Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Endelea Kuwa na Maoni Yanayofaa

Endelea Kuwa na Maoni Yanayofaa

“Maana mwanadamu akiishi miaka mingi, na aishangilie hiyo yote.”​—MHU. 11:8.

1. Ni mambo gani ambayo Yehova ametutolea yanayotusaidia tuwe wenye furaha?

 YEHOVA anataka tuwe wenye furaha, na anatutolea mambo mengi yanayotusaidia kuwa wenye furaha. Kwa mufano, ametupatia uzima. Kwa hiyo, tunaweza kutumia maisha yetu ili kumutukuza, kwa kuwa ametuvuta kwenye ibada ya kweli. (Zab. 144:15; Yoh. 6:44) Yehova anatuhakikishia kwamba anatupenda na anatusaidia tuendelee kumutumikia kwa uaminifu. (Yer. 31:3; 2 Kor. 4:16) Tunaishi katika paradiso ya kiroho, ambamo tunapata chakula kingi cha kiroho na ndugu na dada wanaotupenda. Zaidi ya hilo, tuna tumaini nzuri la wakati ujao.

2. Watumishi fulani waaminifu wa Mungu wanajisikia namna gani?

2 Hata ikiwa wana sababu hizo za kuwa wenye furaha, watumishi fulani waaminifu wa Mungu wanajisikia kwamba hawafae kitu. Wanafikiri kwamba hawako wa maana kwa Yehova na kwamba utumishi wao ni wa bure. Wale wanaondelea kuwa na maoni yasiyofaa, wanaweza kufikiri kwamba kuishi “miaka mingi” ni ndoto tu. Hawana tumaini lolote katika maisha.​—Mhu. 11:8.

3. Mawazo yasiyofaa yanaweza kuletwa na nini?

3 Mawazo yasiyofaa ya ndugu na dada hao yanaweza kuletwa na magonjwa, kuvunjika moyo, ao matatizo fulani ya uzee. (Zab. 71:9; Met. 13:12; Mhu. 7:7) Zaidi ya hilo, kila Mukristo anapaswa kujua kwamba moyo ni mudanganyifu na unaweza kutulaumu hata ikiwa Mungu anapendezwa na sisi. (Yer. 17:9; 1 Yoh. 3:20) Shetani anawasingizia watumishi wa Mungu. Na wale walio na mawazo ya Shetani wanaweza kutufanya tuanze kufikiri kama Elifazi ambaye hakuwa na imani aliyeonyesha kwamba hatuko watu wa maana mbele ya Mungu. Mawazo hayo yalikuwa ya uongo katika siku za Ayubu na hata leo pia.​—Ayu. 4:18, 19.

4. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

4 Katika Biblia, Yehova anaonyesha waziwazi kwamba atawategemeza wale ‘wanaotembea katika bonde lenye kivuli kizito.’ (Zab. 23:4) Anaweza kututegemeza kupitia Neno lake. Biblia ina ‘nguvu ya Mungu kwa ajili ya kupindua ngome zenye nguvu,’ kutia ndani mawazo ya uongo na mawazo yasiyofaa. (2 Kor. 10:4, 5) Tuzungumuzie sasa namna Biblia inaweza kutusaidia tuendelee kuwa na maoni yanayofaa. Habari hii itatusaidia, na vilevile itatuonyesha namna tunavyoweza kuwatia wengine moyo.

BIBLIA INATUSAIDIA TUWE NA MAONI YANAYOFAA

5. Ni nini inaweza kutusaidia kujua kwamba tuna maoni yanayofaa?

5 Mutume Paulo alizungumuzia jambo moja linaloweza kutusaidia kuwa na maoni yanayofaa. Alitolea kutaniko la Korintho shauri hili: ‘Endeleeni kujijaribu kama ninyi muko katika imani.’ (2 Kor. 13:5) “Imani” ni mambo yote ambayo tunaamini yaliyo katika Biblia. Ikiwa maneno na matendo yetu yanapatana na mambo tunayoamini, hilo linaonyesha kwamba tuko “katika imani.” Kwa kweli, tunapaswa kuchunguza ikiwa maisha yetu yanapatana na mafundisho yote ya Kikristo. Hatupaswe kuchagua kanuni fulani ambazo tutafuata na kuzarau zingine.​—Yak. 2:10, 11.

