Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova ‘Ananibebea Muzigo Wangu Kila Siku’

Yehova ‘Ananibebea Muzigo Wangu Kila Siku’

Hata ikiwa nimekuwa na ugonjwa wenye kusumbua sana na ambao nimefikiri kuwa siwezi kuuvumilia, nimejionea namna Baba yetu mupendwa wa mbinguni Yehova amenitegemeza kwa upendo muda wa maisha yangu yote. Na kwa zaidi ya miaka 20, nimepata furaha ya pekee kwa kumutumikia Yehova nikiwa painia.

Nilizaliwa mwaka wa 1956 na ugonjwa wa spina bifida (ugonjwa unaoshambulia mifupa ya mugongo). Kwa kuwa mishipa yangu ya ufahamu iliharibika, nilikuwa na matatizo ya kutembea na matatizo mengine makubwa ya afya.

Muda fulani mbele nizaliwe, bibi na bwana Mashahidi waliokuwa wamisionere walianza kujifunza Biblia pamoja na wazazi wangu. Nilipokuwa mutoto, kulikuwa tu na hesabu ndogo ya wahubiri walioishi katika muji wetu wa Usakos, Namibia. Kwa kuwa hakukuwa kutaniko huko, tulijifunza pamoja habari zilizopangwa kwa ajili ya mikutano. Nilipokuwa na miaka saba, nilifanyiwa urostomi, upasuaji wa kuniwezesha kukojoa. Nilipokuwa na miaka 14, nilianza kusumbuliwa na ugonjwa wa kifafa. Kwa kuwa masomo ya segondere ambako ningesomea ilikuwa mbali na nilihitaji matunzo ya pekee ya wazazi wangu, haikuwezekana nimalize masomo.

Hata hivyo, niliamua kutia nguvu uhusiano wangu na Yehova. Vichapo vyetu vingi vilikuwa havijapatikana katika luga yangu ya kuzaliwa, ni kusema, Kiafrikaans. Kwa hiyo, nilijifunza Kiingereza ili niweze kusoma vitabu vyetu. Nilipokuwa na miaka 19 nilikuwa muhubiri na nikabatizwa. Kwa miaka ine iliyofuata, nilikuwa na matatizo mengi ya afya na nilivunjika moyo sana. Zaidi ya hayo, katika muji wetu ambamo watu walikuwa na uhusiano wa karibu sana, kuwaogopa watu kulinifanya nisihubiri kwa bidii.

Nilipokuwa na miaka 20 hivi, tuliondoka Namibia na kuhamia Afrika Kusini, na kwa mara ya kwanza, nilianza kushirikiana na kutaniko. Hilo lilikuwa jambo nzuri kabisa! Hata hivyo, nilipaswa kufanyiwa tena upasuaji, wakati huu nilifanyiwa kolostomi, ni kusema, upasuaji wa wa kuniwezesha kuondoa uchafu wa tumboni.

Muda fulani baadaye, nilisikiliza hotuba ya mwangalizi wa muzunguko iliyozungumuzia kazi ya upainia. Mashauri yake yalinigusa moyo. Nilijua kwamba ilikuwa vigumu kwangu kufanya upainia kwa sababu ya afya yangu, lakini nilikuwa nimejionea namna Yehova alivyokuwa amenisaidia kuvumilia majaribu mengi. Kwa hiyo nilijaza ombi la kuwa painia wa kawaida. Lakini, wazee walisita kukubali ombi langu kwa sababu nilikuwa na matatizo ya afya.

Hata hivyo, niliamua kufanya yote ambayo ningeweza katika kazi ya kuhubiri. Kwa musaada wa mama yangu na wengine, nilifikia kueneza saa zinazoombwa kwa painia kwa muda wa miezi sita. Hilo lilionyesha kwamba niliazimia kuwa painia na lilionyesha kwamba afya yangu haingenizuia. Kwa hiyo, nilijaza ombi tena, na wakati huu ombi langu likakubaliwa. Tarehe 1 Mwezi wa 9, 1988, nilianza kazi ya upainia wa kawaida.

Kwa miaka yote ambayo nimekuwa painia, Yehova ameendelea kunitegemeza. Kuwafundisha wengine ukweli kuliko kufikiria tu matatizo yangu kumenilinda, kumenipa utulivu, na kumenisaidia nikomae kiroho. Nimepata furaha nyingi kwa kuwasaidia watu wengi wajitoe kwa Yehova na kubatizwa.

Hali yangu ya afya inaendelea kuharibika. Lakini Yehova ‘ananibebea muzigo wangu kila siku.’ (Zab. 68:19) Zaidi ya kunisaidia kuvumilia matatizo yangu; ananisaidia nifurahie maisha!