, tunapaswa kukumbuka kwamba hukumu hiyo ya mwisho itakayoonyesha kabisa ikiwa mutu ni kondoo ao mbuzi, itafanywa wakati wa ziki kubwa. Kwa hiyo, tuna sababu nzuri za kuendelea kuwatolea watu wengi kadiri inavyowezekana nafasi ya kusikiliza na kukubali ujumbe wa Ufalme.

Mbele ya ziki kubwa kuanza, watu wangali na nafasi ya kubadili maoni yao

YESU ATAKUJA AO ATAFIKA WAKATI GANI?

14, 15. Ni mistari gani ine inayozungumuzia kuja kwa Yesu ili kuhukumu?

14 Je, uchunguzi mwingine wa unabii wa Yesu unaonyesha kwamba tunapaswa kubadili namna yetu ya kuelewa wakati mambo mengine makubwa aliyotabiri yatatokea? Maneno ya unabii huo yanatoa jibu. Acheni tuone.

15 Katika sehemu ya unabii wake unaopatikana kwenye Mathayo 24:29–25:46, Yesu anazungumuzia kwanza mambo ambayo yangetokea katika siku hizi za mwisho na wakati wa ziki kubwa inayokuja. Hapo, Yesu anatumia mara munane neno ‘kuja’ ao kufika kwake. * Kuhusu ziki kubwa, Yesu alisema hivi: ‘[Makabila] yatamuona Mwana wa binadamu akija juu ya mawingu.’ ‘Hamujue ni siku gani Bwana yenu atakuja.’ ‘Mwana wa binadamu atakuja katika saa musiyofikiria.’ Na katika mufano wake wa kondoo na mbuzi, Yesu alisema hivi: ‘Mwana wa binadamu atafika katika utukufu wake.’ (Mt. 24:30, 42, 44; 25:31) Mistari yote hiyo ine inazungumuzia kuja kwa Yesu wakati ujao ili kuhukumu. Ni mistari gani mingine ine katika unabii wa Yesu inayozungumuzia kuja kwake?

16. Ni mistari gani ingine inayozungumuzia kuja kwa Yesu?

16 Alipozungumuzia mutumwa mwaminifu na mwenye busara, Yesu alisema: ‘Mutumwa huyo atakuwa mwenye furaha ikiwa bwana wake atakapofika [atakapokuja] atamukuta akifanya hivyo.’ Katika mufano wa mabikira, Yesu alisema hivi: “Walipokuwa wakienda zao kununua, bwana-arusi akafika [akakuja].” Katika mufano wa talanta, Yesu alisema hivi: ‘Baada ya muda murefu bwana wa watumwa hao alikuja.’ Katika mufano huohuo, bwana wa watumwa hao alisema hivi: “Wakati wa kufika [kuja] kwangu ningekuwa nikipokea kilicho changu pamoja na faida.” (Mt. 24:46; 25:10, 19, 27) Mistari hiyo ine inayozungumuzia kuja kwa Yesu inahusu wakati gani?

17. Kwa muda murefu, tulieleza nini kuhusu kufika kwa Yesu kunakozungumuziwa katika Mathayo 24:46?

17 Zamani, tulisema katika vichapo vyetu kwamba mistari hiyo ine ya mwisho inazungumuzia kufika, ao kuja kwa Yesu katika 1918. Fikiria, kwa mufano, maneno ya Yesu kuhusu ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara.’ (Soma Mathayo 24:45-47.) Tulielewa kwamba ‘kufika’ kwa Yesu kunakozungumuziwa katika mustari wa 46 kulihusu wakati alikuja kuchunguza hali ya kiroho ya watiwa-mafuta katika 1918 na kwamba alimuweka mutumwa huyo juu ya mali yake yote katika 1919. (Mal. 3:1) Hata hivyo, kisha kuchunguza tena unabii wa Yesu, tumetambua kwamba tunapaswa kubadili namna tulivyoelewa ni wakati gani sehemu fulani za unabii huo zingetimia. Sababu gani tunasema hivyo?