6. Sababu gani tunapaswa kujichunguza ‘ikiwa tuko katika imani’? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

6 Unaweza kusita kufanya uchunguzi huo, zaidi sana ikiwa unafikiri kwamba una uzaifu mbalimbali. Lakini, maoni ya Yehova ndio ya maana sana kuliko yetu, na mawazo yake ni ya juu zaidi kuliko yetu. (Isa. 55:8, 9) Yeye hachunguze watumishi wake ili kutafuta makosa yao na kuwapa malipizi, lakini anawachunguza ili kuona sifa zao nzuri na kuwasaidia. Kutumia Neno la Mungu ili kuchunguza ‘ikiwa tuko katika imani,’ kutatusaidia tujione kama Mungu anavyotuona. Kufanya hivyo kutatusaidia tuepuke wazo lolote la kufikiri kwamba hatuko wa maana mbele ya Mungu na kutatusaidia tuamini uhakikisho huu ambao Biblia inatutolea. Kama vile kufungua vitambaa vya mulango ao dirisha kunaweza kufanya mwangaza wa jua uingie katika chumba chenye giza, kujua kwamba tuko watu wa maana mbele za Yehova kunaweza kututia moyo.

7. Tunapaswa kufanya nini ili tufaidike na mifano ya watu waaminifu wanaozungumuziwa katika Biblia?

7 Njia nzuri zaidi ya kujichunguza ni kutafakari juu ya mifano ya watu waaminifu wanaotajwa katika Biblia. Linganisha hali zao ao mawazo yao na yako, na ujiulize namna ambavyo wewe ungetenda ikiwa ungekuwa katika hali zao. Tuzungumuzie mifano ya watu watatu inayoonyesha namna Biblia inavyoweza kutusaidia tujichunguze ikiwa tuko “katika imani.” Mifano hiyo itatusaidia kuwa na maoni yanayofaa juu yetu wenyewe.

MUJANE MASKINI

8, 9. (a) Mujane maskini aliishi katika hali gani? (b) Pengine mujane huyo alikuwa na mawazo gani yasiyofaa?

8 Yesu aliona mujane mumoja maskini kwenye hekalu la Yerusalemu. Mufano wa mujane huyo unaweza kutusaidia tuendelee kuwa na maoni yanayofaa hata ikiwa tuko maskini. (Soma Luka 21:1-4.) Fikiria hali za mujane huyo. Alipaswa kuvumilia huzuni ya kufiwa na bwana yake na pia aliishi wakati ambao viongozi wengi wa dini walikuwa ‘wanameza nyumba za wajane’ kuliko kuwasaidia wajane ambao hawakuwa na mutu wa kuwasemea. (Lu. 20:47) Kwa kuwa alikuwa maskini sana, angeweza kutoa kwenye hekalu kiasi kinacholingana tu na mushahara ambao mufanyakazi angelipwa kisha kutumika dakika chache.

9 Jaribu kufikiria namna mujane huyo alivyojisikia alipoingia katika uwanja akibeba sarafu ao vichele vyake viwili vyenye samani ndogo. Pengine aliona muchango wake kuwa mudogo sana alipoulinganisha na ule ambao angetoa ikiwa bwana yake angekuwa angali muzima. Ao pengine alivunjika moyo alipoona michango yenye samani kubwa ya wale waliokuwa mbele yake, ao alijiuliza ikiwa muchango wake ni wa maana kabisa. Hata ikiwa alikuwa na mawazo hayo, alitoa kulingana na uwezo wake kwa ajili ya ibada ya kweli.

10. Namna gani Yesu alionyesha kwamba Mungu alimuona mujane kuwa wa maana?

10 Yesu alionyesha kwamba Yehova alipendezwa na mujane na muchango wake pia. Alisema kwamba mujane huyo ‘alitumbukiza ndani zaidi kuliko hao [matajiri] wote.’ Hata ikiwa muchango wake ulitiwa pamoja na michango ya wengine, Yesu alisifu mujane huyo. Pengine wale waliokuwa wakikusanya michango kwenye hekalu walizarau sarafu hizo mbili zenye samani ndogo na yule aliyezitoa. Lakini, namna Mungu alivyoona mujane huyo na muchango wake ndilo lilikuwa jambo la maana, wala si mawazo ya watu ao hata maoni ya mujane kuhusu hali yake. Je, unaweza kutumia mufano huo ili kuchunguza ikiwa una maoni yanayofaa kuhusu hali yako?

Mufano wa mujane maskini umekufundisha nini? (Ona fungu la 8-10)

11. Habari ya mujane inatufundisha nini?

11 Hali zako zinaweza kukutolea nafasi ya kufanya mengi ao machache katika kazi ya Yehova. Wengine hawana uwezo wa kuhubiri sana kwa sababu ya uzee ao afya mbaya. Je, wana haki ya kufikiri kwamba utendaji wao haustahili kuripotiwa? Hata ikiwa haujazeeka ao una afya nzuri, unaweza kuzarau utumishi wako unapoulinganisha na saa zote ambazo watu wa Mungu wanapitisha kila mwaka katika kazi yake. Hata hivyo, habari ya mujane maskini inatufundisha kwamba Yehova anaona na anasamini kila jambo tunalofanya katika kazi yake, zaidi sana yale tunayofanya tunapokuwa katika hali ngumu. Fikiria utumishi wako wa mwaka jana. Je, ulipaswa kujinyima mambo mengi ili upate saa moja kati ya zile ulizoripoti? Ikiwa ndiyo, uwe hakika kwamba Yehova anapendezwa sana na yale uliyofanya kwa muda wa saa hiyo moja. Tunapoiga mujane huyo maskini kwa kumutolea Yehova kulingana na uwezo wetu, tunaweza kabisa kuwa hakika kwamba tuko “katika imani.”

