Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Watu wa Yehova ‘Wanakataa Ukosefu wa Haki’

Watu wa Yehova ‘Wanakataa Ukosefu wa Haki’

‘Kila mutu anayeliitia jina la Yehova na aukatae ukosefu wa uadilifu [ao haki].’ —2 TIM. 2:19.

1. Ni jambo gani lililo la maana sana katika ibada yetu?

JE, UMEKWISHA kuona jina Yehova limeandikwa kwenye jengo fulani ao juu ya vitu fulani vinavyopatikana katika nyumba ya kuwekea vitu vya zamani? Bila shaka ulipendezwa na kufurahi sana. Zaidi ya yote, jina la Mungu ni la maana sana katika ibada yetu; sisi ni Mashahidi wa Yehova! Katika dunia yote hakuna watu wengine wanaotumia jina la Mungu kama sisi. Ni pendeleo kuitwa kwa jina la Mungu, lakini hilo linatutolea pia daraka fulani.

2. Kuitwa kwa jina la Yehova kunatutolea daraka gani?

2 Hatukubaliwe na Yehova kwa sababu tu tunaitwa kwa jina lake. Tunapaswa pia kuishi kupatana na kanuni zake. Kwa hiyo, Biblia inatukumbusha kwamba watu wa Yehova wanapaswa ‘kugeuka kutoka katika yaliyo mabaya.’ (Zab. 34:14) Mutume Paulo alieleza wazi kanuni hiyo alipoandika: ‘Kila mutu anayeliitia jina la Yehova na aukatae ukosefu wa uadilifu [haki].’ (Soma 2 Timotheo 2:19.) Tunajulikana sana kwa sababu tunatumia jina la Yehova. Lakini, namna gani tunakataa ukosefu wa uadilifu?

 EPUKA KABISA MAMBO MABAYA

3, 4. Watu wenye elimu ya Biblia wameshindwa kuelewa andiko gani, na sababu gani?

3 Tuchunguze habari inayohusiana na mambo ambayo Paulo aliandika katika 2 Timotheo 2:19. Andiko hilo linazungumuzia ‘musingi imara wa Mungu,’ kisha linataja ujumbe wenye sehemu mbili ulioandikwa juu ya musingi huo. Ni wazi kwamba sehemu ya kwanza ya ujumbe huo, ni kusema, “Yehova anawajua walio wake,” ilichukuliwa katika andiko la Hesabu 16:5. (Ona habari iliyotangulia.) Watu wenye elimu ya Biblia wameshindwa kuelewa sehemu ya pili ya ujumbe huo, ni kusema, ‘kila mutu anayeliitia jina la Yehova na aukatae ukosefu wa uadilifu.’ Sababu gani?

4 Inaonekana Paulo alikuwa akirudilia maneno ya andiko fulani. Lakini katika Maandiko ya Kiebrania hakuna andiko linalopatana na maneno ya Paulo. Sasa, mutume Paulo alikuwa akifikiria nini alipoandika: ‘Kila mutu anayeliitia jina la Yehova na aukatae ukosefu wa uadilifu’? Mbele tu Paulo aseme maneno hayo, alitaja mambo yanayozungumuziwa katika Hesabu sura ya 16 kuhusu habari ya uasi wa Kora. Je, sehemu ya pili ya ujumbe wake inahusiana pia na habari hiyo?

5-7. Ni matukio gani ya wakati wa Musa yanayotusaidia tuelewe maneno ya Paulo katika 2 Timotheo 2:19? (Ona picha mwanzoni mwa habari hii.)

5 Biblia inasema kwamba Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu, walijiunga na Kora ili kumupinga Musa na Haruni. (Hes. 16:1-5) Walionyesha wazi kwamba hawakumuheshimu Musa na walikataa kujitiisha kwa mamlaka ambayo Mungu alimupatia. Waasi hao waliendelea kubaki kati ya watu wa Yehova, na kuwatia watumishi waaminifu wa Mungu katika hatari. Wakati siku ilifika ili Yehova aonyeshe tofauti kati ya waabudu wake waaminifu, na waasi, alitoa amri iliyo wazi.

6 Tunasoma hivi: “Basi Yehova akasema na Musa, na kumuambia: ‘Sema na kusanyiko, na kuwaambia, “Ondokeni kuzunguka pande zote za maskani [ao hema] za Kora, Dathani na Abiramu!”’ Kisha Musa akaondoka na kuenda kwa Dathani na Abiramu, na wanaume wazee wa Israeli wakaenda pamoja naye. Ndipo akasema na kusanyiko, na kuwaambia: ‘Geukeni kando, tafazali, kutoka mbele ya mahema ya watu hawa waovu wala musiguse chochote kilicho chao, musije mukafagiliwa mbali katika zambi yao yote.’ Wakaondoka mara moja kutoka mbele ya maskani ya Kora, Dathani na Abiramu, kutoka pande zote.” (Hes. 16:23-27) Kisha Yehova akawaua waasi hao wote. Lakini, waabudu waaminifu, ni kusema, wale ambao waliondoka mara moja ili kuonyesha kwamba walikataa ukosefu wa uadilifu, waliokolewa.

