Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UWAFUNDISHE WATOTO WAKO

Yesu Kristo—Tumukumbuke Kama Mutoto Muchanga ao Kama Mufalme?

Yesu Kristo—Tumukumbuke Kama Mutoto Muchanga ao Kama Mufalme?

Katika Mwezi wa 12, watu wengi duniani pote wanaona picha za Yesu akiwa mutoto muchanga. Anatiwa katika hori, ni kusema, kisanduku kikubwa ambamo nyasi zinawekwa kwa ajili ya wanyama. Lakini tumukumbuke Yesu kama mutoto muchanga tu? * Acha basi tuzungumuzie njia ya maana sana ya kumukumbuka Yesu. Tunaweza kujifunza hilo kutokana na mambo ambayo yalitokea usiku mumoja kwa kikundi cha wachungaji katika mashamba yaliyokuwa karibu na muji wa Bethlehemu.

Malaika anawatokea wachungaji kwa gafula. Anawaambia: Leo “mwokozi ambaye ni Kristo Bwana, amezaliwa kwenu.” Malaika anawaambia pia kwamba watamukuta Yesu “akiwa amefungwa vitambaa na akiwa amelala katika hori.” Wakati uleule, malaika wengine wengi wanatokea na wanaanza ‘kumusifu Mungu.’

Ungejisikia namna gani ikiwa ungewasikia malaika hao wakimusifu Mungu?— Wachungaji wanafurahi! Wanasema hivi: ‘Na tuende moja kwa moja mupaka Bethlehemu, tukaone jambo hili ambalo limetendeka.’ Huko wanamukuta ‘Maria na vilevile Yosefu, na yule mutoto muchanga akiwa amelala katika hori.’

Bila kukawia wengine wanakuja Bethlehemu ambako Maria na Yosefu walikuwa. Wakati wachungaji wanawaambia mambo yaliyotokea, wote wanashangaa sana. Unafurahi kujua mambo hayo mazuri?— Sisi wote ambao tunamupenda Mungu tunafurahi. Sasa, acha tuone sababu gani kuzaliwa kwa Yesu kunaleta furaha kubwa. Ili kuona hivyo, ni lazima tukumbuke mambo ambayo yalitokea mbele Maria aolewe.

Siku moja, malaika anayeitwa Gabrieli anamutembelea Maria. Anamuahidi kwamba atazaa mutoto ambaye ‘atakuwa mukuu naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi.’ Gabrieli anasema tena kwamba mutoto huyo ‘atatawala akiwa mufalme, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.’

Maria anataka kujua namna gani jambo hilo litatokea, kwa sababu hajalala na mwanaume hata siku moja. Kwa hiyo Gabrieli anamufasiria hivi: “Nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika,” na “kile kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.” Ulikuwa muujiza mukubwa kabisa kumuchukua Mwana wa Mungu kutoka mbinguni na kutia uzima wake katika tumbo la uzazi la Maria ili akomae humo kama mutoto muchanga!

Umeona picha ao michezo ikionyesha “wanaume wenye hekima” ao mamajusi watatu wakimutembelea mutoto Yesu pamoja na wachungaji?— Wakati wa sikukuu ya Noeli, mambo kama hayo yanaonyeshwa kwa ukawaida. Lakini si ya kweli. Kwa kweli, wale “wanaume wenye hekima” walikuwa wanajimu ao watu wenye kutabiri matukio kwa kuangalia nyota, walikuwa wanafanya mambo ambayo Mungu anachukia. Acha tuone mambo yaliyotokea walipofika. Biblia inasema hivi: ‘Walipoingia ndani ya ile nyumba wakamuona huyo mutoto muchanga pamoja na Maria mama yake.’ Wakati huo, Yesu hakuwa tena mutoto muchanga katika hori; alikuwa mutoto aliyekuwa akiishi katika nyumba pamoja na Yosefu na Maria!

Wanaume hao wenye hekima walimupata Yesu namna gani?— Waliongozwa na “nyota,” lakini nyota hiyo haikuwaongoza Bethlehemu, iliwaongoza kwanza kwa Mufalme Herode huko Yerusalemu. Biblia inasema kwamba Herode alimutafuta Yesu ili amuue. Sasa fikiria jambo hili. Unawaza ni nani alifanya ile ambayo ilionekana kuwa nyota iwaongoze wale watu wenye elimu ya nyota kwa Herode?— Si Yehova, Mungu wa kweli, ambaye aliwaongoza, lakini ni mupinzani ao adui yake, Shetani Ibilisi!

Leo, Shetani anajaribu kufanya watu wamufikirie Yesu kuwa tu mutoto muchanga asiye na uwezo. Lakini malaika Gabrieli alimuambia Maria hivi: ‘Atatawala akiwa mufalme, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.’ Sasa Yesu anatawala akiwa Mufalme mbinguni, na hivi karibuni atawaharibu maadui wote wa Mungu. Jambo hilo ndilo tunapaswa kukumbuka kumuhusu Yesu, na ni lazima tuwaelezee wengine jambo hilo.

^ Ikiwa unasoma sehemu hii pamoja na mutoto, unapoona alama hii—, utue na umutie moyo aeleze mawazo yake.