Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tuige Imani ya Musa

Tuige Imani ya Musa

‘Kwa imani, Musa alipokuwa mutu muzima, alikataa kuitwa mwana wa binti ya Farao.’—EBR. 11:24.

1, 2. (a) Alipokuwa na miaka 40, Musa alichukua uamuzi gani? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.) (b) Sababu gani Musa alichagua kuteseka pamoja na watu wa Mungu?

MUSA alijua mambo ambayo angepata huko Misri. Aliona nyumba kubwa-kubwa za matajiri. Aliishi katika nyumba ya Mufalme. ‘Alifundishwa hekima yote ya Wamisri.’ Alijifunza mambo kuhusu nyota, hesabu na sayansi zingine. (Mdo. 7:22) Alikuwa na nafasi ya kupata mali, cheo na mambo mengine ambayo kila Mumisri angetamani kuwa nayo!

2 Lakini, alipokuwa na miaka 40, Musa alichukua uamuzi ambao ulishangaza familia ya Mufalme iliyomulea. Hakuchagua hata maisha ya Mumisri wa hali ya chini, lakini alichagua kuishi pamoja na watumwa! Musa alifanya hivyo kwa sababu alikuwa na imani. (Soma Waebrania 11:24-26.) Imani yake ilimusaidia kuona mbali kuliko kuona tu mambo yaliyomuzunguka. Kwa kuwa alikuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Mungu, Musa alikuwa na imani katika Yehova, “Yeye asiyeonekana,” na aliamini ahadi zake.​—Ebr. 11:27.

3. Habari hii itajibia maulizo gani matatu?

3 Sisi pia tunapaswa kuona mbali kuliko kuona tu mambo yanayoonekana na macho ya mwanadamu. Tunapaswa kuwa “namna ya watu walio na imani.” (Ebr. 10:38, 39) Ili tuwe na imani yenye nguvu, acheni tuzungumuzie yale yaliyoandikwa kuhusu Musa kwenye andiko la Waebrania 11:24-26. Tunapochunguza habari hiyo, tutafute majibu ya maulizo haya: Namna gani imani ilimuchochea  Musa atupilie mbali tamaa za kimwili? Alipolaumiwa, namna gani imani ilimusaidia afurahie mapendeleo yake ya utumishi? Na sababu gani Musa ‘alikaza macho kwenye malipo ya sawabu [ao zawadi]’?

MUSA ALITUPILIA MBALI TAMAA ZA MWILI

4. Musa alitambua nini kuhusu ‘kufurahia zambi’?

4 Kupitia macho ya imani, Musa alitambua kwamba ‘kufurahia zambi’ kulikuwa kwa muda mufupi. Pengine watu fulani walikuwa wakifikiri kwamba hata ikiwa Misri ilizama katika ibada ya sanamu na uchawi, iliendelea kuwa serikali kubwa ya dunia, wakati ambapo watu wa Yehova walikuwa wakiteswa katika utumwa! Lakini, Musa alijua kwamba Mungu angebadilisha mambo. Hata ikiwa wale waliopenda tu kutimiza tamaa zao walionekana kuwa na maisha mazuri, Musa aliamini kwamba waovu wangefikia kuharibiwa. Kwa hiyo, aliepuka kabisa ‘kufurahia zambi kwa muda.’

5. Ni jambo gani litatusaidia tuepuke kabisa ‘kufurahia zambi kwa muda?’

5 Namna gani unaweza kuepuka kabisa ‘kufurahia zambi kwa muda’? Usisahau hata kidogo kwamba raha inayotokana na mambo mabaya ni ya muda mufupi tu. Kupitia macho ya imani, ona kwamba “ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake.” (1 Yoh. 2:15-17) Fikiria yale yatakayowapata wale wanaotenda zambi bila kutubu. Wako ‘kwenye udongo unaoteleza . . . wanapomalizwa [ao kuangamizwa] kwa matisho ya gafula!’ (Zab. 73:18, 19) Unapochochewa kufanya zambi, ujiulize hivi: ‘Ninapenda maisha yangu yawe namna gani wakati ujao?’

6. (a) Sababu gani Musa alikataa “kuitwa mwana wa binti ya Farao”? (b) Sababu gani unafikiri kwamba Musa alichukua uamuzi muzuri?

