Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Ulijua?

Je, Ulijua?

Watengenezaji wa mashua wa zamani walifanya nini ili kuzuia maji yasiingie katika mashua zao?

Lionel Casson, mutu mwenye elimu kuhusu mashua za zamani, anaeleza jambo lenye watengenezaji wa mashua wakati wa Waroma walifanya kisha kufunga matundu katika miunganisho ya mbao za chini za mashua zao. Lilikuwa jambo la kawaida kwao “kupaka lami [gundi] ao lami na nta kwenye miunganisho ao hata kwenye sehemu yote ya inje, na kueneza lami upande wote wa ndani.” Muda murefu mbele ya Waroma, Waakadia wa zamani na Wababiloni walitumia pia lami ili kuzuia maji yasiingie katika mashua zao.

lami ya majimaji kama hii ilijaa katika inchi zinazozungumuziwa ndani ya biblia

Maandiko ya Kiebrania yanazungumuzia ufundi wenye kufanana na huo katika andiko la Mwanzo 6:14. Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “lami” linamaanisha gundi, kitu kilichotokana na mafuta ya petroli.

Gundi ya asili ni ya aina mbili, kuna gundi ya majimaji na gundi iliyo ngumu. Watengenezaji wa mashua wa zamani walitumia gundi ya majimaji; waliipaka moja kwa moja kwenye mashua zao. Kisha kupakaliwa, gundi ya majimaji ilikauka na kuwa ngumu na kufanyiza sehemu iliyozuia maji kuingia.

Lami ilikuwa nyingi katika inchi zinazozungumuziwa ndani ya Biblia. Bonde la Sidimu, katika eneo la Bahari ya Chumvi, ‘lilikuwa limejaa mashimo ya lami.’—Mwanzo 14:10.

Watu walikuwa wanatumia njia gani ili kulinda samaki wakati wa zamani?

Samaki imekuwa chakula cha maana wakati murefu. Mbele ya kuanza kusafiri pamoja na Yesu, wamoja kati ya mitume wake walikuwa wavuvi wa samaki kwenye Bahari ya Galilaya. (Mathayo 4:18-22) Samaki fulani zilizokamatwa hapo zilitayarishwa katika “viwanda” vilivyokuwa karibu-karibu.

Muchoro kwenye mbao unaoonyesha wavuvi wa zamani wa misri

Ufundi wa kulinda samaki ambao labda ulitumiwa katika Galilaya ya zamani unaendelea kutumiwa leo katika maeneo fulani. Kwanza samaki zinaondolewa vitu vya ndani na kusafishwa na maji. Kitabu kimoja (Studies in Ancient Technology) kinaeleza mambo yanayofanywa kisha: “Chumvi ya majiwe-majiwe inapakaliwa ndani ya mashavu, kinywa, na magamba. Marundo ya samaki na chumvi yenye kufunikwa na mukeka yanapangwa moja juu ya nyingine. Kisha kufanya siku 3-5 kwenye jua, marundo hayo yanageuzwa ili yafanye tena siku zingine kama hizo. Katika kipindi hicho cha kukaushwa, samaki zinavuja maji na chumvi inaingia ndani. Kisha kukaushwa, samaki ni zenye kukaza na zinakuwa ngumu.”

Haijulikane ikiwa samaki zilizolindwa kupitia ufundi huo zilifanya muda gani. Lakini, kwa sababu Wamisri wa zamani walikuwa wanaenda Siria ili kuuzisha samaki zilizokaushwa na kutiwa chumvi, hilo linaonyesha kwamba ufundi huo ulitumika vizuri.