Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 MAZUNGUMUZO YA BIBLIA PAMOJA NA JIRANI

Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Wakati Gani? (Sehemu ya 2)

Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Wakati Gani? (Sehemu ya 2)

Habari inayofuata ni mufano wa mazungumuzo yenye Shahidi fulani wa Yehova anaweza kuwa nayo pamoja na jirani yake. Kwa mufano, Shahidi fulani anayeitwa Richard amerudia kumuona mwanaume anayeitwa Jon nyumbani kwake.

KUJIKUMBUSHA KWA KIFUPI NDOTO YA NEBUKADNEZA

Richard: Jon, ninafurahi kukuona tena. Sikuzote, ninafurahia kabisa mazungumuzo tunayofanya kila juma juu ya Biblia. * Habari za siku mingi?

Jon: Niko muzima, asante.

Richard: Ninafurahi kusikia uko muzima. Siku nilikuwa hapa, tulizungumuzia sababu gani Mashahidi wa Yehova wanasema kama Ufalme wa Mungu ulianza kutawala katika mwaka wa 1914. * Kama tulivyozungumuza, tunapata ushuhuda mukubwa katika unabii wa kitabu cha Biblia cha Danieli sura ya 4. Unakumbuka mambo yanayoelezwa katika sura hiyo?

Jon: Ndiyo, ni ndoto ya Mufalme Nebukadneza inayohusu muti mukubwa.

Richard: Ndiyo, ni vile kabisa. Katika ndoto yake, Nebukadneza aliona muti mukubwa sana uliofikia mupaka mbinguni. Alisikia malaika wa Mungu anaamuru muti huo ukatwe, lakini kisiki na mizizi yake viachwe katika udongo. Kisha “nyakati saba,” muti huo ungeota tena. * Tulizungumuzia pia sababu gani unabii huo uko na utimizo mbili. Unakumbuka utimizo wake wa kwanza?

Jon: Ni jambo fulani lililomufikia Nebukadneza mwenyewe, sivyo? Alirukwa na akili kwa miaka saba.

Richard: Hiyo ni kweli kabisa. Nebukadneza alirukwa na akili kwa wakati fulani, na kwa sababu hiyo utawala wake ulikatizwa. Lakini katika utimizo mukubwa wa unabii huo, utawala wa Mungu ungekatizwa kwa njia fulani kwa nyakati saba. Kama tulivyoona, nyakati saba zilianza wakati muji wa Yerusalemu uliharibiwa katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Kuanzia wakati huo na kuendelea, hakuna tena mufalme yeyote duniani aliyesimamia Yehova Mungu katika kutawala watu wake. Lakini, wakati nyakati hizo saba ziliisha, Mungu angeweka Mufalme mupya juu ya watu wake, mutu fulani huko mbinguni. Katika maneno mengine, kwenye mwisho wa nyakati hizo saba, Ufalme wa Mungu ungeanza kutawala mbinguni. Sasa, tumekwisha kuzungumuzia nyakati saba zilianza wakati gani. Kwa hiyo, tukitambua urefu wa nyakati hizo saba, tutajua ni wakati gani Ufalme wa Mungu ulianza kutawala. Ungali unanifuata?

Jon: Ndiyo, unanisaidia kukumbuka mambo tulizungumuza ile siku.

Richard: Sawa. Tuanze basi mazungumuzo yetu ili tuone urefu wa hizo nyakati saba. Ninatoka tu kusoma habari hiyo ili nijikumbushe mawazo ya maana. Nitajikaza kukufasiria mambo hayo.

Jon: Sawa.

 NYAKATI SABA ZINAISHA—SIKU ZA MWISHO ZINAANZA

Richard: Katika utimizo wa kwanza wa unabii huo uliomuhusu Nebukadneza, nyakati saba ilikuwa miaka saba ya kwelikweli. Lakini katika utimizo mukubwa unaohusu Ufalme wa Mungu, nyakati saba zinapaswa kuwa ndefu zaidi kupita miaka saba ya kwelikweli.

Jon: Sababu gani unasema vile?

Richard: Sababu moja ni hii: kumbuka kwamba nyakati saba zilianza wakati muji wa Yerusalemu uliharibiwa mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Tukianza kuhesabia kuanzia mwaka huo, miaka saba ya kwelikweli ingeisha mwaka wa 600 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Lakini hakuna jambo la maana lilifanyika mwaka huo linalopatana na utawala wa Mungu. Tena, kama vile tuliona wakati uliopita, mamia ya miaka iliyopita wakati Yesu alikuwa hapa duniani, alionyesha kwamba nyakati saba zilikuwa hazijaisha.

Jon: Ah, ndiyo. Ninakumbuka hilo.

Richard: Kwa hiyo, nyakati saba zinapaswa kuwa wakati murefu zaidi, lakini haiko miaka saba ya kwelikweli.

Jon: Ni miaka ngapi?

Richard: Kitabu cha Biblia cha Ufunuo, kinachofanana sana na kitabu cha Danieli, kinatusaidia kutambua kwa uhakika urefu wa zile nyakati saba. Kinaonyesha kipindi cha nyakati tatu na nusu kuwa siku 1260. * Kwa hiyo, nyakati saba, ni kusema, nyakati tatu na nusu mara mbili, zingekuwa siku 2520. Tungali pamoja?

