Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Lazima Umupende Yehova Mungu Wako’

‘Lazima Umupende Yehova Mungu Wako’

‘Lazima umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.’MT. 22:37.

1. Ni nini iliyofanya Mungu na Mwana wake waendelee kupendana sana?

YESU KRISTO, Mwana wa Yehova, alisema hivi: ‘Ninamupenda Baba.’ (Yoh. 14:31) Alisema tena hivi: ‘Baba anamupenda Mwana.’ (Yoh. 5:20) Hilo halipaswe kutushangaza kwa sababu, kwa muda miaka mingi mbele aje duniani, Yesu alikuwa “stadi [ao fundi] wa kazi” wa Mungu. (Met. 8:30) Kadiri Yehova na Yesu waliendelea kufanya kazi pamoja, Mwana alijifunza mambo mengi kuhusu sifa za Baba yake na alikuwa na sababu nyingi za kumupenda. Kwa hiyo, kufanya mambo pamoja kulifanya waendelee kupendana sana.

2. (a) Upendo unamaanisha nini? (b) Tutazungumuzia maulizo gani?

2 Upendo unamaanisha kujisikia unapendezwa ao unafurahia sana mutu fulani. Mutunga-zaburi Daudi aliimba hivi: ‘Ninakupenda wewe, Ee Yehova, nguvu zangu.’ (Zab. 18:1) Sisi pia tunapaswa kumupenda Mungu, kwa sababu yeye pia anatupenda. Ikiwa tunamutii Yehova, atatupenda. (Soma Kumbukumbu la Torati 7:12, 13.) Lakini, kwa kuwa hatuwezi kumuona Mungu, inawezekana tumupende kabisa? Kumupenda Yehova kunamaanisha nini? Sababu gani tunapaswa kumupenda? Na namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunamupenda Mungu?

 INAWEZEKANA KUMUPENDA MUNGU

3, 4. Sababu gani inawezekana tumupende Yehova?

3 Hatuwezi kumuona Mungu kwa sababu yeye ni “Roho.” (Yoh. 4:24) Hata hivyo, inawezekana kumupenda Yehova, na Maandiko yanatuambia kwamba tunapaswa kumupenda. Kwa mufano, Musa aliwaambia Waisraeli hivi: ‘Lazima umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote.’—Kum. 6:5.

4 Inawezekana tumupende Mungu sana? Ndiyo, kwa sababu alituumba tukiwa na tamaa ya kumuabudu na alitupatia uwezo wa kuonyesha upendo. Ikiwa tunatosheleza vizuri tamaa yetu ya kumuabudu Mungu, upendo wetu kwa Mungu utaendelea kukomaa na hilo litatuletea furaha. Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho, kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao.” (Mt. 5:3) Kuhusiana na ile ambayo watu fulani wanaita tamaa tunayozaliwa nayo ya kuabudu, kitabu kimoja kimesema hivi: ‘Tunapaswa kuogopa sana, kushangaa sana, na kuonyesha heshima tunapoona namna wanadamu duniani pote wanatafuta na wanaamini kwamba kuna mutu mukubwa zaidi kuliko wote.’—Man Does Not Stand Alone, cha Abraham. C. Morrison.

5. Tunajua namna gani kwamba kumutafuta Mungu haiko kupoteza wakati?

5 Je, kumutafuta Mungu ni kupoteza wakati? Hapana, kwa sababu anataka tumupate. Mutume Paulo alieleza jambo hilo waziwazi alipokuwa akihubiria kikundi cha watu waliokusanyika kwenye Areopago. Hilo lilitokea karibu na Parthenoni, hekalu lililotolewa kwa Athena, mungu-mwanamuke aliyelinda muji wa Athene. Wazia ukiwa hapo Paulo anapozungumuza kuhusu “Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo” na kisha anaeleza kwamba ‘hakae katika mahekalu yaliyofanywa kwa mikono.’ Paulo aliongezea kwamba Mungu ‘alifanya kutoka kwa mutu mumoja kila taifa la watu, ili wakae juu ya uso wa dunia nzima, naye aliamuru nyakati na mipaka ya makao ya watu, ili wao wamutafute Mungu, ikiwa wangeweza kupapasa-papasa wakimutafuta na kwa kweli wamupate, ijapokuwa, kweli, hayuko mbali sana na kila mumoja wetu.’ (Mdo. 17:24-27) Bila shaka, watu wanaweza kumupata Mungu. Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni saba na nusu ‘wamemupata kabisa,’ na wanamupenda kwelikweli.

