Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Ni nani hasa anayeutawala ulimwengu?

Kama Mungu ndiye anayetawala ulimwengu huu, hakungekuwa na matatizo mengi hivi

Watu wengi wanaamini kwamba Mungu wa kweli ndiye anayetawala ulimwengu huu. Lakini kama Mungu ndiye anayetawala, je, ulimwengu ungekuwa na matatizo mengi hivi? (Kumbukumbu la Torati 32:4, 5) Kulingana na Biblia, ulimwengu unaongozwa na kiumbe fulani mwovu.Soma 1 Yohana 5:19.

Ilikuwaje mpaka kiumbe mwovu akaanza kuwatawala wanadamu? Mwanzoni mwa historia ya wanadamu, malaika fulani alimwasi Mungu na akawashawishi wanadamu wawili wa kwanza waasi pia. (Mwanzo 3:1-6) Wanadamu hao waliamua kumtii malaika huyo mwasi, Shetani, na hivyo kukubali awe mtawala wao. Mungu Mweza-Yote ndiye Mtawala anayestahili, lakini anataka watu wakubali utawala wake kwa hiari. (Kumbukumbu la Torati 6:6; 30:16, 19) Kwa kusikitisha, wanadamu wengi wamepotoshwa na kufanya uamuzi mbaya kama ule wa wanadamu wawili wa kwanza.Soma Ufunuo 12:9.

Ni nani atakayetatua matatizo yanayowapata wanadamu?

Je, Mungu ataruhusu utawala mwovu wa Shetani uendelee? Hapana! Mungu atamtumia Yesu kuondoa uovu ambao umesababishwa na Shetani.Soma 1 Yohana 3:8.

Yesu atatumia mamlaka aliyopewa na Mungu kumwangamiza Shetani. (Waroma 16:20) Kisha, Mungu atawatawala wanadamu na kuwarudishia maisha yenye furaha na amani kama alivyokusudia mwanzoni.Soma Ufunuo 21:3-5.