6 Imani ilimusaidia Musa achague kazi ya maana katika maisha yake. ‘Kwa imani, Musa alipokuwa mutu muzima, alikataa kuitwa mwana wa binti ya Farao.’ (Ebr. 11:24) Musa hakufikiri kwamba angemutumikia Mungu akiwa katika nyumba ya Mufalme na kutumia mali yake na mapendeleo yake ili kuwasaidia ndugu zake Waisraeli. Lakini, yeye aliazimia kumupenda Yehova kwa moyo wake wote, kwa nafsi yake yote, na kwa nguvu zake zote. (Kum. 6:5) Uamuzi ambao Musa alifanya ulimuepusha na huzuni. Hazina nyingi za Misri ambazo aliacha zingechukuliwa na Waisraeli wenyewe! (Kut. 12:35, 36) Farao mwenyewe alinyenyekezwa na kuuawa. (Zab. 136:15) Lakini, Musa aliokolewa, na Mungu alimutumia ili kuongoza kwa usalama taifa nzima la Israeli. Maisha yake yalikuwa yenye maana kabisa.

7. (a) Kulingana na Mathayo 6:19-21, sababu gani tunapaswa kufanya mipango kwa ajili ya wakati wa milele? (b) Toa mufano unaoonyesha wazi tofauti iliyo kati ya hazina za kimwili na hazina za kiroho.

7 Ikiwa wewe ni kijana anayemutumikia Yehova, namna gani imani inaweza kukusaidia kuchagua kazi ya kufanya? Utatenda kwa hekima ikiwa unafanya mipango kwa ajili ya wakati ujao. Lakini, je, imani katika ahadi za Mungu itakuchochea kufanya mipango kwa ajili ya mambo ambayo hayatafanya muda murefu ao kwa ajili ya wakati ujao wa milele? (Soma Mathayo 6:19-21.) Muchezaji mumoja muzuri sana wa danse anayeitwa Sophie alijikuta katika hali hiyo. Alipewa nafasi ya kulipiwa masomo ya juu na alitamani kuwa muchezaji wa danse mwenye kujulikana sana katika Amerika. Sophie alisema hivi: “Nilipenda kusifiwa. Nilijiona kuwa muchezaji muzuri sana kuliko wenzangu wote. Hata hivyo sikuwa na furaha.” Kisha kutazama video, Vijana WanajiulizaNamna Gani Nitatumia Maisha Yangu? (Les jeunes s’interrogent — Que vais-je faire de ma vie ?) Sophie anasema hivi: “Nilitambua kwamba sifa niliyopata katika ulimwengu ilichukua nafasi ya ibada ambayo ningemutolea Yehova kwa moyo wangu wote. Nilisali sana kwa Yehova. Kisha niliacha kazi yangu ya kucheza danse.” Sophie anajisikia namna gani kuhusu uamuzi ambao alichukua? Yeye anasema hivi: “Sihuzunikie kuacha maisha yangu ya zamani. Leo, nina furaha ya kweli kabisa. Ninafanya kazi ya upainia pamoja na bwana yangu. Hatutafute kujulikana sana, na hatuna vitu vingi vya kimwili. Lakini tuna uhusiano muzuri na Yehova, tuna wanafunzi wa Biblia na miradi ya kiroho. Sina huzuni yoyote.”

8. Ni shauri gani la Biblia linaloweza kusaidia kijana aamue namna atakavyotumia maisha yake?

8 Yehova anajua mambo ya lazima kwetu.  Musa alisema hivi: ‘Yehova Mungu wako anataka nini kutoka kwako ila kumwogopa Yehova Mungu wako, ili kutembea katika njia zake zote na kumupenda yeye na kumutumikia Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote; kuzishika amri za Yehova na sheria zake ninazokuamuru wewe leo, kwa faida yako?’ (Kum. 10:12, 13) Wakati ungali kijana, chagua kazi itakayokuwezesha kumupenda Yehova na kumutumikia “kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote.” Uwe hakika kwamba kufanya hivyo ni “kwa faida yako mwenyewe.”