7 Yehova anasoma mioyo! Anaona uaminifu wa watu wake. Lakini, watu wake wanapaswa kutenda bila kuchelewa, kwa kujitenga na watu wenye ukosefu wa uadilifu. Kwa hiyo, alipoandika kwamba ‘Kila mutu anayeliitia jina la Yehova aukatae ukosefu wa uadilifu,’ inaonekana Paulo alikuwa akifikiria habari inayopatikana katika Hesabu 16:5, 23-27. Hilo linaeleweka sababu mbele tu Paulo ataje maneno hayo alisema: “Yehova anawajua walio wake.”—2 Tim. 2:19.

“KATAA MASWALI YA UPUMBAVU NA YA KIJINGA”

8. Sababu gani kuliitia jina la Yehova, ao kuwa katika kutaniko la Kikristo hakutoshe?

8 Alipotaja mambo hayo yaliyotokea wakati wa Musa, Paulo alitaka kumukumbusha Timotheo kwamba ni vizuri kutenda bila kuchelewa ili kuendelea kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova. Haikutosha tu kuwa katika kutaniko la Kikristo, kama vile tu wakati wa Musa haikutosha kuliitia jina la Yehova. Waabudu waaminifu wanapaswa kukataa ukosefu wa uadilifu bila kuchelewa. Hilo  lilimaanisha nini kwa Timotheo? Na shauri hilo la Paulo lililoongozwa na roho linaweza kutufundisha nini?

9. ‘Maswali ya upumbavu na ya kijinga’ yalikuwa na matokeo gani mabaya katika kutaniko la kwanza la Kikristo?

9 Neno la Mungu linatutolea shauri nzuri juu ya aina za ukosefu wa uadilifu ambazo tunapaswa kukataa kabisa. Kwa mufano, katika mistari inayozunguka 2 Timotheo 2:19, tunaona kwamba Paulo anamuambia Timotheo ‘asipigane juu ya maneno’ na ‘aepuke kabisa maneno matupu.’ (Soma 2 Timotheo 2:14, 16, 23.) Watu fulani katika kutaniko walikuwa wakiendelesha mafundisho ya waasi-imani. Pia, inaonekana kwamba wengine walikuwa na mawazo yenye kutokeza ubishi. Hata kama mawazo hayo hayakupingana moja kwa moja na maandiko, yangeweza kutokeza migawanyiko. Yalifanya watu wawachekelee wengine na kubishana juu ya maneno. Jambo hilo liliharibu hali njema ya kiroho katika kutaniko. Kwa hiyo, Paulo alikazia ulazima wa ‘kukataa maswali ya upumbavu na ya kijinga.’

10. Tutafanya nini ikiwa tunakutana na waasi-imani?

10 Leo, watu wa Yehova hawashawishiwe sana na uasi-imani katika kutaniko. Lakini, tunapokutana na mafundisho yasiyopatana na Biblia, hata kama yanatoka wapi, tunapaswa kuyaepuka kabisa. Kubishana na waasi-imani iwe ni moja kwa moja, kwa kuandikiana nao kwa njia ya Internete, ao kwa njia nyingine yoyote ni kukosa hekima. Hata kama nia yetu ni kuwasaidia, kubishana kwa njia hiyo kunapingana na muongozo wa kiroho ambao tunatoka tu kujifunza. Lakini, kwa sababu sisi ni watu wa Yehova, tunaepuka kabisa, ni kusema, tunakataa kabisa uasi-imani.

Epuka kubishana na waasi-imani(Ona fungu la 10)

11. Ni nini inaweza kutokeza ‘maswali ya upumbavu,’ na namna gani wazee wanaweza kuwa mufano muzuri?

11 Zaidi ya uasi-imani, kuna mambo mengine ambayo yanaweza kuvuruga amani katika kutaniko. Kwa mufano, kuwa na maoni tofauti juu ya kujifurahisha kunaweza kuongoza kwenye ‘maswali ya upumbavu na ya kijinga.’ Bila shaka, wakati watu fulani wanafuatilia mambo ya kujifurahisha ambayo yanavunja kanuni za Yehova, wazee wa kutaniko hawataruhusu jambo hilo, hata kama wengine katika kutaniko hawatakubaliana nao. (Zab. 11:5; Efe. 5:3-5) Lakini, wazee wanapaswa kuwa waangalifu ili wasiwalazimishe wengine wafuate maoni yao. Wazee waaminifu wanafuata shauri hili wanalopewa: ‘Lichungeni kundi la Mungu lililo chini ya uangalizi wenu, . . . wala si kama kwa kupiga ubwana juu ya wale ambao ni uriti wa Mungu, bali kuwa vielelezo kwa kundi.’—1 Pet. 5:2, 3; soma 2 Wakorintho 1:24.

