Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Kweli Yesu Aliwafufua Wafu?

Je, Kweli Yesu Aliwafufua Wafu?

Je, kweli Yesu aliwafufua wafu?

Yesu alimfufua Lazaro aliyekuwa amekufa kwa siku nne

Biblia inasema waziwazi kwamba Yesu aliwafufua watu waliokufa. Masimulizi hayo si hadithi tu, kwani yalifanyika wakati na mahali hususa. Kwa mfano, katika majira ya kiangazi ya mwaka wa 31 W.K., umati mkubwa ulisafiri pamoja na Yesu kutoka Kapernaumu hadi Naini. Walipofika walikutana na umati mwingine. Punde baada ya hapo kijana aliyekufa alifufuliwa na tunaweza kuamini kwa sababu ufufuo huo umesimuliwa katika Neno la Mungu, Biblia, na ulishuhudiwa na watu hao wote.—Soma Luka 7:11-15.

Yesu, pia alimfufua rafiki yake Lazaro aliyekuwa amekufa kwa siku nne. Unaweza kuamini jambo hilo pia kwa sababu lilishuhudiwa na watu wengi.—Soma Yohana 11:39-45.

Kwa nini Yesu aliwafufua wafu?

Yesu aliwafufua wafu kwa sababu alikuwa na huruma. Vilevile, alifanya hivyo ili kuonyesha kwamba Baba yake, Muumba wa viumbe vyote, alikuwa amempa nguvu za kushinda kifo.—Soma Yohana 5:21, 28, 29.

Kwa kuwa Yesu aliwafufua wafu, tunaweza kuamini ahadi zake za wakati ujao. Atawafufua watu wengi, kutia ndani wasio waadilifu ambao hawakumjua Mungu wa kweli. Watapewa nafasi ya kumjua na kumpenda Yehova Mungu.—Soma Matendo 24:15.