Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wachungaji, Muige Wachungaji Wakubwa Zaidi

Wachungaji, Muige Wachungaji Wakubwa Zaidi

‘Kristo aliteseka kwa ajili yenu, akiwaachia ninyi kielelezo ili mufuate hatua zake kwa ukaribu.’​—1 PET. 2:21.

1, 2. (a) Mambo yanakuwa namna gani kondoo wanapotunzwa vizuri? (b) Sababu gani watu wengi katika siku za Yesu walikuwa kama kondoo wasio na muchungaji?

 KONDOO zinakuwa katika hali nzuri wakati muchungaji anazihangaikia. Kitabu kimoja kinachozungumuza kuhusu kuchunga kondoo kinasema hivi: “Muchungaji anayepatia tu kondoo majani bila kuhangaikia mahitaji mengine, kisha miaka michache kondoo nyingi zitagonjwa na kuwa zaifu.” Lakini, kondoo zinapotunzwa vizuri, zinakuwa na afya nzuri.

2 Ni hivyo pia kuhusu kutaniko. Ikiwa wachungaji wanahangaikia na kutunza kila kondoo, kutaniko nzima litakuwa na hali nzuri ya kiroho. Unaweza kukumbuka kwamba Yesu alisikitikia kikundi cha watu kwa sababu ‘walikuwa wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na muchungaji.’ (Mt. 9:36) Sababu gani walikuwa katika hali hiyo yenye kuhuzunisha? Kwa sababu wale waliopaswa kuwafundisha Sheria ya Mungu walikuwa wakali, waliwawekea sheria nyingi, na walikuwa wanafiki. Kuliko kusaidia na kutunza kondoo wa kundi lao, wale waliokuwa na daraka la kufundisha walitia “mizigo mizito” kwenye mabega ya watu.​—Mt. 23:4.

3. Wazee wa kutaniko wanapaswa kukumbuka nini wanapotimiza daraka lao la kuchunga kutaniko?

3 Leo, wachungaji, ni kusema, wazee wa kutaniko wana daraka nzito. Kondoo wanaochunga ni wa Yehova na Yesu. Yesu mwenyewe alijiita kuwa “muchungaji mwema.” (Yoh. 10:11) Kondoo ‘walinunuliwa kwa bei’ ambayo Yesu mwenyewe alilipa kupitia ‘damu yake yenye samani.’ (1 Kor. 6:20; 1 Pet. 1:18, 19) Anapenda kondoo sana hivi kwamba alikubali kutoa uzima wake kwa ajili yao. Siku zote wazee wanapaswa kukumbuka kwamba wako chini ya uongozi wa Yesu, ni kusema, wanapaswa kujitiisha kwa Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ambaye ni ‘muchungaji mukubwa wa kondoo.’​—Ebr. 13:20.

4. Habari hii itajibu ulizo gani?

4 Kwa hiyo basi, namna gani wachungaji Wakristo wanapaswa kutendea kondoo? Washiriki wa kutaniko wanaombwa ‘kutii wale wanaowaongoza.’ Kwa upande mwingine, wazee wanashauriwa kwamba waepuke ‘kupiga ubwana juu ya wale ambao ni uriti wa Mungu.’ (Ebr. 13:17; soma 1 Petro 5:2, 3.) Namna gani basi, wazee wanaweza kuongoza bila kupiga ubwana juu ya kutaniko, ao namna gani wanaweza kuepuka kutumia vibaya mamlaka ambayo Mungu amewatolea wanaposhugulikia kondoo?

“ATAWABEBA KATIKA KIFUA CHAKE”

5. Maneno ya mufano yanayotumiwa kwenye Isaya 40:11 yanatufundisha nini kumuhusu Yehova?

5 Nabii Isaya alisema hivi kumuhusu Yehova: ‘Atalichunga kundi lake mwenyewe kama muchungaji. Atawakusanya pamoja wana​-kondoo kwa mukono wake; naye atawabeba katika kifua chake. Wale wanaonyonya atawaongoza kwa uangalifu.’ (Isa. 40:11) Maneno hayo ya mufano yanaonyesha kwamba Yehova anashugulikia wale walio wazaifu na wanaohitaji kuhangaikiwa sana katika kutaniko. Kama vile muchungaji anavyojua mahitaji ya kila kondoo katika kundi lake na kuwa tayari kuyatimiza, Yehova anaelewa mahitaji ya washiriki wa kutaniko na anafurahia kuwatolea yale wanayohitaji. Wakati fulani muchungaji anabeba kondoo anayetoka tu kuzaliwa katika vazi lake; vilevile Yehova, “Baba ya rehema nyororo,” atatubeba wakati wa taabu. Atatufariji tunapopatwa na majaribu makali ao tunapohitaji musaada wa pekee.​—2 Kor. 1:3, 4.