12, 13. (a) Mashahidi wa Yehova wana maoni gani kuhusu mambo ya kujifurahisha, na wanatumikisha kanuni gani za Biblia? (b) Namna gani kanuni zinazozungumuziwa katika fungu la 12 zinaweza kutumika pia katika sehemu mbalimbali za maisha yetu?

12 Kuhusu mambo ya kujifurahisha, tengenezo la Yehova halitutolee sheria juu ya filme, michezo ya video, vitabu, ao muziki ambao tunapaswa kuepuka. Sababu gani? Biblia inatia moyo kila mumoja wetu azoeze ‘nguvu zake za ufahamu . . . ili kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.’ (Ebr. 5:14) Biblia inatutolea kanuni za lazima ambazo tunaweza kufikiria tunapochagua namna fulani ya kujifurahisha. Katika sehemu zote za maisha, kusudi letu linapaswa kuwa ‘kuendelea kuhakikisha lile linalokubalika kwa Bwana.’ (Efe. 5:10) Biblia inafundisha kwamba baba wa familia wana mamlaka fulani; kwa hiyo wanaweza kuamua kukataza namna fulani ya kujifurahisha katika familia yao. *1 Kor. 11:3; Efe. 6:1-4.

13 Kanuni hizo za Biblia hazihusu  tu mambo ya kujifurahisha. Kuwa na maoni tofauti kuhusu namna ya kuvaa na kujipamba, afya na chakula, na mambo mengine ya kipekee kunaweza pia kutokeza ubishi. Kwa hiyo, ikiwa hakuna kanuni yoyote ya Biblia inayovunjwa, watu wa Yehova wataepuka kubishana juu ya mambo hayo, kwa sababu ‘mutumwa wa Bwana hahitaji kupigana, bali anahitaji kuwa mupole kwa wote.’—2 Tim. 2:24.

EPUKA MARAFIKI WABAYA!

14. Paulo alitumia mufano gani ili kukazia ulazima wa kuepuka marafiki wabaya?

14 Ni katika njia gani ingine wale ‘wanaoliitia jina la Yehova wanakataa ukosefu wa uadilifu’? Kwa kuepuka urafiki wa karibu pamoja na watu wenye ukosefu wa uadilifu. Ni jambo lenye kufaa kwamba kisha kutumia mufano wa ‘musingi imara wa Mungu’ Paulo alitumia mufano mwingine. Aliandika kuhusu “nyumba kubwa” iliyo na ‘vyombo vya zahabu na feza, na pia muna vyombo vya miti na vya udongo, na vingine ni kwa ajili ya kusudi lenye kuheshimika lakini vingine ni kwa ajili ya kusudi lenye kukosa heshima.’ (2 Tim. 2:20, 21) Kisha aliwashauria Wakristo ‘wajiepushe kabisa,’ ao wajitenge na vyombo kwa ajili ya kusudi ‘lenye kukosa heshima.’

15, 16. Mufano wa “nyumba kubwa” unaweza kutufundisha nini?

15 Mufano huo unamaanisha nini? Paulo analinganisha kutaniko la Kikristo na “nyumba kubwa” na analinganisha watu walio katika kutaniko na “vyombo,” ao vitu vilivyo katika nyumba. Katika nyumba, vyombo fulani vinaweza kuwa hatari ikiwa vimechafuliwa ao havitunzwe vizuri. Kwa hiyo mwenye nyumba atatenganisha vyombo vilivyochafuliwa, na vyombo vizuri kama vile vyombo vinavyotumiwa ili kupika chakula.

16 Vilevile, leo watu wa Yehova wanaojikaza kuwa na mwenendo muzuri wanapaswa kuepuka urafiki pamoja na watu fulani katika kutaniko, ambao kila mara hawaheshimu kanuni za  Yehova. (Soma 1 Wakorintho 15:33.) Kwa kuwa tunapaswa kuepuka watu kama hao ndani ya kutaniko, tuseme nini kuhusu watu walio inje ya kutaniko? Tunapaswa “kugeuka mbali” nao, ni kusema, kuepuka kabisa kufanya urafiki pamoja nao. Wengi kati yao ni ‘wenye kupenda pesa, wasiotii wazazi, wasio washikamanifu, wachongezi, wakali, wasiopenda wema, wasaliti, na wanaopenda raha badala ya kumupenda Mungu’!—2 Tim. 3:1-5.

