Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Yehova Anawajua Walio Wake”

“Yehova Anawajua Walio Wake”

‘Ikiwa yeyote anamupenda Mungu, huyo anajulikana naye.’1 KOR. 8:3.

1. Eleza habari moja ya Biblia inayoonyesha namna watumishi fulani wa Yehova walijidanganya wenyewe. (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

ASUBUHI moja, Haruni, Kuhani Mukubwa, alisimama mbele ya hema la Yehova, akiwa na chetezo (chombo kinachotumiwa ili kuchoma uvumba). Pembeni yake, Kora pamoja na wanaume 250 walikuwa pia wanachoma uvumba kwa ajili ya Yehova, kila mumoja wao akiwa na chetezo chake. (Hes. 16:16-18) Wanaume hao wote walionekana kuwa waabudu waaminifu wa Yehova. Lakini, tofauti na Haruni, wanaume hao wengine walikuwa waasi wenye kiburi waliotaka pia kuwa makuhani. (Hes. 16:1-11) Walijidanganya kwa kuwaza kwamba Mungu angekubali ibada yao. Lakini, kuwaza hivyo ilikuwa kumukosea heshima Yehova, ambaye anaweza kusoma mioyo na ambaye angeweza kuona unafiki wao.—Yer. 17:10.

2. Musa alitabiri nini, na je, maneno yake yalitimia?

2 Siku iliyotangulia, Musa alikuwa ametabiri hivi: “Asubuhi Yehova atajulisha ni nani aliye wake.” (Hes. 16:5) Kwa kweli, Yehova alifunua wazi tofauti kati ya waabudu wa kweli na waabudu wa uongo wakati ‘moto ulikuja kutoka kwa Yehova na kuwateketeza [Kora na] wale wanaume 250 waliokuwa wakitoa uvumba.’ (Hes. 16:35; 26:10) Yehova hakumuua Haruni pamoja na waasi hao; hilo lilionyesha kwamba alimukubali kuwa  kuhani mukubwa na mutumishi wake wa kweli.—Soma 1 Wakorintho 8:3.

3. (a) Ni hali gani ilitokea wakati wa mutume Paulo? (b) Paulo alijua namna gani kama Yehova angemaliza uasi uliokuwa katika kutaniko?

3 Hali kama hiyo ilitokea pia miaka 1500 baadaye, wakati wa mutume Paulo. Watu fulani waliojiita kuwa Wakristo walianza kufundisha mambo ya uongo; lakini, waliendelea kuwa katika kutaniko. Ikiwa mutu hakuwa mwangalifu hangeona tofauti kati ya waasi-imani hao na watu wengine katika kutaniko. Lakini uasi-imani wao ungetia imani ya Wakristo waaminifu katika hatari. Mbwa-mwitu hao waliovaa ngozi ya kondoo walianza ‘kupindua imani ya wengine.’ (2 Tim. 2:16-18) Hata hivyo, Yehova alikuwa anaona kwa uangalifu, na Paulo alijua jambo hilo kutokana na namna Mungu aliwatendea waasi, ni kusema, Kora na wale waliomuunga mukono miaka mingi iliyopita. Kwa hiyo, acheni tuchunguze andiko moja lenye kupendeza na tuone mambo ya lazima ambayo tunaweza kujifunza katika andiko hilo.

‘MIMI NI YEHOVA; SIBADILIKE’

4. Paulo aliamini kabisa jambo gani, na namna gani alionyesha hilo alipomuandikia Timotheo?

4 Paulo aliamini kabisa kwamba Yehova angefunua waabudu wa uongo, na angetambua wale wanaomutii. Paulo aliongozwa na roho ili kumuandikia Timotheo; na maneno ambayo alichagua yanaonyesha kwamba aliamini kabisa jambo hilo. Kisha kuzungumuzia hatari ya kiroho ambayo waasi-imani wangeleta katika kutaniko, Paulo aliandika: ‘Hata hivyo, musingi imara wa Mungu unakaa ukiwa umesimama, ukiwa na muhuri huu: Yehova anawajua walio wake, na: Kila mutu anayelitaja jina la Yehova na aukatae ukosefu wa uadilifu [ao haki].’—2 Tim. 2:18, 19.

5, 6. Ni jambo gani linalopendeza kuhusu namna Paulo alichagua maneno “musingi imara wa Mungu,” na maneno hayo yalimuchochea Timotheo namna gani?

5 Ni jambo gani linalopendeza kuhusu namna Paulo alichagua maneno yake katika andiko hilo? Hii ndiyo mahali moja tu katika Biblia ambapo tunapata maneno ‘musingi imara wa Mungu.’ Biblia inatumia neno ‘musingi’ kwa njia ya mufano kuhusu mambo mengi, kwa mufano inapotaja Yerusalemu, muji mukubwa wa Israeli ya zamani. (Zab. 87:1, 2) Daraka la Yesu katika kusudi la Yehova linalinganishwa pia na musingi. (1 Kor. 3:11; 1 Pet. 2:6) Paulo alikuwa akifikiria nini wakati aliandika kuhusu ‘musingi imara wa Mungu’?

