Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA | UFALME WA MUNGU—UNAWEZA KUKULETEA FAIDA GANI?

Ufalme wa Mungu—Utakuletea Faida Gani?

Ufalme wa Mungu—Utakuletea Faida Gani?

Labda ulielewa kupitia habari zilizotangulia kwamba Mashahidi wa Yehova wanaona Ufalme wa Mungu kuwa wa maana sana. Na labda ulipendezwa na baraka fulani za Ufalme wa Mungu za wakati unaokuja zenye zilizungumuziwa katika habari hizo. Na wakati huohuo, labda unajiuliza ikiwa ahadi hizo zitatimia kwelikweli.

Ni jambo la hekima kuwa muangalifu kuliko kuamini kila jambo unalosikia. (Methali 14:15) Kwa njia fulani, uangalifu wako unaweza kulinganishwa na ule wa Waberoya * wa zamani. Wakati waliambiwa juu ya habari njema ya ufalme, Waberoya walikubali mambo walisikia, si kwa sababu tu walipenda mambo hayo yakuwe ya kweli. Lakini, walichunguza Maandiko kwa uangalifu “ili kuona kama mambo hayo ndivyo yalivyo.” (Matendo 17:11) Kwa maneno mengine, Waberoya walilinganisha habari njema waliyosikia na mambo Maandiko yanasema. Kisha wakati fulani, walifikia kusadiki kwamba habari njema ilitegemea kabisa Neno la Mungu.

Mashahidi wa Yehova wanakuomba kwa furaha ufanye pia hivyo. Kupitia programu yetu ya kujifunza Biblia na watu bila kulipa, tunakutolea nafasi ya kulinganisha mambo sisi Mashahidi wa Yehova tunaamini juu ya Ufalme wa Mungu na mambo Biblia inafundisha.

Zaidi ya kujifunza juu ya Ufalme wa Mungu, funzo lako la Biblia linaweza kukusaidia upate majibu ya maulizo fulani ya maana sana katika maisha.

Zaidi ya yote, kujifunza Biblia kutakusaidia ‘umukaribie Mungu.’ (Yakobo 4:8) Na ukimukaribia Mungu zaidi, utaelewa zaidi namna Ufalme wa Mungu unaweza kukuletea mambo mazuri, leo na hata milele. Yesu mwenyewe alimuambia Baba yake hivi katika sala: ‘Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemutuma, Yesu Kristo.’—Yohana 17:3.

 

^ fu. 4 Beroya ulikuwa muji katika Makedonia ya zamani.