ALIFURAHIA KAZI YAKE

9. Eleza sababu gani pengine ingekuwa vigumu Musa atimize kazi yake.

9 Musa ‘aliona shutuma [ao lawama] ya Kristo kuwa ni utajiri mukubwa kuliko hazina za Misri.’ (Ebr. 11:26) Musa alitumwa akiwa “Kristo,” ao ‘Mutiwa-mafuta,’ kwa kuchaguliwa na Yehova ili kuwatoa Waisraeli katika Misri. Musa alijua kwamba haingekuwa rahisi kufanya kazi hiyo, na kwamba hilo lingemuletea “shutuma” ao lawama. Muda mufupi uliopita, Mwisraeli mumoja alikuwa amemuzarau Musa kwa kumwambia hivi: ‘Ni nani aliyekuweka wewe rasmi kuwa mukubwa na muamuzi juu yetu?’ (Kut. 2:13, 14) Baadaye, Musa mwenyewe alimuuliza Yehova hivi: “Farao atawezaje kunisikiliza?” (Kut. 6:12) Ili kujitayarisha na kupambana na lawama hiyo, Musa alimwambia Yehova mambo ambayo yalimuogepesha na kumuhangaisha. Namna gani Yehova alimusaidia Musa atimize daraka hilo kubwa?

10. Namna gani Yehova alimusaidia Musa ili atimize mugawo wake?

10 Kwanza, Yehova alimuhakikishia Musa hivi: “Nitakuwa pamoja nawe.” (Kut. 3:12) Pili, Yehova alimutegemeza kwa kumufasiria maana fulani ya jina lake. Alimuambia hivi: “Nitakuwa Kile Nitakachokuwa.” * (Kut. 3:14) Tatu, Mungu alimupatia Musa uwezo wa kufanya miujiza iliyohakikisha kabisa kwamba alitumwa na Mungu. (Kut. 4:2-5) Ine, Yehova alimupatia Musa mutu wa kutumika naye. Mutu huyo alikuwa Haruni ambaye pia, alikuwa musemaji wa Musa ili kumusaidia atimize mugawo wake. (Kut. 4:14-16) Mwishoni mwa maisha yake, Musa alikuwa hakika kwamba Mungu anawapatia watumishi Wake yale wanayohitaji ili kutimiza mugawo wowote ambao Anawatolea. Kwa hiyo, Musa alimuhakikishia Yoshua ambaye angechukua nafasi yake hivi: “Yehova ndiye anayepiga mwendo mbele yako. Yeye mwenyewe ataendelea kuwa pamoja nawe. Hatakutupa wala kukuacha kabisa. Usiogope wala usiingiwe na hofu.”—Kum. 31:8.

11. Sababu gani Musa alifurahia sana mugawo wake?

11 Kwa musaada wa Yehova, Musa alifurahia sana mugawo wake huo wenye kuogopesha, aliuona kuwa ‘utajiri mukubwa kuliko hazina za Misri.’ Zaidi ya hilo, Musa hangelinganisha hata kidogo pendeleo la kumutumikia Mungu Mweza-Yote na lile la kumutumikia Farao. Tena, hangelinganisha hata kidogo pendeleo lake la kuwa “Kristo,” ao mutiwa-mafuta wa Yehova na lile la kuwa mwana wa Mufalme wa Misri. Musa alibarikiwa kwa sababu alifurahia mugawo ao kazi yake. Alifurahia urafiki wa pekee pamoja na Yehova, aliyemutolea nguvu ya ajabu alipokuwa akiwaongoza Waisraeli katika Inchi ya Ahadi.​—Kum. 34:10-12.

12. Yehova ametutolea mapendeleo gani ambayo tunapaswa kufurahia?

12 Sisi pia tumetumwa na Mungu. Kupitia Mwana wake, Yehova ametutolea kazi mbalimbali, kama alivyofanya kwa Paulo na  mitume wengine. (Soma 1 Timotheo 1:12-14.) Sisi wote tuna pendeleo la kutangaza habari njema. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Ndugu na dada fulani wanatumika wakiwa watumishi wa wakati wote. Ndugu waliobatizwa wenye kukomaa wanatumikia wengine wakiwa wazee na watumishi wa huduma katika makutaniko. Hata hivyo, watu wa familia yako wasio mashahidi na wengine, wanaweza kuzarau faida ya mapendeleo yako ao kukulaumu kwa sababu ya roho yako ya kujitoa. (Mt. 10:34-37) Ikiwa wanafikia kukuvunja moyo, unaweza kuanza kujiuliza ikiwa ulichukua uamuzi muzuri ao ikiwa ni lazima utimize mugawo wako. Ukipatwa na jambo hilo, namna gani imani inaweza kukusaidia uvumilie?