6 Paulo anataja ‘musingi imara wa Mungu’ ili kurudilia maneno ambayo Musa alisema katika Hesabu 16:5 kuhusu Kora na wale waliomuunga mukono. Ni wazi kwamba Paulo alikuwa akizungumuzia mambo yaliyotokea wakati wa Musa ili kumutia Timotheo moyo na kumukumbusha kwamba Yehova ana uwezo wa kutambua na kuzuia matendo ya uasi. Waasi-imani hawangemuzuia Yehova kutimiza mapenzi yake katika kutaniko kama vile Kora hakumuzuia kutimiza mapenzi yake wakati wa zamani. Paulo hakueleza zaidi maana ya maneno ‘musingi imara wa Mungu.’ Lakini, bila shaka maneno yake yalimuchochea Timotheo kuwa na maoni yanayofaa na kumutumainia Yehova.

7. Sababu gani tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atatenda kwa haki na kwa uaminifu?

7 Kanuni za Yehova ni nzuri sana na haziwezi kubadilika. Zaburi 33:11 inasema hivi: “Shauri la Yehova litasimama milele; mawazo ya moyo wake ni kwa kizazi kimoja baada ya kizazi kingine.” Maandiko mengine yanasema kwamba utawala wa Yehova, upendo mwaminifu, haki, na uaminifu wake vinadumu milele. (Kut. 15:18; Zab. 106:1; 112:9; 117:2) Malaki 3:6 inasema kwamba  Yehova ‘habadilike.’ Vilevile, Yakobo 1:17 inasema kwamba Yehova “habadilike, kama kugeuka kwa kivuli.”

“MUHURI” UNAOKUKOMALISHA IMANI YETU

8, 9. Mufano wa Paulo wa “muhuri” unaweza kutufundisha nini?

8 Mufano ambao Paulo anatumia katika 2 Timotheo 2:19 unazungumuzia musingi ulio na muhuri ao ujumbe fulani. Wakati wa zamani, watu walizoea kuandika juu ya musingi wa jengo, pengine ili kuonyesha mutu aliyelijenga ao mwenye jengo hilo. Kati ya watu walioandika Biblia Paulo alikuwa wa kwanza kutumia mufano huo. * Muhuri juu ya ‘musingi imara wa Mungu’ una sehemu mbili. Kwanza, “Yehova anawajua walio wake” na pili, ‘Kila mutu anayelitaja jina la Yehova na aukatae ukosefu wa uadilifu [ao haki].’ Hilo linatukumbusha mambo ambayo tunasoma katika Hesabu 16:5.Soma.

9 Mufano wa Paulo wa “muhuri” unaweza kutufundisha nini? Watu wa Mungu wanaelewa kwamba kanuni za Yehova zinaweza kutegemea kweli mbili za maana sana: (1) Yehova anawapenda wale walio waaminifu kwake, na (2) Yehova anachukia ukosefu wa haki. Jambo hilo linahusiana namna gani na uasi katika kutaniko?

10. Matendo ya waasi-imani yalikuwa na matokeo gani juu ya Wakristo waaminifu wakati wa Paulo?

10 Inaonekana kwamba Timotheo na Wakristo wengine waaminifu walivurugika kwa sababu ya matendo ya waasi-imani waliokuwa kati yao. Pengine Wakristo fulani walijiuliza sababu gani watu kama hao waliruhusiwa kubaki katika kutaniko. Labda Wakristo waaminifu walijiuliza ikiwa kwa kweli Yehova aliona tofauti kati ya uaminifu wao na ibada yenye unafiki ya waasi-imani.—Mdo. 20:29, 30.

Matendo ya waasi-imani hayangemuvuruga Timotheo

(Ona fungu la 10-12)

11, 12. Namna gani barua ya Paulo ilitia nguvu imani ya Timotheo?

11 Bila shaka barua ya Paulo ilitia nguvu imani ya Timotheo kwa kumukumbusha mambo yaliyotokea wakati Haruni alitetewa, lakini Kora na wale waliomuunga mukono walifunuliwa, walikataliwa, na waliharibiwa. Ndiyo maana Paulo alisema kwamba, hata ikiwa kulikuwa waasi-imani katika kutaniko, Yehova angetambulisha watu wake, kama vile tu alifanya wakati wa Musa.

12 Yehova habadilike hata kidogo; kwa hiyo tunaweza kumutegemea. Anachukia ukosefu wa haki,  na kwa wakati unaofaa atawahukumu watenda-zambi. Kwa sababu alikuwa ‘mutu anayelitaja jina la Yehova,’ Timotheo alikumbushwa pia kwamba alipaswa kuwa muangalifu ili asishawishiwe na matendo ya waasi-imani ya ukosefu wa haki. *

WAABUDU WA KWELI WATABARIKIWA

13. Tunaweza kuwa hakika na jambo gani?

13 Maneno ya Paulo yaliyoongozwa na roho yanaweza pia kutia nguvu imani yetu. Kwanza kabisa, inatia moyo kujua kwamba Yehova anaona uaminifu wetu kwake. Yeye anaona, lakini pia anapendezwa sana na watu wake. Biblia inasema: ‘Macho ya Yehova yanaenda huku na huku duniani kote ili aonyeshe nguvu zake kwa ajili ya wale ambao moyo wao ni mukamilifu kumuelekea yeye.’ (2 Nya. 16:9) Kwa hiyo, tuko hakika kabisa kwamba yote ambayo tunamufanyia Yehova “kutokana na moyo safi” si ya bure.—1 Tim. 1:5; 1 Kor. 15:58.