6. Namna gani muzee anaweza kufuata mufano wa Yehova?

6 Muzee wa kutaniko anaweza kujifunza somo nzuri kutokana na mufano huo! Kwa kumuiga Yehova, anapaswa kuwa muangalifu ili ajue mahitaji ya kondoo. Muzee atakuwa tayari kutoa kitia-moyo na musaada unaohitajiwa, ikiwa anajua magumu na mahitaji yanayoombwa kushugulikiwa haraka ya kila kondoo. (Met. 27:23) Kwa hiyo, muzee anapaswa kuchukua wakati wa kuzungumuza na ndugu na dada na kuwasikiliza. Bila kujiingiza katika mambo yao ya kipekee, muzee anapaswa kuwa mwangalifu kuhusu yale anayoona na kusikia katika kutaniko na kuwa tayari ‘kuwasaidia wale walio zaifu.’​—Mdo. 20:35; 1 Thes. 4:11.

7. (a) Kondoo wa Mungu walitendewa namna gani katika siku za Ezekieli na Yeremia? (b) Yehova alikataa wachungaji ambao hawakuwa waaminifu, tunaweza kujifunza nini kutokana na jambo hilo?

7 Fikiria mwenendo wa wachungaji ambao Mungu alikataa. Katika siku za Ezekieli na Yeremia, Yehova alitupilia mbali wale waliopaswa kutunza kondoo wake lakini ambao hawakuwa wakifanya hivyo namna ilivyostahili. Kwa kuwa hakukuwa mutu wa kuchunga kondoo, kundi lilishambuliwa na kondoo zote zilitawanyika. Kuliko kulisha kondoo, wachungaji hao walitafuta faida zao wenyewe na ‘walijilisha wenyewe.’ (Eze. 34:7-10; Yer. 23:1) Mungu amekataa viongozi wa dini zinazojiita kuwa za Kikristo kwa sababu kama hizo. Yehova alikataa wachungaji ambao hawakuwa waaminifu, wazee pia wanajifunza nini kutokana na jambo hilo? Wazee wanapaswa kuhangaikia kondoo wa Yehova kwa upendo.

“NILIWEKA KIELELEZO KWA AJILI YENU”

8. Wazee wanapaswa kutenda namna gani wanaposhauri wengine?

8 Kwa sababu ya kutokamilika, inaweza kuwa vigumu kwa watu fulani katika kutaniko kuelewa waziwazi yale ambayo Yehova anapenda wafanye. Wanaweza kutenda kinyume na mashauri ya Biblia, ao kwa njia inayoonyesha kwamba hawakomae kiroho. Katika hali hiyo, wazee watatenda namna gani? Wanapaswa kuiga uvumilivu ambao Yesu alionyesha kuhusiana na wanafunzi wake walipokuwa wakibishana mara nyingi kuhusu ni nani kati yao angekuwa mukubwa zaidi katika Ufalme wa Mungu. Kuliko kuwakasirikia, Yesu aliendelea kuwafundisha kwa uvumilivu na kuwatolea mashauri yenye upendo kuhusu unyenyekevu. (Lu. 9:46-48; 22:24-27) Kwa kuwanawisha miguu, Yesu aliwafundisha unyenyekevu, sifa ambayo waangalizi Wakristo wanapaswa kuonyesha.​—Soma Yohana 13:12-15; 1 Pet. 2:21.

9. Yesu aliomba wanafunzi waepuke muelekeo gani?

9 Maoni ya Yesu kuhusu daraka la kuwa muchungaji yalitofautiana na yale ambayo Yakobo na Yohana walikuwa nayo. Mitume hao wawili walitafuta vyeo vya juu katika Ufalme wa Mungu. Lakini Yesu alisahihisha maoni yao, aliposema hivi: ‘Munajua kwamba watawala wa mataifa wanatawala watu wao kwa nguvu na wakubwa wao wanamiliki watu wao. Lakini kwenu isiwe hivyo, ila yeyote anayetaka kuwa mukubwa kati yenu sharti awe mutumishi wa wote.’ (Mt. 20:25, 26, Habari Njema Kwa Watu Wote) Mitume walipaswa kuepuka muelekeo wa kutaka “kupiga ubwana” juu ya ndugu zao, ao ‘kuwatawala kwa nguvu.’

