Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | LIES THAT MAKE GOD SEEM UNLOVABLE

Fundisho la Uongo Ambalo Limemufanya Mungu Kuwa Fumbo

Fundisho la Uongo Ambalo Limemufanya Mungu Kuwa Fumbo

MAMBO AMBAYO WATU WENGI WANAAMINI:

Dini ya Kikristo “katika aina zake tatu kubwa, ni kusema, Kanisa Katoliki la Roma, Kanisa Ortodoksi la Mangaribi, na Uprotestanti, zinakubali kwamba kuna Watu watatu katika Mungu mumoja: Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mutakatifu. Kulingana na teolojia ya dini ya Kikristo, maneno hayo hayamaanishe kwamba kuna miungu mitatu lakini yanamaanisha kuwa watu hao watatu wanafanyiza mutu mumoja.”​—The New Encyclopædia Britannica.

KWELI YA BIBLIA:

Yesu, Mwana wa Mungu, hakusema hata kidogo kwamba alikuwa sawa na Baba yake ao kwamba yeye na Baba yake walikuwa mutu mumoja. Lakini, alisema hivi: ‘Ninaenda kwa Baba, kwa sababu Baba ni mukubwa kuliko mimi.’ (Yohana 14:28) Pia alimuambia mumoja wa wanafunzi wake hivi: “Ninapanda kwenda kwa Baba yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu na Mungu wenu.”​—Yohana 20:17.

Roho takatifu si mutu. Wakristo wa kwanza ‘walijazwa roho takatifu,’ na Yehova alisema hivi: “Nitaimimina sehemu ya roho yangu juu ya kila namna ya mwili.” (Matendo 2:1-4, 17) Roho takatifu si sehemu ya Utatu. Lakini ni nguvu ya Mungu ya utendaji.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Karl Rahner na Herbert Vorgrimler, watu wenye elimu ya dini ya Katoliki, wanaeleza kwamba Utatu “haungeweza kujulikana bila ufunuo, na hata kisha ufunuo hauwezi kuelewa kabisa fundisho hilo.” Je, unaweza kweli kumupenda mutu fulani ambaye haiwezekane kumujua ao kumuelewa? Kwa hiyo, fundisho la Utatu, linawazuia watu kumujua na kumupenda Mungu.

Marco, aliyetajwa katika habari iliyotangulia, aliona kwamba fundisho la Utatu lilimuzuia kumukaribia Mungu. Anasema hivi: “Nilifikiri kwamba Mungu alikuwa ananificha namna alivyo, na jambo hilo lilimufanya Mungu awe mbali sana na watu, awe fumbo, na asiyeweza kukaribiwa.” Hata hivyo, Biblia inasema kwamba Mungu ‘hayuko mbali sana na kila mumoja wetu.’ (Matendo 17:27) Hakutuficha namna alivyo. Anataka tumujue. Yesu alisema hivi: “Tunaabudu tunachokijua.”​—Yohana 4:22.

Marco anasema hivi: “Wakati nilijifunza kwamba Mungu si sehemu ya Utatu, mwishowe niliweza kufanya uhusiano wa pekee pamoja na yeye.” Ikiwa tunamuona Yehova kuwa mutu mumoja kuliko kumuona kuwa fumbo la ajabu​-ajabu, itakuwa vyepesi sana kumupenda. Biblia inasema hivi: ‘Yeye ambaye hapendi hajamujua Mungu, kwa sababu Mungu ni upendo.’​—1 Yohana 4:8.