13. Namna gani Yehova anatutolea yale tunayohitaji ili kutimiza migawo yetu mbalimbali?

13 Umuombe Yehova, ukiwa na imani kwamba atakutegemeza. Umuelezee mambo yanayokuogopesha na kukuhangaisha. Usisahau kwamba ni Yehova ndiye alikutolea mugawo wako na atakusaidia kuutimiza. Namna gani? Atatumia njia zilezile alizotumia ili kumusaidia Musa. Kwanza, Yehova anakuhakikishia hivi: ‘Nitakutia nguvu. Nitakusaidia kwelikweli. Nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa uadilifu.’ (Isa. 41:10) Pili, anakukumbusha kwamba yeye anatimiza ahadi zake, anasema hivi: “Mimi nimesema hilo; pia nitalitimiza.” (Isa. 46:11) Tatu, Yehova anakupa “nguvu zinazopita zile za kawaida” ili kukusaidia utimize huduma yako. (2 Kor. 4:7) Ine, ili uendelee kutimiza mugawo wako kwa uvumilivu, Baba yetu mwenye kutuhangaikia anakutolea familia ya ndugu na dada duniani pote ili ‘kuendelea kufarijiana na kujengana.’ (1 Thes. 5:11) Kwa kuwa Yehova anakutolea yale unayohitaji ili kutimiza migawo yako, imani yako itakuwa nguvu na utatambua kwamba mapendeleo uliyo nayo katika kazi yake ni utajiri mukubwa sana kuliko hazina yoyote unayoweza kupata katika dunia hii.

ALIKAZA MACHO KWENYE ZAWADI

14. Sababu gani Musa alikuwa hakika kwamba angepata zawadi?

14 Musa ‘alikaza macho kwenye malipo ya sawabu [ao zawadi].’ (Ebr. 11:26) Ijapokuwa Musa hakujua mambo mengi kuhusu wakati ujao, yeye aliacha ujuzi wake uongoze maisha yake. Kama babu yake Abrahamu, Musa alikuwa hakika kwamba Yehova anaweza kuwafufua watu waliokufa. (Lu. 20:37, 38; Ebr. 11:17-19) Musa alifanya miaka 40 katika ukimbizi na miaka 40 katika jangwa. Lakini, kwa kuwa alitazamia kupata baraka za wakati ujao, yeye hakuona kwamba alipoteza wakati  wake muda wa miaka hiyo yote. Hata ikiwa hakuwa na mafasirio yote kuhusu namna Mungu angetimiza ahadi zake, macho yake ya imani yaliona zawadi ambayo haionekane.

15, 16. (a) Sababu gani tunapaswa kukaza macho kwenye zawadi yetu? (b) Ni baraka gani ambazo tunangojea kwa hamu katika utawala wa Ufalme wa Mungu?

15 Wewe ‘unakaza macho’ kwenye zawadi yako? Kama Musa, sisi pia hatujapata mafasirio yote kuhusu ahadi za Mungu. Kwa mufano ‘hatujue wakati uliowekwa’ kuhusu ziki kubwa. (Mk. 13:32, 33) Hata hivyo, tunajua mengi kuhusu Paradiso ya wakati ujao kuliko Musa. Hata ikiwa hatuna mafasirio yote, Mungu ametutolea ahadi nyingi kuhusu uzima katika Ufalme wake ambazo tunaweza ‘kukazia’ macho. Kuwa na picha nzuri ya ulimwengu mupya katika akili kutatuchochea tutafute kwanza Ufalme. Namna gani? Fikiri kidogo: Unaweza kuuza nyumba fulani ikiwa kuna mambo ambayo hauelewe vizuri kuhusu nyumba hiyo? Hapana! Vivyo hivyo, hatuwezi kutumia maisha yetu kwa kufuatia tumaini ambalo hatuelewe vizuri. Imani yetu inapaswa kutusaidia tuone vizuri na kukaza katika akili picha ya maisha katika Paradiso.