10. Yesu anapenda wazee watendee kundi namna gani, na ni mufano gani ambao mutume Paulo aliwaachia wazee?

10 Yesu anatazamia wazee watendee kundi namna yeye mwenyewe alivyolitendea. Wanapaswa kuwa tayari kutumikia ndugu na dada zao, wala si kuwatawala. Mutume Paulo alikuwa munyenyekevu, kwa kuwa aliwaambia hivi wanaume wazee wa kutaniko la Efeso: ‘Ninyi munajua vema jinsi tangu siku ya kwanza niliyokanyaga wilaya ya Asia nilivyokuwa pamoja nanyi wakati wote, nikimutumikia Bwana nikiwa na unyenyekevu mukubwa zaidi wa akili.’ Mutume Paulo alipenda wazee hao wawe wanyenyekevu na watumike kwa bidii ili kuwasaidia wengine katika kutaniko. Alisema hivi: ‘Nimewaonyesha ninyi wazi katika mambo yote kwamba kwa kufanya kazi kwa bidii hivyo ni lazima muwasaidie wale walio zaifu.’ (Mdo. 20:18, 19, 35) Mutume Paulo aliwaambia Wakorintho kwamba yeye hakuwa bwana juu ya imani yao. Lakini, alikuwa mufanyakazi munyenyekevu kama wao, na alitaka kuwasaidia wamutumikie Yehova kwa furaha. (2 Kor. 1:24) Mutume Paulo aliwaachia wazee wa leo mufano muzuri wa unyenyekevu na wa kutumika kwa bidii.

TOA MASHAURI YANAYOTEGEMEA “NENO LA UAMINIFU”

11, 12. Namna gani muzee anaweza kumusaidia Mukristo mwenzake achukue uamuzi unaofaa?

11 Muzee wa kutaniko anapaswa ‘kushikilia imara neno la uaminifu kuhusiana na ufundi wa kufundisha.’ (Tito 1:9) Lakini anafanya hivyo “katika roho ya upole.” (Gal. 6:1) Kuliko kuwakaza ndugu na dada kutenda katika njia fulani, muchungaji muzuri anajikaza kugusa moyo wao. Muzee anaweza kumuonyesha ndugu ao dada kanuni fulani za Maandiko ambazo anaweza kufikiria anapotaka kuchukua uamuzi wa maana sana. Anaweza kumuonyesha yale ambayo vichapo vyetu vinasema kuhusu jambo hilo. Anaweza pia kumuomba ndugu ao dada afikirie ikiwa matendo yake yatamufurahisha ao kumuchukiza Yehova. Muzee anaweza kumuonyesha kwamba ni jambo la lazima kutafuta uongozi wa Mungu katika sala mbele ya kuchukua uamuzi wowote. (Met. 3:5, 6) Kisha kuzungumuzia jambo hilo pamoja na Mukristo mwenzake, muzee atamuacha yeye mwenyewe ajichukulie uamuzi.​—Rom. 14:1-4.

12 Ni Biblia pekee ndio wazee wanapaswa kutumia ili kutolea wengine maagizo. Kwa hiyo, ni jambo la maana watumie Biblia kwa ufundi na kushikamana na yale inayosema. Wakifanya hivyo, hawatatumia vibaya mamlaka yao. Tena, wako chini ya usimamizi wa Yesu, na kila mushiriki wa kutaniko atatoa hesabu mbele ya Yehova na Yesu kuhusiana na maamuzi anayochukua.​—Gal. 6:5, 7, 8.

“VIELELEZO KWA KUNDI”

Wazee wanasaidia familia zao kujitayarisha kwa ajili ya mahubiri (Ona fungu la 13)

13, 14. Wazee wanapaswa kuwa mifano kwa kundi katika mambo gani?

13 Kisha kuwashauria wanaume wazee katika kutaniko ‘wasipige ubwana juu ya wale waliokabiziwa,’ Mutume Petro aliwatia moyo ‘wawe vielelezo [mifano] kwa kundi.’ (1 Pet. 5:3) Namna gani muzee anaweza kuwa kielelezo ao mufano kwa kundi? Tufikirie sifa mbili ambazo yule ‘anayejitahidi kufikia cheo cha [daraka la] mwangalizi’ anapaswa kuonyesha. Anapaswa kuwa mwenye “utimamu wa akili” na “mwanamume anayeisimamia nyumba yake mwenyewe kwa njia nzuri.” Ikiwa muzee ana familia, anapaswa kuisimamia vizuri, kwa kuwa, ‘ikiwa mutu yeyote hajue jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kutaniko la Mungu?’ (1 Tim. 3:1, 2, 4, 5) Ili kustahili kuwa mwangalizi, mutu anapaswa kuwa na akili timamu ao akili nzuri, ni kusema, anapaswa kuelewa vizuri kanuni za Mungu na kujua namna ya kuzitumia katika maisha yake mwenyewe. Hilo litamusaidia awe mutulivu na asiyeamua mambo haraka​-haraka. Wazee wanapoonyesha sifa hizo, ndugu na dada katika kutaniko wanawatumainia.

