Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ibada ya Familia—Namna Gani Unaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?

Ibada ya Familia—Namna Gani Unaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?

Baba mumoja wa Brazili anasema hivi: “Kila mara mazungumuzo yanakuwa yenye kufurahisha sana wakati wa Ibada ya Familia ya mangaribi na ikiwa siyakatize yanaweza kuendelea mupaka usiku sana.” Baba mumoja wa familia huko Japani anasema kwamba kijana wake wa miaka kumi haangalie tena saa na anapenda mazungumuzo yaendelee. Sababu gani? Baba huyo anasema hivi: “Anaipenda sana, na inamusaidia awe mwenye furaha.”

Bila shaka, si watoto wote wanaofurahia sana ibada ya familia. Sababu gani? Baba mumoja wa Togo alitoa shauri hili: “Ibada ya Yehova haipaswe kuwa yenye kuchokesha.” Ikiwa inakuwa yenye kuchokesha, je, hilo linatokana na namna inavyoongozwa? Familia nyingi zimetambua kwamba ibada ya familia inaweza kuleta “furaha tele” kama Isaya alivyosema kuhusu Sabato.​—Isa. 58:13, 14.

Baba Wakristo wanatambua kwamba ili washiriki wa familia wafurahie zaidi ibada ya familia, inapaswa kufanywa katika hali yenye kupendeza. Ndugu Ralf, aliye na binti watatu na kijana mumoja, anasema kwamba ibada yao ya familia inafanywa kama mazungumuzo, hapana kama masomo; kwa sababu kila mutu anashiriki katika mazungumuzo. Hata hivyo, wakati fulani inaweza kuwa vigumu kufanya kila mutu aendelee kuifurahia na kushiriki katika mazungumuzo. Mama mumoja anasema hivi: “Kila mara ninashindwa kufanya ibada ya familia ifurahishe kama vile ningetaka iwe.” Siri ya kuweza ni nini?

FANYA IBADA YA FAMILIA ITIE NDANI MAMBO MBALIMBALI

Baba mumoja wa Ujerumani aliye na watoto wawili anasema hivi: “Tunapaswa kutumia njia mbalimbali za kufundisha.” Natalia, mama wa watoto wawili, anasema kwamba “jambo la maana sana ni kufanya mambo mbalimbali katika ibada ya familia, si jambo moja tu.” Wengi wanagawanya ibada yao ya familia katika sehemu mbalimbali. Cleiton, baba wa vijana wawili anayeishi huko Brazili, anaeleza hivi: “Kufanya hivyo kunasaidia ibada ya familia ipendeze zaidi, na kila mutu anafurahia kushiriki katika mazungumuzo.” Ikiwa watoto wana umri tofauti, wazazi wanaweza kufikiria mahitaji ya kila mutoto kwa kugawanya wakati wa funzo kwa sehemu mbalimbali. Wazazi wanaweza kuzungumuzia mahitaji ya kila mushiriki wa familia na kuchagua mambo yatakayozungumuziwa na namna ya kuyazungumuzia.

Familia fulani zinafanya nini ili mazungumuzo yao yatie ndani mambo mbalimbali? Familia zingine zinaanza ibada ya familia kwa kuimba nyimbo za kumusifu Yehova. Juan wa Meksiko anasema hivi: “Kufanya hivyo kunaleta hali nzuri na kunatayarisha akili zetu kwa ajili ya mazungumuzo yatakayofuata.” Familia yake inachagua nyimbo zinazohusiana na habari fulani zitakazozungumuziwa mangaribi hiyo.

Sirilanka

Familia nyingi zinasoma sehemu fulani ya Biblia pamoja. Ili ibada ya familia itie ndani mambo mengi, kila mushiriki wa familia anasoma maneno ya watu fulani wanaotajwa katika Biblia. Baba mumoja huko Japani anaonyesha kwamba “ilikuwa vigumu kidogo kusoma kwa njia hiyo mwanzoni.” Lakini vijana wake wawili walifurahi sana kuona wazazi wao wakifanya hivyo pamoja nao. Familia fulani zinacheza michezo inayohusu hadisi za Biblia. Roger, baba wa vijana wawili huko Afrika Kusini, anasema hivi: “Kila mara watoto wanavumbua katika hadisi za Biblia mambo ambayo sisi wazazi tulikuwa hatujaona.”