Jon: Ndiyo, niko nakufuata. Lakini sione namna gani hilo linaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu ulianza kutawala katika mwaka wa 1914.

Richard: Sawa, acha tuone ikiwa tunaweza kufanya upatanisho kati ya mambo hayo mawili. Wakati fulani katika unabii wa Biblia, siku inafananisha mwaka. * Ikiwa tunatumia kanuni ya siku moja kuwa mwaka moja, nyakati saba zitakuwa na urefu wa miaka 2520. Tukihesabu kuenda mbele kuanzia mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, miaka 2520 inatufikisha mwaka wa 1914. * Hilo ndilo linatusaidia kujua kuwa nyakati saba ziliisha mwaka wa 1914, na mwaka huo ndio Yesu alianza kutawala akiwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Na jambo la maana zaidi ni hili: kuanzia mwaka wa 1914, kumekuwa matukio makubwa duniani, yenye Biblia ilitabiri yataonekana katika siku za mwisho.

Jon: Ni matukio gani?

Richard: Fikiria mambo Yesu alisema katika andiko la Mathayo 24:7. Kuhusu wakati angeanza kutawala huko mbinguni, Yesu alisema hivi: ‘Taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, kutakuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya inchi mahali pamoja baada ya pengine.’ Unaona? Yesu alitabiri kuwa kungekuwa njaa na matetemeko ya inchi katika kipindi hicho cha wakati. Dunia yetu imepatwa na shida nyingi za namna hiyo katika miaka mia moja iliyopita, sivyo?

Jon: Ndiyo.

Richard: Katika andiko hili, Yesu alitabiri kama kungekuwa pia vita wakati wa kuwapo kwake akiwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Na kitabu cha Biblia cha Ufunuo kilitabiri kama vita haingekuwa tu nafasi moja lakini vita mbalimbali vingegusa dunia yote wakati wa siku za mwisho. * Unakumbuka vita ya kwanza ya ulimwengu ilitokea mwaka gani?

Jon: Ilitokea katika mwaka wa 1914, mwaka uleule ambao unasema Yesu alianza kutawala! Nilikuwa sijafikiria namna mambo hayo mawili yanapatana.

Richard: Tunapochanga  pamoja mambo haya mawili, ni kusema, unabii juu ya nyakati saba na unabii mwengine mbalimbali wa Biblia kuhusu siku za mwisho, tunaona kama yanapatana kabisa. Mashahidi wa Yehova wanaamini kabisa kama Yesu alianza kutawala akiwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu katika mwaka wa 1914 na kama siku za mwisho zilianza katika mwaka huo. *

Jon: Ningali ninajaribu kuelewa mambo hayo.

Richard: Ninakuelewa kabisa. Kama vile nilikuambia wakati uliopita, iliniomba pia wakati ili kuelewa mambo hayo vizuri. Lakini kufikia hapa, ninatumaini mazungumuzo yetu yamekusaidia uone kama hata ikiwa mwaka wa 1914 hautajwe waziwazi katika Biblia, mambo Mashahidi wa Yehova wanaamini juu ya mwaka huo yanategemea Maandiko.

Jon: Ndiyo, sikuzote hilo limenifanya nipendezwe sana na ninyi, kila jambo munasema linategemea andiko. Hamuseme mawazo yenu wenyewe. Lakini, ningali ninajiuliza sababu gani mambo hayo ni magumu kuelewa. Sababu gani Mungu hakutuambia mara moja katika Biblia kama mwaka wa 1914 ndio mwaka Yesu angeanza kutawala mbinguni?

Richard: Jon, hilo ni ulizo nzuri. Kwa kweli, kuna mambo mengi yenye hayaonyeshwe waziwazi katika Maandiko. Basi, sababu gani Mungu aliandikisha Biblia kwa njia inayoomba watu wajikaze sana ili kuielewa? Labda tunaweza kuzungumuzia hilo siku ingine.

Jon: Nitafurahi sana.

Uko na ulizo fulani juu ya habari za Biblia lenye umekwisha kujiuliza? Unapenda kujua mengi juu ya mambo Mashahidi wa Yehova wanaamini ao juu ya mambo fulani wanayofanya? Ikiwa jibu ni ndiyo, usisite kuuliza ulizo hilo wakati utakutana na Shahidi wa Yehova. Atafurahi kuzungumuzia mambo hayo pamoja na wewe.

^ fu. 5 Kupitia programu yao ya kujifunza Biblia na watu bila kulipa, Mashahidi wa Yehova wanazungumuza kwa ukawaida juu ya Biblia pamoja na jirani zao.

^ fu. 24 Ona muchoro “Muti wa Ndoto ya Nebukadneza.” Katika muchoro huo, maneno M.K.Y. ni Mbele ya Kuzaliwa kwa Yesu, na K.K.Y. ni Kisha Kuzaliwa kwa Yesu.

^ fu. 30 Soma sura ya 9 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.