MAANA YA KUMUPENDA MUNGU

6. Kulingana na Yesu, ni amri gani ‘iliyo kubwa na ya kwanza’?

6 Upendo wetu kwa Yehova unapaswa kuanzia moyoni. Yesu alionyesha waziwazi jambo hilo Mufarisayo mumoja alipomuuliza hivi: ‘Mwalimu, amri iliyo kubwa katika sheria ni gani?’ Yesu alimujibia hivi: “‘Lazima umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.’ Hii ndiyo amri iliyo kubwa na ya kwanza.”—Mt. 22:34-38.

7. Inamaanisha nini kumupenda Mungu (a) kwa ‘moyo wetu wote’? (b) kwa ‘nafsi yetu yote’? (c) kwa ‘akili yetu yote’?

7 Yesu alimaanisha nini aliposema kwamba tunapaswa kumupenda Mungu kwa ‘moyo wetu wote’? Alimaanisha kwamba tunapaswa kumupenda Yehova kwa moyo wetu wote wa mufano, ni kusema, tamaa zetu, mawazo yetu ya moyoni na namna tunavyojisikia. Tunapaswa pia kumupenda kwa ‘nafsi yetu yote,’ ni kusema, uzima na mwili wetu. Zaidi ya hilo, tunapaswa kumupenda Mungu kwa ‘akili yetu yote,’ ni kusema, uwezo wetu wote wa kufikiri. Kwa kifupi, tunapaswa kumupenda Yehova sana, kwa uwezo wetu wote.

8. Kumupenda Mungu sana, kutatuchochea tufanye nini?

8 Ikiwa tunamupenda Mungu kwa moyo, nafsi, na akili yetu yote, tutajifunza Neno lake kwa bidii, tutafanya kila jambo analotuomba, na tutahubiri kwa bidii habari njema ya Ufalme. (Mt. 24:14; Rom. 12:1, 2) Kumupenda kabisa Yehova kutatufanya tuendelee kumukaribia. (Yak. 4:8) Bila shaka, haiwezekane kuonyesha hapa sababu zote zinazopaswa kutufanya tumupende  Mungu. Lakini, acheni tuzungumuzie sababu fulani.

SABABU GANI TUNAPASWA KUMUPENDA YEHOVA?

9. Sababu gani tunamupenda Yehova?

9 Yehova ndiye Muumbaji wetu na anayetutimizia mahitaji yetu. Mutume Paulo alisema hivi: “Kupitia kwake tuna uhai na tunaenda na kuwako.” (Mdo. 17:28) Yehova ametupatia dunia hii nzuri ili tuishi ndani yake. (Zab. 115:16) Anatutolea pia chakula na vitu vingine tunavyohitaji ili tuendelee kuishi. Ndiyo sababu, Paulo aliwaambia wakaaji wa Listra waliokuwa wanaabudu miungu ya uongo kwamba ‘Mungu aliye hai . . . hakujiacha mwenyewe bila ushahidi kwa kuwa alitenda mema, akiwapa ninyi mvua kutoka mbinguni na majira yenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yenu kikamili kwa chakula na uchangamufu.’ (Mdo. 14:15-17) Je, hilo haliwezi kutuchochea tumupende Muumbaji wetu Mukubwa na anayetutimizia mahitaji yetu?—Mhu. 12:1.

