Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UMUKARIBIE MUNGU

“Tazama! Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”

“Tazama! Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”

Unatamani kuwa na afya nzuri na maisha marefu wewe na familia yako? Unatamani kuishi katika dunia ambamo maumivu, mateso, na kifo yatakuwa mambo ya zamani? Dunia kama hiyo si jambo la kuwazia tu. Tofauti na wazo hilo, dunia mupya ya haki litakuwa jambo la kweli hivi karibuni, kwa sababu Yehova Mungu amekusudia hivyo. Ona namna utimizo wa kusudi lake unaelezwa katika andiko la Ufunuo 21:3-5.​—Soma.

[Mungu] atafuta kila chozi kutoka katika macho yao.” (Ufunuo 21:4) Ni machozi ya namna gani ambayo Mungu atafuta? Si machozi ya furaha ao machozi yanayolinda macho yetu. Ahadi ya Mungu inahusu machozi yanayotokezwa na mateso na huzuni. Mungu hatakausha tu machozi hayo lakini atayafuta kabisa kwa kuondoa mambo yanayotokeza machozi bila kutaka, ni kusema, mateso na huzuni.

“Kifo hakitakuwapo tena.” (Ufunuo 21:4) Ni nini kingine kimetokeza machozi mengi bila kutaka isipokuwa adui kifo? Yehova ataondoa wanadamu watiifu katika utumwa wa kifo. Atafanya hivyo namna gani? Kwa kuondoa kile kinachotokeza kifo, ni kusema, zambi tuliyoriti kutoka kwa Adamu. (Waroma 5:12) Kupitia zabihu ya ukombozi ya Yesu, Yehova atawafanya wanadamu watiifu wawe wakamilifu. * Kisha adui wa mwisho, ni kusema, kifo, ‘ataangamizwa.’ (1 Wakorintho 15:26) Wanadamu waaminifu wataishi kama Mungu alivyokusudia waishi, ni kusema, wataishi wakiwa na afya kamilifu.

“Wala . . . maumivu hayatakuwapo tena.” (Ufunuo 21:4) Ni maumivu ya namna gani ambayo hayatakuwapo tena? Ni maumivu yote ya kiakili, kimoyoni, na ya kimwili ambayo yametokana na zambi na kutokamilika na ambayo yamefanya maisha yawe mabaya sana kwa mamilioni ya watu.

Hivi karibuni watu wataishi kweli bila machozi, kifo, na maumivu. Unaweza kujiuliza, ‘Wataishi hivyo wakiwa wapi?’ ‘Je, ahadi hiyo ya Mungu inahusu labda maisha huko mbinguni?’ Hapana. Ona sababu gani tunasema hapana. Sababu ya kwanza, ahadi hiyo inaanza kwa maneno “hema la Mungu liko pamoja na wanadamu,” na wanadamu wanaishi hapa duniani. (Ufunuo 21:3) Sababu ya pili, ahadi hiyo inaeleza dunia ambamo “kifo hakitakuwapo tena,” ni kusema, dunia ambamo kifo kilikuwa kwanza lakini hakitakuwapo tena. Mbinguni hakujakuwa kifo hata siku moja, lakini kifo kimekuwa hapa duniani kwa muda murefu. Kwa hiyo, ni wazi kwamba ahadi ya Mungu ya maisha mazuri itatimizwa hapa duniani.

Mungu atakausha machozi mengi ambayo yamemwangika kwa sababu ya mateso na huzuni

Yehova anataka tuamini ahadi yake ya kuleta dunia mupya ya haki. Kisha tu kueleza baraka za wakati unaokuja, anatuhakikishia ahadi yake kwa kusema hivi: “Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Kisha anaongeza hivi: “Maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.” (Ufunuo 21:5) Unaweza kujifunza mambo mengi kuhusu namna wewe na watu ambao unapenda munaweza kuwa kati ya waabudu wenye furaha ambao wataona namna ahadi ya Mungu itakavyotimia kwa utukufu wa Mungu.

Tafazali, Mwezi Huu wa 12, Usome Maandiko Haya Katika Biblia

1 Petro sura ya 1-5; 2 Pe 1-3; 1 Yo 1-5; 2 Yo 1-13; 3 Yo 1-14; Yud 1-25 mupaka Ufunuo sura ya 1-22

^ Ili kujua mengi juu ya zabihu ya ukombozi ya Kristo, soma sura ya 5 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.