Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 Kichwa | MAWAZO YA MUNGU JUU YA KUVUTA TUMBAKU

Tatizo Lenye Kuenea Katika Dunia Yote

Tatizo Lenye Kuenea Katika Dunia Yote

Kuvuta tumbaku ni muuaji asiyechoka.

  • Kuvuta tumbaku kuliua watu 100000000 katika miaka mia moja iliyopita.

  • Kunaua watu 6000000 hivi kila mwaka.

  • Kwa kukadiria, kunaua mutu mumoja kila sekunde sita.

Na hakuna alama inayoonyesha kuwa kutakuwa badiliko.

Watu wenye mamlaka wanakadiria kwamba ikiwa hali zinazoonekana leo juu ya kuvuta tumbaku zinaendelea, kufikia mwaka wa 2030, hesabu ya vifo vinavyotokana na kuvuta tumbaku itaongezeka na kufikia 8000000. Na wanatabiri kwamba kuvuta tumbaku kutaua watu 1000000000 kufikia mwisho wa miaka kati ya 2001 na 2100.

Haiko wavutaji wa tumbaku tu ndio wanakufa na tumbaku. Watu wanaokufa na tumbaku wanatia ndani watu wa familia ya mutu aliyekufa kwa sababu ya kuvuta tumbaku wanaosumbuliwa na matatizo ya moyoni na ukosefu wa feza, na pia watu 600000 wanaokufa kila mwaka kwa sababu ya kupumua moshi wa tumbaku ijapokuwa hawavute tumbaku. Tatizo hilo linaenea kwa kila mutu kwa sababu linaongeza garama za matunzo.

Tofauti na magonjwa yenye kuenea haraka yanayofanya waganga wapambane ili kuvumbua dawa, tatizo hilo linaweza kumalizwa na namna ya kulimaliza inajulikana vizuri. Musomi Margaret Chan, kiongozi mukubwa wa Shirika la Afya Ulimwenguni, alisema hivi: “Tatizo linaloenea sana la tumbaku lililetwa na wanadamu, na linaweza kumalizwa kupitia bidii nyingi ya serikali na watu.”

Tatizo la kuvuta tumbaku limepiganishwa sana katika dunia yote. Katika Mwezi wa 8, 2012, inchi 175 hivi zilikubaliana kuchukua hatua za kukataza kuvuta tumbaku. * Hata hivyo, kuna sababu kubwa zinazofanya tatizo hilo lenye kuenea liendelee. Kila mwaka, watengenezaji wa tumbaku wanatumia mamiliare ya dola katika kufanya matangazo ili kuvutia wavutaji wapya wa tumbaku, zaidi sana kati ya wanawake na vijana wakubwa wanaoishi katika inchi zinazoendelea. Kwa sababu ya uwezo wa tumbaku wa kumufanya mutu kuwa mutumwa, hesabu ya watu wanaokufa juu ya kuvuta tumbaku itaendelea kuongezeka kati ya watu miliare moja ambao tayari ni watumwa wa tumbaku. Ikiwa watu wanaovuta tumbaku sasa hawaache, hesabu ya vifo itaongezeka sana katika miaka 40 inayokuja.

Matangazo ya tumbaku na kufanywa kuwa mutumwa wa tumbaku vimefanya watu wengi wabanwe na tabia hiyo hata ikiwa wanapenda kuiacha. Naoko alipitia hali hiyo. Alianza kuvuta tumbaku akiwa kijana. Kuiga namna tabia hiyo inaonyeshwa katika vyombo vya kutangaza habari kulimufanya ajisikie kuwa mutu wa hali ya juu. Hata ikiwa aliona wazazi wake wote wawili wanakufa na kansa ya mapafu, aliendelea kuvuta tumbaku, hata akilea watoto wake wawili wanawake. Anasema hivi: “Nilikuwa ninaogopa kupata kansa ya mapafu na nilikuwa ninaogopa pia juu ya afya ya watoto wangu, lakini sikuweza kuacha tabia hiyo. Niliwaza kuwa singeweza kuacha kuvuta tumbaku.”

Lakini, Naoko aliacha kuvuta tumbaku. Kitu chenye kimesaidia mamilioni ya watu waache kuvuta tumbaku kilimusaidia pia aache tabia hiyo. Ni kitu gani? Tafazali, soma habari inayofuata.

^ fu. 11 Hatua hizo zinatia ndani kufundisha watu juu ya hatari za kuvuta tumbaku, kukataza biashara ya tumbaku, kuongeza kodi za tumbaku, na kuunda programu za kusaidia watu waache kuvuta tumbaku.