10. Tunapaswa kufanya nini kwa kuwa Mungu amefanya mupango ili kuondoa zambi na kifo?

10 Mungu amefanya mipango ili kuondoa zambi na kifo tulivyoriti kutoka kwa Adamu. (Rom. 5:12) Kwa kweli, ‘Mungu anapendekeza upendo wake mwenyewe kwetu kwa kuwa, tulipokuwa tungali watenda-zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.’ (Rom. 5:8) Bila shaka, tunamupenda Yehova sana kwa sababu amefanya mipango ili tusamehewe zambi zetu ikiwa tunatubu na kuonyesha imani katika zabihu ya ukombozi ya Yesu.—Yoh. 3:16.

11, 12. Ni katika njia gani Yehova ametutolea tumaini?

11 Yehova ametutolea tumaini linalojaza mioyo yetu shangwe na amani. (Rom. 15:13) Tumaini ambalo Mungu ametutolea linatusaidia tuvumilie majaribu. Wakristo watiwa-mafuta watakaokuwa ‘waaminifu hata kufikia kifo watapewa taji la uzima huko mbinguni.’ (Ufu. 2:10) Wakristo waaminifu walio na tumaini la kuishi duniani watapokea baraka za milele katika Paradiso duniani. (Lu. 23:43) Matumaini hayo yanatufanya tujisikie namna gani? Mioyo yetu inajaa furaha, amani na upendo kwa Mutoaji wa “kila zawadi njema na kila tuzo kamilifu,” sivyo?—Yak. 1:17.

12 Mungu ametutolea tumaini nzuri la ufufuo. (Mdo. 24:15) Kwa kawaida, tunahuzunika sana mutu fulani tunayemupenda anapokufa, lakini kwa sababu ya tumaini la ufufuo, hatuhuzunike kama watu wasio na tumaini. (1 Thes. 4:13) Kwa sababu ya upendo, Yehova Mungu anatamani sana kufufua wafu, zaidi sana watumishi wake waaminifu, kama vile Ayubu. (Ayu. 14:15) Wazia furaha ambayo watu watakuwa nayo wakati wataonana tena na wale watakaofufuliwa ili kuishi hapa duniani. Bila shaka, mioyo yetu inajaa upendo mwingi sana kwa Baba yetu wa mbinguni, ambaye ametutolea tumaini hilo nzuri la ufufuo!

13. Ni nini inatuhakikishia kwamba Mungu anatuhangaikia kabisa?

13 Yehova anatuhangaikia kabisa. (Soma Zaburi 34:6, 18, 19; 1 Petro 5:6, 7.) Kwa kuwa tunajua kwamba Mungu wetu mwenye upendo iko tayari kila mara kusaidia wale wanaomutumikia kwa uaminifu, tunajisikia salama katika ‘kundi la malisho yake.’ (Zab. 79:13) Zaidi ya hilo, mambo ambayo Mungu atatufanyia kupitia Ufalme wa Masiya yataonyesha waziwazi kwamba Mungu anatupenda. Kisha Yesu, Mufalme aliyechaguliwa, kuondoa jeuri, uonevu, na ubaya duniani, wanadamu watiifu wataishi kwa amani na hawatakosa kitu chochote. (Zab. 72:7, 12-14, 16) Haukubali kwamba mambo hayo yanatutolea sababu ya kumupenda Mungu anayetuhangaikia, kwa moyo, nafsi, nguvu na akili yetu yote?—Lu. 10:27.

14. Mungu ametutolea pendeleo gani nzuri sana?

14 Yehova ametutolea pendeleo nzuri sana la kuwa Mashahidi wake. (Isa. 43:10-12) Tunamupenda Mungu kwa sababu ametutolea pendeleo la kutetea mamlaka yake na kuwatolea  watu tumaini la kweli katika ulimwengu huu wenye kuchafuka. Zaidi ya hilo, tuna imani na usadikisho tunaohitaji ili kutangaza habari njema. Sababu gani? Kwa sababu ujumbe tunaotangaza unatoka katika Neno la Mungu wa kweli anayetimiza ahadi zake zote. (Soma Yoshua 21:45; 23:14.) Bila shaka kuna baraka na sababu nyingi sana za kumupenda Yehova. Lakini, namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunamupenda?