Afrika Kusini

Njia nyingine ya kufanya ibada ya familia itie ndani mambo mbalimbali ni kutumika pamoja ili kutimiza muradi fulani, kama vile kujenga safina ya Noa ao hekalu la Sulemani. Ili kutimiza miradi hiyo munahitaji kufanya utafiti ambao unaweza kuwa wenye kufurahisha sana. Kwa mufano, huko Asia, binti mumoja wa miaka mitano pamoja na wazazi wake na tate ao nkambo yake mwanamuke walifanya hivyo. Walifanya pamoja muchezo kwenye ubao kuhusu safari za umisionere za mutume Paulo katika chumba chao ambamo wanaikalisha wageni. Familia zingine zimefanya michezo kwenye ubao kuhusu habari zinazopatikana katika kitabu cha Kutoka. Donald wa huko Togo aliye na miaka 19, anasema kwamba kufanya mambo mbalimbali wakati wa ibada ya familia “kulileta mambo mapya katika ibada yao ya familia na katika familia yenyewe.” Je, unaweza kufikiria jambo fulani linaloweza kufanya ibada ya familia yako iwe yenye kufurahisha hata zaidi?

Amerika

NI JAMBO LA MAANA KUJITAYARISHA

Kufanya mambo mbalimbali wakati wa ibada ya familia na kubadili njia za kufundisha kunasaidia ibada ya familia ipendeze. Lakini ili ibada iwe yenye kujenga, kila mutu anapaswa kujitayarisha. Watoto wadogo wanachoka wakati fulani, kwa hiyo baba anapaswa kufikiria kwa uangalifu habari zitakazozungumuziwa na kujitayarisha vizuri. Baba mumoja anasema hivi: “Wakati ninajitayarisha vizuri, kila mutu anafaidika na funzo.” Baba mumoja wa huko Ujerumani anaambia familia yake mambo watakayozungumuzia katika majuma yanayofuata. Ikiwa amepanga familia yake itazame video inayotegemea Biblia, baba mumoja wa huko Benini aliye na watoto sita anawatolea maulizo mbele ya wakati. Bila shaka, kujitayarisha kunasaidia ibada ya familia iwe yenye kufurahisha na yenye kujenga.

Ikiwa washiriki wa familia wanajua mbele ya wakati mambo watakayochunguza, wanaweza kuyazungumuzia muda wote wa juma, na hilo linafanya wangojee ibada ya familia kwa hamu. Na ikiwa kila mushiriki anapewa mugawo fulani, ataona kuwa yeye pia anatimiza jambo fulani katika ibada ya familia.

MUJIKAZE KUIFANYA KWA UKAWAIDA

Familia nyingi zinashindwa kufanya ibada ya familia kwa ukawaida.

Baba wengi wanalazimika kutumika saa nyingi ili wapate mahitaji ya familia zao. Kwa mufano, baba mumoja wa huko Meksiko anatoka kwake saa kumi na mbili asubuhi na anarudia saa mbili ya usiku. Zaidi ya hilo, wakati fulani, munaweza kubadili programe ya Ibada ya Familia kwa sababu ya programe nyingine ya kiroho.

Hata hali iwe namna gani, tunapaswa kuazimia kufanya ibada ya familia kwa ukawaida. Loïs, wa huko Togo, aliye na miaka 11, anaeleza namna gani familia yao inavyojikaza anaposema hivi: “Hata ikiwa mambo fulani yanafanya tusiheshimu kabisa wakati wa ibada ya familia, tunajikaza siku zote ili tu ibada ya familia ifanyike.” Kwa hiyo, familia nyingi zinapanga ibada ya familia mwanzoni mwa juma. Wanafanya hivyo kwa sababu, ikiwa kunatokea jambo fulani ambalo hawakutazamia, wanaweza kupanga kufanya ibada ya familia mwishoni mwa juma.

Jina “ibada ya familia” linaonyesha kwamba programe hiyo ni sehemu ya ibada tunayomutolea Yehova. Kwa hiyo, acheni kila mushiriki wa familia amutolee Yehova kila juma ‘ngombe​-dume wachanga wa midomo yake.’ (Hos. 14:2) Na acheni kila mutu katika familia afurahie wakati huo, ‘kwa maana shangwe ya Yehova ndiyo ngome yetu.’​—Neh. 8:9, 10.