Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 HABARI KUU | JE, TUNAMHITAJI MUNGU?

Kwa Nini Tujiulize Swali Hilo?

Kwa Nini Tujiulize Swali Hilo?

“Je, wewe ni miongoni mwa watu wasioamini Mungu? Wengi hawaamini.” Maneno hayo yalikuwa kwenye bango lililotengenezwa na kikundi cha watu wasioamini Mungu. Wanahisi kwamba hawamhitaji Mungu.

Kwa upande mwingine, watu wengi wanaodai kumwamini Mungu hufanya maamuzi mabaya yanayoonyesha kwamba Mungu hayuko. Kasisi Mkatoliki, Salvatore Fisichella, alisema hivi kuhusu waumini wa kanisa lake: “Mtu akitazama mtindo wetu wa maisha hawezi kutambua kama sisi ni Wakristo, tunaishi kama watu wasioamini.”

Watu hawajali kwamba kuna Mungu. Wao hufikiri ni vigumu kumkaribia Mungu. Hata hivyo wao humtafuta Mungu wakati ambapo wanahitaji msaada—kana kwamba Mungu ni mtumishi wao.

Wengine hawaoni umuhimu wa kufuata mafundisho ya dini. Kwa mfano, asilimia 76 ya Wakatoliki nchini Ujerumani wanaamini kwamba ni sawa mwanamume na mwanamke kuishi pamoja kabla ya kufunga ndoa—maoni ambayo yanapingana na mafundisho ya Biblia na hata mafundisho ya kanisa. (1 Wakorintho 6:18; Waebrania 13:4) Bila shaka, mbali na Wakatoliki watu wa dini nyingine pia hawaishi kulingana na mafundisho ya dini zao. Viongozi wa dini mbalimbali husikitika kwa sababu waumini wao wanaishi sawa na watu wasioamini Mungu.

Mifano hiyo inatufanya tujiulize swali hili: Je, kweli tunamhitaji Mungu? Hilo si suala jipya. Linapatikana katika kurasa za mwanzo za Biblia. Ili tupate majibu, acheni tuchunguze baadhi ya mambo yanayotajwa kwenye kitabu cha Biblia cha Mwanzo.