18. Kisha kuchunguza kwa ukamili unabii wa Yesu, tunaweza kusema nini kuhusu kuja kwake?

 18 Katika mistari inayotangulia Mathayo 24:46, neno “atakapofika” linazungumuzia wakati ambapo Yesu atakuja ili kutangaza hukumu na kuitekeleza wakati wa ziki kubwa. (Mt. 24:30, 42, 44) Tena, kama tulivyoona katika  fungu la 12, ‘kufika’ kwa Yesu kunakozungumuziwa katika Mathayo 25:31 kunahusu wakati huohuo wa hukumu. Kwa hiyo, inaonekana wazi kwamba kuja kwa Yesu kunakozungumuziwa katika Mathayo 24:46, 47 ili kumuweka mutumwa mwaminifu juu ya mali yake yote, kutatokea pia wakati ujao, wakati wa ziki kubwa. * Kwa kweli, uchunguzi kamili wa unabii wa Yesu unaonyesha kwamba mistari yote hiyo munane ambayo tumechunguza kuhusu kuja kwake, itatimizwa wakati wa hukumu yake, ni kusema, wakati wa ziki kubwa.

19. Tumezungumuzia mafasirio gani mapya, na ni maulizo gani yatakayojibiwa katika habari mbili zinazofuata?

19 Kwa kifupi, tumejifunza nini? Mwanzoni mwa habari hii, tuliuliza maulizo matatu kuhusu ni wakati gani mambo fulani yangetokea. Kwanza, tuliona kwamba ziki kubwa haikuanza katika 1914 lakini itaanza wakati ambapo Umoja wa Mataifa utashambulia Babiloni Mukubwa. Kisha, tulizungumuzia sababu gani Yesu hakuanza kuhukumu watu walio mufano wa kondoo ao mbuzi katika 1914, lakini atafanya hivyo wakati wa ziki kubwa. Mwishowe, tulichunguza sababu gani Yesu hakuja kumuweka mutumwa mwaminifu juu ya mali yake yote katika 1919, lakini atafanya hivyo wakati wa ziki kubwa. Kwa hiyo, basi, mambo yote hayo matatu ambayo tumezungumuzia yatatokea katika kipindi kilekile cha wakati ujao, ni kusema, wakati wa ziki kubwa. Namna gani mafasirio hayo mapya yanatusaidia kuelewa vizuri zaidi mufano wa mutumwa mwaminifu? Pia, namna gani yanatusaidia kuelewa vizuri zaidi mifano mingine ya Yesu inayotimia katika wakati huu wa mwisho? Maulizo hayo ya maana yatazungumuziwa katika habari zinazofuata.

 

^ Fungu la 4: Ili kupata habari zaidi, soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15/02/1994, ukurasa wa 8-21 na wa tarehe 01/05/1999, ukurasa wa 8-20.

^ Fungu la 8: Moja kati ya mambo yanayozungumuziwa katika mistari hiyo ni ‘kukusanya watu waliochaguliwa.’ (Mt. 24:31) Kwa hiyo, inaonekana kwamba watiwa-mafuta wote watakaokuwa wangali bado duniani kisha sehemu ya kwanza ya ziki kubwa watainuliwa mbinguni mbele ya vita ya Har-magedoni kuanza. Mafasiriyo hayo mapya yanachukua nafasi ya yale yaliyotolewa katika “Maswali Kutoka kwa Wasomaji Wetu” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15/08/1990, ukurasa wa 30.

^ Fungu la 11: Soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15/10/1995, ukurasa wa 18-28.

^ Fungu la 12: Soma masimulizi yanayolingana na hayo katika Luka 21:28.

^ Fungu la 15: Maneno ‘kuja’ na ‘kufika’ yanatafsiriwa kutokana na tendo lilelile la Kigiriki, erʹkho·mai.

^ Fungu la 18: Kama tulivyoona, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “atakapofika” kwenye Mathayo 24:46 ni aina ya tendo lilelile la Kigiriki linalotafsiriwa “akija” kwenye Mathayo 24:30, 42, 44.

(Ona  fungu la 13)