NAMNA YA KUONYESHA KWAMBA TUNAMUPENDA MUNGU

15. Kujifunza na kutumia mashauri ya Neno la Mungu kunatusaidia namna gani?

15 Jifunze Neno la Mungu kwa bidii na kutumia mashauri yake. Kufanya hivyo kunaonyesha kwamba tunamupenda Yehova na tunataka kabisa neno lake liwe ‘nuru kwa barabara yetu.’ (Zab. 119:105) Tunapopambana na matatizo, tunaweza kufarijiwa na maneno haya: ‘Moyo uliovunjika na kupondwa, Ee Mungu, hautauzarau.’ ‘Fazili zako zenye upendo, Ee Yehova, ziliendelea kunitegemeza. Fikira zangu zinazofazaisha zilipokuwa nyingi ndani yangu, faraja zako mwenyewe zilianza kuikumbatia nafsi yangu.’ (Zab. 51:17; 94:18, 19) Yehova na Yesu wanawahurumia wale wanaoteseka. (Isa. 49:13; Mt. 15:32) Kujifunza Biblia kunatusaidia tuelewe vizuri kabisa namna Yehova anavyotupenda, na hilo linatuchochea tumupende zaidi na zaidi.

16. Namna gani kusali kwa ukawaida kunatusaidia tumupende Mungu zaidi?

16 Sali kwa ukawaida. Sala zinatusaidia tuendelee kumukaribia ‘Musikiaji wa sala.’ (Zab. 65:2) Tunapotambua kwamba Mungu anajibia sala zetu, hilo linatusaidia tumupende zaidi. Kwa mufano, pengine tumetambua kwamba Mungu haruhusu tupate majaribu ambayo hatuwezi kuvumilia. (1 Kor. 10:13) Ikiwa tunamulilia kabisa Yehova tunapokuwa na wasiwasi, tunaweza kupata ‘amani ya Mungu inayozidi fikira zote.’ (Flp. 4:6, 7) Nyakati fulani, tunaweza kutoa sala ya kimya-kimya—kama Nehemia alivyofanya—na tunaweza kutambua baadaye kwamba imejibiwa. (Neh. 2:1-6) ‘Tunapodumu katika sala’ na kutambua namna Yehova anavyojibu maombi yetu, tunamupenda zaidi. Imani yetu inapojaribiwa, tunakuwa hakika kwamba Yehova atatusaidia tuvumilie.—Rom. 12:12.

17. Ikiwa tunamupenda Mungu, tutaona kuhuzuria mikutano yetu namna gani?

 17 Zoea kuhuzuria mikutano na mikusanyiko ya Kikristo. (Ebr. 10:24, 25) Waisraeli walikusanyika ili kusikiliza na kujifunza kuhusu Yehova kusudi waweze kumuogopa na kushika Sheria yake. (Kum. 31:12) Ikiwa tunamupenda Mungu kabisa, hatutaona kuhuzuria mikutano kuwa muzigo. (Soma 1 Yohana 5:3.) Kwa hiyo, tusiruhusu kitu chochote kitufanye tuzarau mikutano yetu. Hatupendi kitu chochote kitufanye tupoteze upendo wetu wa mwanzoni.—Ufu. 2:4.