Litakuwa jambo la kufurahisha sana kuzungumuza na watumishi wa Mungu waaminifu kama vile Musa! (Ona fungu la 16)

16 Ili kufanya picha ya Ufalme wa Mungu iwe wazi zaidi katika akili yako, ‘kazia’ macho maisha yako katika Paradiso. Jiwazie kuwa katika Paradiso. Kwa mufano, unapojifunza kuhusu maisha ya watumishi wa Mungu walioishi mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, fikiria maulizo unayoweza kuwauliza wanapofufuliwa. Fikiria maulizo ambayo wanaweza kukuuliza kuhusu maisha yako katika siku za mwisho. Wazia furaha utakayokuwa nayo unapokutana na mababu zako kisha miaka mingi na unapowafasiria mipango ambayo Mungu alichukua ili wafufuliwe na kuwa na tumaini la uzima wa milele. Fikiria furaha utakayokuwa nayo unapojifunza kuhusu wanyama wengi wa pori kwa kuwatazama wakiishi kwa amani. Wazia namna utajisikia kuwa karibu sana na Yehova kadiri unavyoelekea kwenye ukamilifu.

17. Namna gani kuweka katika akili picha iliyo wazi zaidi ya zawadi yetu isiyoonekana kunaweza kutusaidia leo?

17 Kuweka katika akili picha iliyo wazi zaidi ya zawadi yetu isiyoonekana, kunatusaidia tuvumilie, tuwe na furaha, na tuchukue maamuzi yenye kutegemea wakati wetu ujao wa milele. Mutume Paulo aliwaandikia Wakristo wenzake watiwa-mafuta hivi: ‘Tukitumainia kile ambacho hatuone, sisi huendelea kukingojea kwa uvumilivu.’ (Rom. 8:25) Maneno hayo yanawahusu Wakristo wote walio na tumaini la kuishi milele. Hata ikiwa hatujapokea zawadi yetu, imani yetu ni yenye nguvu sana hivi kwamba tunaendelea kungojea kwa uvumilivu ‘malipo ya sawabu [ao zawadi].’ Kama vile Musa, hatuone miaka fulani tuliyofanya katika kazi ya Yehova kuwa ya bure. Lakini, tuko hakika kwamba “vitu vinavyoonekana ni vya muda, lakini vitu visivyoonekana ni vya milele.”—Soma 2 Wakorintho 4:16-18.

18, 19. (a) Sababu gani tunapaswa kujikaza kulinda imani yetu? (b) Tutazungumuzia nini katika habari inayofuata?

18 Imani inatusaidia kuona ‘usibitisho [ao uhakikisho] ulio wazi wa mambo halisi ingawa hayaonekane.’ (Ebr. 11:1) Mutu wa kimwili haone faida ya kumutumikia Yehova. Mutu huyo anaona hazina za kiroho kuwa ‘upumbavu.’ (1 Kor. 2:14) Lakini, sisi tunatumaini kupata uzima wa milele na kujionea ufufuo, mambo ambayo watu wa dunia hii hawaone. Kama vile wanafilozofia wa siku za mutume Paulo waliomuita ‘mupiga-mudomo’ ambaye hajue kitu, leo watu wengi wanafikiri kwamba tumaini tunalohubiri halina maana yoyote kabisa.​—Mdo. 17:18.

19 Kwa kuwa tunazungukwa na watu wasio na imani, tunapaswa kujikaza kulinda imani yetu. Muombe sana Yehova ili “imani yako isififie.” (Lu. 22:32) Endelea kutambua matokeo ya zambi, pendeleo nzuri unalo la kumutumikia Yehova, na tumaini lako la uzima wa milele. Imani ya Musa ilimusaidia aone mbali kuliko kuona tu vitu vya Misri. Katika habari inayofuata, tutazungumuzia namna imani ilimusaidia Musa amuone “Yeye asiyeonekana.”—Ebr. 11:27.

^ fu. 10 Mutu mumoja mwenye elimu ya Biblia aliandika hivi kuhusiana na maneno ya Mungu katika andiko la Kutoka 3:14: “Hakuna kitu kinachoweza kumuzuia Mungu atimize mapenzi yake . . . Jina hili [Yehova] lilikuwa ngome ya Waisraeli, liliwatolea tumaini na faraja.”