‘UONDOE UZIMA WANGU’

12-14. (a) Maoni yasiyofaa yalimufanya Eliya ajisikie namna gani? (b) Sababu gani Eliya alijisikia hivyo?

12 Nabii Eliya alikuwa mwaminifu kwa Yehova na alikuwa na imani yenye nguvu. Lakini, wakati fulani alivunjika moyo sana na hata alimuomba Yehova amuue aliposema hivi: ‘Sasa inatosha, Ee [Yehova]. Uondoe uzima wangu.’ (1 Fal. 19:4, Verbum Bible) Wale ambao hawajavunjika moyo kama Eliya wanaweza kuzarau sala yake na kuiona kuwa ‘mazungumuzo ya ovyoovyo’ tu. (Ayu. 6:3) Hata hivyo, alikuwa amevunjika moyo kabisa. Yehova hakumukaripia Eliya kwa sababu aliomba kufa, lakini alimusaidia.

13 Ni nini ilimufanya Eliya afikie kujisikia hivyo? Muda kidogo mbele ya jambo hilo, Eliya alifanya muujiza ulioonyesha kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli. Kisha muujiza huo, manabii 450 wa Baali waliuawa. (1 Fal. 18:37-40) Inaonekana kwamba Eliya alifikiri hilo litawasaidia watu warudilie ibada ya kweli, lakini hawakufanya hivyo. Yezebeli, Malkia muovu, alimutumia Eliya ujumbe kwamba alikuwa akifanya mipango ya kumuua. Eliya aliogopa asiuawe. Kwa hiyo, alikimbia upande wa kusini na kupita katika muji fulani wa Yuda na akaingia katika jangwa hatari.​—1 Fal. 19:2-4.

14 Alipokuwa pekee yake, Eliya alianza kufikiri kwamba kazi yake ya kuwa nabii ilikuwa ya bure. Alimuambia Yehova hivi: “Mimi si bora kuliko mababu zangu.” Alijisikia kwamba alikuwa wa bure kama vile mavumbi na mifupa ya mababu zake waliokuwa wamekufa. Alijiona kuwa asiyefaa kitu. Alifikiri kwamba hakuwa wa maana kwa Yehova wala kwa mutu mwengine yeyote.

15. Namna gani Mungu alimuhakikishia Eliya kwamba alikuwa wa maana machoni pake?

15 Lakini Mweza​-Yote alikuwa na maoni tofauti kumuelekea Eliya. Yehova aliendelea kumuona kuwa mutu wa maana na alimutendea mambo fulani ili kumuhakikishia jambo hilo. Mungu alituma malaika ili amutie Eliya moyo. Pia, alimutolea chakula na maji ili kumutegemeza muda wote wa siku 40 ya safari yake kuelekea kusini mwa Mulima Horebu. Zaidi ya hilo, Mungu alirekebisha maoni yasiyofaa ya Eliya ya kufikiri kwamba kati ya Waisraeli wote ni yeye tu aliyebaki mwaminifu kwa Yehova. Jambo la kupendeza zaidi ni kwamba, Mungu alimupatia Eliya migawo mingine, naye aliikubali. Kwa sababu alikubali musaada wa Yehova, Eliya alirudilia kazi yake ya kuwa nabii akiwa na nguvu mupya.​—1 Fal. 19:5-8, 15-19.

16. Ni njia gani ambazo Mungu ametumia ili kukutegemeza?

16 Mambo yaliyomupata Eliya yanaweza kukusaidia uchunguze ikiwa uko katika imani na kukufanya uwe na maoni yanayofaa. Kwanza, fikiria namna Yehova amekutegemeza kupitia njia mbalimbali. Pengine mutumishi fulani wa Yehova, ao muzee wa kutaniko ao Mukristo mwengine mwenye kukomaa kiroho, alikusaidia ulipohitaji musaada. (Gal. 6:2) Pengine umepata mashauri mazuri katika Biblia, katika vichapo vyetu, na kwenye mikutano. Wakati mwingine utakapofaidika kupitia moja ya njia hizo, kumbuka kwamba huo ni musaada kutoka kwa Yehova na usikose kumushukuru.​—Zab. 121:1, 2.