18. Kumupenda Mungu kunatuchochea tufanye nini kuhusiana na habari njema?

18 Waelezee wengine kwa bidii “ile kweli ya habari njema.” (Gal. 2:5) Kumupenda Mungu kunatuchochea tuwaelezee wengine kuhusu Ufalme wa Masiya, Mwana wake mupendwa, ‘atakayepanda kwa kuitetea kweli’ kwenye Har-magedoni. (Zab. 45:4; Ufu. 16:14, 16) Ni furaha kabisa kushiriki katika kazi ya kufanya wanafunzi kwa kuwasaidia watu wajifunze kumuhusu Mungu mwenye upendo na kuhusu ulimwengu mupya ambao ameahidi!—Mt. 28:19, 20.

19. Sababu gani tunapaswa kuonyesha shukrani kwa kazi ya wazee?

19 Onyesha shukrani kwa kazi ya wazee. (Mdo. 20:28) Wazee ni zawadi kutoka kwa Yehova, na wanatumika kila mara kwa faida yetu. Wazee wako ‘kama mahali pa kujificha kutokana na upepo na mahali pa kujificha kutokana na zoruba ya mvua, kama vijito vya maji katika inchi isiyo na maji, kama kivuli cha mwamba muzito katika inchi iliyochoka.’ (Isa. 32:1, 2) Inafurahisha sana kupata mahali pa kujificha kunapotokea upepo mukali ao mvua kali! Wakati kuna jua kali, tunafurahia sana kujificha chini ya kivuli cha mwamba. Maneno hayo ya mufano yanatusaidia kuona kwamba wazee wanatusaidia tuendelee kumutumikia Yehova ijapokuwa matatizo ya maisha. Tunapotii wale wanaotuongoza, tunaonyesha kwamba sisi ni wenye shukrani sana kwa “zawadi zikiwa wanadamu” ao wazee na hilo linaonyesha kwamba tunamupenda Mungu na Kristo, ambaye ni Kichwa cha kutaniko.—Efe. 4:8; 5:23; Ebr. 13:17.

Yehova ametutolea wachungaji wanaohangaikia kabisa kundi

(Ona fungu la 19)

ENDELEA KUMUPENDA MUNGU

20. Ikiwa tunamupenda Mungu, tutatumia namna gani maneno ya Yakobo 1:22-25?

20 Ikiwa tunapenda kuwa na uhusiano muzuri pamoja na Yehova, hatupaswe kuwa ‘wasikiaji tu wa neno, lakini watendaji.’ (Soma Yakobo 1:22-25.) ‘Mutendaji’ ana imani inayozaa matendo kama vile kuhubiri kwa bidii na kutoa maelezo kwenye mikutano ya Kikristo. Kwa kuwa unamupenda Mungu kabisa, utatii “sheria kamilifu” ya Yehova inayotuonyesha kila jambo ambalo anataka tufanye.—Zab. 19:7-11.

21. Sala zetu za kutoka moyoni zinaweza kufananishwa na nini?

21 Kumupenda Yehova Mungu kutatuchochea tumukaribie kila mara katika sala yenye kutoka moyoni. Alipokuwa akizungumuzia uvumba uliokuwa ukichomwa kila siku kwenye mazabahu kulingana na agano la Sheria, mutunga-zaburi Daudi aliimba hivi: “Sala yangu na itayarishwe kama uvumba mbele zako [Yehova], kuinuliwa kwa mikono yangu kama toleo la jioni la nafaka.” (Zab. 141:2; Kut. 30:7, 8) Acheni maombi yetu ya unyenyekevu, sala zetu za kusihi, na maneno yetu ya kumusifu na kumushukuru Mungu yawe kama uvumba wenye harufu nzuri unaofananisha sala zinazokubaliwa na Mungu.—Ufu. 5:8.

22. Tutazungumuzia nini katika habari inayofuata?

22 Yesu alisema kwamba tunapaswa kumupenda Mungu na jirani yetu pia. (Mt. 22:37-39) Kama tutakavyoona katika habari inayofuata inayozungumuzia sifa hiyo, kumupenda Yehova na kanuni zake kunatusaidia kuishi vizuri na wanadamu wenzetu na kuonyesha upendo kwa majirani wetu.