YEHOVA ANATUBARIKI KWA SABABU YA UAMINIFU WETU

17. Waisraeli waaminifu walitenda namna gani ili kuonyesha kwamba hawakuunga mukono ukosefu wa uadilifu?

17 Biblia inazungumuzia wazi namna Waisraeli walitenda kwa uaminifu walipoambiwa “Ondokeni kuzunguka pande zote za maskani za Kora, Dathani, na Abiramu.” Biblia inasema kwamba ‘waliondoka mara moja.’ (Hes. 16:24, 27) Hawakuwa na wakati wa kusita-sita ao kuchelewa. Biblia inaeleza pia namna walitii kwa moyo wote. “Wakaondoka mara moja . . . kutoka pande zote.” Wale waliokuwa waaminifu hawakutaka kujiingiza katika hatari. Walitii kwa moyo wote. Walijitia upande wa Yehova na hivyo kuonyesha kwamba hawakuunga mukono ukosefu wa uadilifu. Mufano huo unaweza kutufundisha nini?

18. Paulo alikuwa akifikiria nini alipomushauria Timotheo ‘akimbie tamaa zinazotukia ujanani’?

18 Ili kulinda urafiki wetu pamoja na Yehova, tunapaswa kutenda haraka sana na bila kubadili musimamo wetu. Hayo ndiyo mawazo ambayo mutume Paulo alikuwa nayo wakati alimushauria Timotheo ‘akimbie tamaa zinazotukia ujanani.’ (2 Tim. 2:22) Wakati huo, Timotheo alikuwa mutu muzima; inawezekana alikuwa na miaka 30 hivi. Lakini, mutu anapokomaa, “tamaa zinazotukia ujanani” haziishe mara moja. Alipopambana na tamaa hizo, Timotheo alipaswa ‘kuzikimbia.’ Katika maneno mengine, Timotheo alipaswa ‘kukataa ukosefu wa uadilifu.’ Yesu alitaja jambo hilohilo aliposema: “Ikiwa jicho lako linakufanya ukwazike, ling’oe na kulitupa mbali nawe.” (Mt. 18:9) Leo, Wakristo wanatii shauri hilo wanapopambana na hatari za kiroho wakiwa na musimamo wenye nguvu bila kusitasita na bila kuchelewa.

19. Ili kujilinda na hatari za kiroho, namna gani watu fulani leo wameamua kutenda bila kuchelewa?

19 Ndugu na dada fulani ambao walikuwa walevi mbele ya kuwa Mashahidi wa Yehova wameamua kukataa kunywa tena pombe. Wengine wanaepuka namna fulani za kujifurahisha ambazo si mbaya lakini ambazo zinaweza kuwarudisha katika uzaifu fulani. (Zab. 101:3) Kwa mufano, mbele ya kuwa Shahidi wa Yehova, ndugu mumoja alikuwa anapenda sana karamu za kucheza dansi zilizokuwa na mambo mengi machafu. Lakini kisha kujifunza Biblia, aliamua kuepuka kabisa karamu za dansi, hata ikiwa karamu hizo zilifanywa na Mashahidi wenzake; hakutaka kuamusha tamaa mbaya za wakati uliopita. Bila shaka, Wakristo hawalazimishwe kuepuka kabisa pombe, kucheza dansi, ao mambo mengine ambayo si mabaya kabisa. Hata hivyo, sisi wote tunapaswa kutenda bila kukawia ili kujilinda na hatari za kiroho.

20. Hata kama si vyepesi ‘kukataa ukosefu wa uadilifu,’ tuna uhakika gani, na hilo linatutia moyo namna gani?

20 Kuitwa kwa jina la Yehova ni pendeleo, lakini hilo linatutolea pia daraka fulani. Tunapaswa ‘kukataa ukosefu wa uadilifu’ na ‘kugeuka kutoka katika yaliyo mabaya.’ (Zab. 34:14) Kwa kweli, sikuzote si vyepesi kufanya hivyo. Lakini inatia moyo kujua kwamba Yehova ataendelea kuwapenda “wale walio wake” na wanaofuata njia zake za uadilifu.—2 Tim. 2:19; soma 2 Mambo ya Nyakati 16:9a.

^ fu. 12 Ona habari “Je, Mashahidi wa Yehova Huwakataza Wafuasi wao Sinema, Vitabu, au Nyimbo Fulani?” iliyo kwenye adresi yetu ya Internete jw.org/sw, chini ya kichwa KUTUHUSU > MASWALI YANAYOULIZWA MARA NYINGI.