Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Kweli Biblia ni Neno la Mungu?

Ungetazamia Neno la Mungu liwe tofauti na vitabu vingine, na Biblia ni kitabu kilicho tofauti. Mamiliare ya Biblia zimechapishwa katika mamia ya luga. Hekima ya Biblia ina uwezo wa kubadilisha watu wawe na tabia nzuri.​—Soma 1 Wathesalonike 2:13; 2 Timotheo 3:16.

Tunajua kwamba Biblia ni Neno la Mungu kwa sababu inatabiri bila makosa mambo ya wakati unaokuja. Hakuna mutu anayeweza kufanya hivyo kwa uwezo wake mwenyewe. Kwa mufano, fikiria kitabu cha Isaya. Kopi moja ya kitabu hicho iliyoandikwa miaka zaidi ya mia moja mbele ya kuzaliwa kwa Yesu ilipatikana katika pango karibu na Bahari ya Chumvi. Kopi hiyo inasema kwamba muji wa Babiloni ungebaki bila kukaliwa. Jambo hilo lilitimia miaka mingi kisha utumishi wa Yesu duniani.​—Soma Isaya 13:19, 20; 2 Petro 1:20, 21.

Biblia iliandikwa namna gani?

Biblia iliandikwa katika kipindi cha miaka 1 600 hivi. Ni watu karibu 40 walioandika Biblia, na walizungumuzia kichwa kimoja cha habari bila kupingana. Hilo liliwezekana namna gani? Mungu aliongoza mambo waliyoandika.​—Soma 2 Samweli 23:2.

Wakati fulani Mungu alizungumuza na waandikaji hao kupitia malaika, maono, ao ndoto. Mara nyingi, Mungu alitia mawazo yake katika akili ya muandikaji na kumuruhusu achague maneno ya kutumia ili kueleza ujumbe wa Mungu.​—Soma Ufunuo 1:1; 21:3-5.