17. Ni mambo gani yanayomufanya Yehova apendezwe sana na watumishi wake?

17 Pili, usisahau kwamba maoni yasiyofaa yanaweza kutudanganya. Lakini namna Mungu anavyotuona ndilo jambo la maana. (Soma Waroma 14:4.) Yehova anapendezwa sana na ushikamanifu na uaminifu wetu kwake. Yehova hapendezwi nasi kwa sababu tu tunafanya mambo mengi katika kazi yake. Kama Eliya, kuna mambo mengi ambayo umefanya katika kazi ya Yehova bila wewe kujua. Pengine umesaidia ndugu na dada fulani katika kutaniko, ao watu wengi katika eneo lako wamesikia kweli kwa sababu ya bidii yako.

18. Migawo ambayo Yehova anakutolea inakuhakikishia nini?

18 Mwishowe, ona kila mugawo ambao Yehova anakutolea kuwa uhakikisho wa kwamba iko pamoja nawe. (Yer. 20:11) Kama vile Eliya, unaweza kuvunjika moyo kwa sababu haupate matokeo mazuri katika mahubiri, ao kwa sababu haufikie miradi fulani ya kiroho. Hata hivyo, una pendeleo kubwa sana la kushiriki katika kazi ya kuhubiri habari njema na kuwa mumoja wa Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo, endelea kuwa mwaminifu kwa Yehova. Ukifanya hivyo, utaweza ‘kuingia katika shangwe ya bwana wako.’​—Mt. 25:23.

‘SALA YA MUTU WENYE KUKANDAMIZWA’

19. Mwandikaji wa Zaburi ya 102 alijisikia namna gani?

19 Mwandikaji wa Zaburi ya 102 alivunjika moyo. ‘Aliteseka,’ [ao alikandamizwa] ni kusema, aliteseka sana kimwili na kuumia moyoni. Pia, alikosa nguvu ya kupambana na matatizo yake. (Zab. 102, maelezo ya utangulizi) Maneno yake yanaonyesha kwamba kila wakati alikuwa akifikiria tu maumivu yake, alijisikia kuwa peke yake, na alikuwa na maoni yasiyofaa. (Zab. 102:3, 4, 6, 11) Alifikiri kwamba Yehova alitaka kumutupilia mbali.​—Zab. 102:10.

20. Namna gani sala inaweza kumusaidia mutu aliye na maoni yasiyofaa?

20 Lakini mutunga​-zaburi angeweza tena kutumia maisha yake ili kumusifu Yehova. (Soma Zaburi 102:19-21.) Zaburi ya 102 inaonyesha kwamba, hata wale walio katika imani wanaweza kupatwa na magumu na kila mara wanaweza kufikiria tu matatizo yao. Mutunga​-zaburi alijisikia kama “ndege aliye peke yake juu ya dari.” Alifikiri kwamba magumu ndiyo yanamuzunguka kila wakati. (Zab. 102:7) Wakati wowote unapojisikia hivyo, muambie Yehova yote yaliyo katika moyo wako kama vile mutunga​-zaburi alivyofanya. Sala za mutu mwenye kukandamizwa, ni kusema, sala zako, zinaweza kukusaidia upambane na maoni yasiyofaa. Yehova anaahidi kwamba ‘atasikiliza sala ya waliovuliwa [ao maskini]; naye hatazarau sala yao.’ (Zab. 102:17) Tumainia ahadi hiyo.

21. Namna gani mutu anayepambana na mawazo yasiyofaa anaweza kuwa tena na maoni yanayofaa?

21 Zaburi ya 102 inaonyesha pia namna ya kuwa tena na maoni yanayofaa. Mutunga​-zaburi alianza kuwa tena na maoni yenye kufaa alipofikiria sana uhusiano wake pamoja na Yehova. (Zab. 102:12, 27) Alifarijiwa alipotambua kwamba kila mara Yehova iko tayari kuwategemeza watumishi Wake wanapopambana na magumu. Kwa hiyo, ikiwa mawazo yasiyofaa yanakuzuia kwa muda fulani kufanya mengi katika kazi ya Mungu, sali kuhusu tatizo hilo. Muombe Mungu asikilize sala yako. Usifanye hivyo tu ili upate kitulizo, lakini pia “ili jina la Yehova litangazwe.”​—Zab. 102:20, 21.

22. Namna gani kila mumoja wetu anaweza kumupendeza Yehova?

22 Bila shaka Biblia inatusaidia tujue ikiwa tuko katika imani na inatuonyesha kwamba sisi ni watu wa maana sana mbele za Yehova. Ni kweli kwamba, katika ulimwengu huu muovu, hatuwezi kumaliza maoni yetu yote yasiyofaa ao mambo yote yenye kuvunja moyo. Lakini, kila mumoja wetu anaweza kumupendeza Yehova na kuokolewa ikiwa anaendelea kutumikia Mungu kwa uaminifu.​—Mt. 24:13.