14. Yehova anakataa ibada ya namna gani?

14 Pia, ni vizuri kujua kwamba Yehova anakataa ibada yenye unafiki. Kwa kuwa macho yake “yanaenda huku na huku duniani kote,” anaweza kuona watu ambao hawana ‘moyo mukamilifu kumuelekea yeye.’ Andiko la Methali 3:32 linasema: “Mutu mwenye hila ni chukizo kwa Yehova.” Mutu mwenye hila ni yule anayejionyesha kuwa mutiifu lakini anafanya zambi kwa siri. Mutu mwenye hila anaweza kudanganya wengine kwa muda fulani; lakini kwa kuwa Yehova ni mweza-yote na ni mwenye haki, hilo linatuhakikishia kwamba ‘mutu anayefunika makosa yake hatafanikiwa.’—Met. 28:13; soma 1 Timotheo 5:24; Waebrania 4:13.

15. Tunapaswa kuepuka nini, na sababu gani?

15 Watumishi wengi wa Yehova wanamutumikia kwa moyo wote. Si jambo la kawaida kuona mutu fulani katika kutaniko anajifanya kimakusudi kuwa muabudu wa uongo. Lakini, kwa sababu jambo hilo lilitokea wakati wa Musa na katika kutaniko la kwanza la Kikristo, linaweza pia kutokea wakati wetu. (2 Tim. 3:1, 5) Je, hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kuwa na mashaka juu ya Wakristo wenzetu, na juu ya uaminifu wao kwa Yehova? Hapana hata kidogo! Ni jambo lisilofaa kuwa na mashaka juu ya ndugu na dada bila sababu yoyote. (Soma Waroma 14:10-12; 1 Wakorintho 13:7.) Pia, kukosa kuwatumainia wengine katika kutaniko kunaweza kutuingiza katika hatari ya kiroho.

16. (a) Kila mumoja wetu anapaswa kufanya nini ili kuondoa alama yoyote ya unafiki katika moyo wake? (b) Kisanduku “ Endeleeni Kujijaribu . . . Endeleeni Kusibitisha . . .” kinaweza kutufundisha nini?

16 Kila Mukristo anapaswa ‘kuchunguza kazi [ao matendo] yake.’ (Gal. 6:4) Kwa sababu ya kutokamilika, tunaweza kuonyesha tabia hizo mbaya za udanganyifu bila sisi wenyewe kujua. (Ebr. 3:12, 13) Kwa hiyo, ni vizuri kila mara tuchunguze sababu zinazotufanya tumutumikie Yehova. Kila mumoja wetu anaweza kujiuliza: ‘Je, ninamuabudu Yehova kwa sababu ninamupenda, na kwa sababu ninakubali utawala wake? Ao ninafikiria tu baraka za kimwili ambazo ninatumaini kupata katika Paradiso?’ (Ufu. 4:11) Kwa kweli, sisi wote tunaweza kupata faida kwa kuchunguza matendo yetu na kuondoa alama yoyote ya unafiki.

FAIDA ZA KUBAKI MUAMINIFU

17, 18. Sababu gani tunapaswa kujikaza kumuabudu Yehova kwa moyo wote na kwa kweli?

17 Tunapojikaza  kumuabudu Yehova kwa moyo wote na kwa kweli, tutapata faida nyingi. Mutunga-zaburi anasema hivi: ‘Mwenye furaha ni mutu ambaye Yehova hamuhesabie kosa.’ (Zab. 32:2) Ndiyo, wale wanaoondoa unafiki moyoni mwao ni wenye furaha sasa, na watapata furaha kubwa wakati unaokuja.

18 Kwa wakati unaofaa, Yehova atafunua wote wanaotenda zambi ao ambao hawamuabudu kwa moyo wote; ataonyesha wazi ‘tofauti kati ya muadilifu na muovu, kati ya mutu anayemutumikia Mungu na mutu ambaye hajamutumikia.’ (Mal. 3:18) Tunapongojea wakati huo, tunatiwa moyo kwa kujua kwamba “macho ya Yehova yako juu ya waadilifu, na masikio yake yanaielekea dua yao.”—1 Pet. 3:12.

^ fu. 8 Andiko la Ufunuo 21:14, lililoandikwa miaka mingi kisha Paulo kumuandikia Timotheo, linataja ‘mawe 12 ya musingi’ yaliyo na majina ya mitume 12.

^ fu. 12 Habari inayofuata itazungumuzia namna tunaweza kumuiga Yehova kwa kukataa ukosefu wa haki.