Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Sababu gani tusali Ufalme wa Mungu uje?

Ungependa kujua mengi juu ya Ufalme wa Mungu na mambo Ufalme huo utafanya?

Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni. Yesu aliwaambia wafuasi wake wasali ufalme huo uje kwa sababu utarudisha haki na amani duniani. Hakuna serikali ya watu inayoweza kumaliza kabisa-kabisa jeuri, ukosefu wa haki, na magonjwa, lakini Ufalme wa Mungu unaweza na utafanya hivyo. Mungu amemuchagua Mwana wake, Yesu, akuwe Mufalme wa Ufalme huo. Yehova amechagua pia kikundi cha wafuasi wa Yesu watawale pamoja na Yesu katika Ufalme huo.—Soma Luka 11:2; 22:28-30.

Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utawaondoa watu wote wanaopinga utawala wa Mungu. Kwa hiyo, tunapoomba Ufalme wa Mungu uje, tunaomba uje kuchukua nafasi ya serikali zote za watu.—Soma Danieli 7:13, 14; Ufunuo 11:15, 18.

Sababu gani Ufalme wa Mungu utaletea watu faida?

Yesu ni Mufalme anayestahili kwa sababu ni mwenye huruma. Kwa kuwa ni Mwana wa Mungu, ana uwezo pia wa kusaidia watu wote wanaomuomba Mungu musaada.—Soma Zaburi 72:8, 12-14.

Ufalme wa Mungu utaletea faida watu wote wanaosali kwa moyo wote uje na kuishi kupatana na mapenzi ya Mungu. Ukijifunza mambo Biblia inafundisha juu ya Ufalme wa Mungu hautajuta hata siku moja.—Soma Luka 18:16, 17; Yohana 4:23.