14 Wazee wanaonyesha mufano muzuri pia wanapokuwa kwenye mustari wa mbele katika kazi ya kuhubiri. Kuhusiana na hilo, Yesu aliwaachia wazee mufano. Kuhubiri habari njema ya Ufalme kulikuwa sehemu ya maana sana ya utendaji wa Yesu duniani. Alionyesha wanafunzi wake namna kazi hiyo inapaswa kufanywa. (Mk. 1:38; Lu. 8:1) Katika siku zetu, ni jambo lenye kutia-moyo kuona ndugu na dada wakihubiri pamoja na wazee, kuona bidii ya wazee katika kazi hiyo inayookoa maisha ya watu, na kujifunza kutokana na njia zao mbalimbali za kufundisha! Wazee wanapotumia wakati wao ili kuhubiri habari njema kwa bidii ijapokuwa wana programe yenye kujaa mambo mengi, hilo linatia moyo kutaniko nzima kuhubiri kwa bidii. Wazee wanaweza pia kutolea ndugu na dada mufano muzuri kwa kutayarisha mikutano na kutoa majibu na kwa kushiriki katika mambo mengine kama vile kufanya usafi na kutunza Jumba la Ufalme.​—Efe. 5:15, 16; soma Waebrania 13:7.

Wazee wanapaswa kuwa mifano katika mahubiri (Ona fungu la 14)

‘MUTEGEMEZE WALIO ZAIFU’

15. Sababu gani wazee wanafanya ziara za uchungaji?

15 Muchungaji muzuri iko tayari kusaidia kondoo inapoumia ao kugonjwa. Vivyo hivyo, wazee wanahitaji kutenda haraka ili kushugulikia ndugu na dada wenye kuteseka ao wale wanaohitaji musaada wa kiroho. Ni lazima kuwa waangalifu sana kuhusiana na mahitaji ya kimwili ya ndugu na dada wenye kuzeeka na wagonjwa, lakini wanahitaji zaidi sana musaada wa kiroho na vitia-moyo. (1 Thes. 5:14) Vijana katika kutaniko wanaweza kuwa na matatizo mengi, kama vile kupambana na ‘tamaa zinazotokea katika ujana.’ (2 Tim. 2:22) Kwa hiyo, uchungaji unatia ndani kutembelea washiriki wa kutaniko mara kwa mara ili kujua hali zao na kuwatolea vitia-moyo vya Maandiko wanavyohitaji. Matatizo mengi yanaweza kuepukwa ikiwa wazee wanawasaidia ndugu na dada zao mbele ya mambo kuharibika zaidi.

16. Wakati ndugu ao dada anahitaji musaada wa kiroho, wazee wanaweza kufanya nini?

16 Namna gani ikiwa ndugu ao dada ana tatizo kubwa linalotia uhusiano wake na Yehova katika hatari? Yakobo, mwandikaji wa Biblia, aliuliza hivi: ‘Je, kuna yeyote mugonjwa kati yenu? Na awaite wanaume wazee wa kutaniko, nao wasali juu yake, wakimupaka mafuta katika jina la Yehova. Na sala ya imani itamuponya huyo asiyejisikia vizuri, na Yehova atamwinua. Pia ikiwa amefanya zambi, atasamehewa.’ (Yak. 5:14, 15) Hata ikiwa mutu aliye mugonjwa kiroho ‘hawaite wanaume wazee,’ wanapaswa kufanya haraka kumusaidia mara tu wanapojua hali yake. Wazee wanaposali pamoja na kwa ajili ya ndugu na dada zao na kuwategemeza wakati wa uhitaji, wanawaburudisha na kuwatia moyo kiroho wale ambao wanachunga.​—Soma Isaya 32:1, 2.

17. Wazee wanapomuiga ‘muchungaji mukubwa,’ matokeo yanakuwa nini?

17 Katika mambo yote wanayofanya katika tengenezo la Yehova, wachungaji Wakristo wanajikaza kuiga ‘muchungaji mukubwa,’ Yesu Kristo. Kwa musaada wa kiroho wa kila muchungaji, kundi linafaidika sana na linaendelea katika hali nzuri. Kwa hiyo, sisi ni wenye shukrani na tunachochewa kumusifu Muchungaji wetu muzuri zaidi, Yehova.