Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA

Sababu Gani Unapaswa Kupendezwa na Biblia?

Sababu Gani Unapaswa Kupendezwa na Biblia?

Biblia ni kitabu ambacho kinapendwa sana na watu wengi duniani. Sababu gani? Sababu moja ni kwamba Biblia inaeleweka kwa vyepesi. Ina habari za kweli juu ya watu ambao waliishi kwelikweli na juu ya uhusiano kati yao wenyewe na kati yao na Mungu. Habari hizo zinafundisha mambo mazuri kwa kutumia maneno mepesi na yaliyo wazi. Maneno hayo yanaweza kutafsiriwa katika luga nyingi na kueleweka kwa watu wa kila mahali na wa vizazi vyote. Na kanuni za Biblia ni zenye kufaa sikuzote.

Jambo la maana zaidi, Biblia inajieleza kuwa kitabu kinachozungumuza juu ya Mungu na pia kilichotoka kwa Mungu. Inaonyesha jina la Mungu, sifa zake, na kusudi lake lisilobadilika ambalo alikuwa nalo alipoumba dunia na wanadamu. Biblia inaeleza pia mapambano ya muda murefu kati ya wema na uovu: habari yenye kuvutia inayohusu ulimwengu wote ambayo mwisho wake utakuwa wenye kufurahisha. Tunaposoma Biblia tukiwa na mawazo mazuri, jambo hilo linatusaidia kuwa na imani na tumaini.

Katika Biblia, tunapata habari ambazo hatuwezi kupata mahali pengine. Kwa mufano, Biblia inatueleza ukweli juu ya habari kama hizi:

  • Uzima wetu ulianza namna gani na sababu gani tunateseka

  • Mipango ambayo Mungu alifanya ili kukomboa wanadamu

  • Mambo ambayo Yesu alifanya kwa ajili yetu

  • Wakati ujao wa dunia na wanadamu

Ni vizuri uchunguze habari zinazofuata na kuona Biblia inazungumuzia habari gani.