Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Watu Ambao Mungu wao Ni Yehova”

“Watu Ambao Mungu wao Ni Yehova”

“Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!” —ZAB. 144:15.

1. Watu wengi wenye akili wana maoni gani kuhusu jambo la kwamba Mungu iko na watumishi duniani?

WATU wengi wenye akili wanasema kwamba dini nyingi zenye zinajidai kuwa za Kikristo na dini zingine hazifanye jambo lolote ili kusaidia watu. Wamoja kati yao wanaamini kwamba dini hizo haziwezi kukubaliwa na Mungu kwa sababu ya mwenendo na mafundisho yao. Hata hivyo, wanaamini kwamba kuna watu wazuri katika dini zote na kwamba Mungu anawaona na anawakubali kuwa watumishi wake hapa duniani. Kwa hiyo, hawaone kwamba ni lazima kutoka katika dini ya uongo ili kumuabudu Yehova wakiwa tofauti na watu wengine. Lakini, Mungu pia anaona hivyo? Tutapata jibu ya ulizo hilo kwa kufikiria historia ya waabudu wa kweli wa Yehova yenye kupatikana katika Biblia.

WANAFANYA AGANO PAMOJA NA YEHOVA

2. Ni nani walikuja kuwa watu wa Yehova, na ni nini iliwatofautisha na watu wengine? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

2 Mwanzo-mwanzo wa miaka ya 1900 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Yehova alikuwa na watu wenye walikuwa tofauti na wengine. Abrahamu, ambaye aliitwa “baba ya wale  wote walio na imani,” alikuwa anasimamia mamia ya watu waliokuwa katika nyumba yake. (Rom. 4:11; Mwa. 14:14) Viongozi wa Kanaani walimuona kuwa mutu mwenye mamlaka makubwa katikati yao na walimuheshimu. (Mwa. 21:22; 23:6) Yehova alifanya agano pamoja na Abrahamu na pamoja na wazao wake. (Mwa. 17:1, 2, 19) Mungu alimuambia Abrahamu hivi: ‘Hili ndilo agano langu ambalo ninyi mutashika kati yangu na ninyi, hata uzao wako baada yako. Kila mwanaume wa kwenu lazima atahiriwe. Nayo ikuwe ishara ya agano kati yangu mimi na ninyi.’ (Mwa. 17:10, 11) Kwa hiyo, Abrahamu pamoja na wanaume wote wa nyumba yake wakatahiriwa. (Mwa. 17:24-27) Kutahiriwa ilikuwa alama yenye ilionyesha kwamba wazao wa Abrahamu tu ndio walifanya agano la pekee pamoja na Yehova.

3. Namna gani wazao wa Abrahamu walifikia kuwa wengi?

3 Yakobo ao Israeli, ambaye alikuwa mutoto wa mutoto wa Abrahamu, alikuwa na watoto 12. (Mwa. 35:10, 22b-26) Kisha, watoto hao walikuja kuwa wazee wa ukoo wa makabila 12 ya taifa la Israeli. (Mdo. 7:8) Kwa sababu ya njaa, Yakobo pamoja na watu wa nyumba yake walikimbilia katika inchi ya Misri kwenye Yosefu, mutoto wa Yakobo, alikuwa anasimamia mambo ya chakula na ambaye Farao alikuwa anatumainia sana. (Mwa. 41:39-41; 42:6) Wazao wa Yakobo waliongezeka na kuwa wengi sana, ni kusema, “kutaniko la vikundi vya watu.”—Mwa. 48:4; soma Matendo 7:17.

WANAKOMBOLEWA NA YEHOVA

4. Mwanzoni, Wamisri waliishi namna gani na wazao wa Yakobo?

4 Wazao wa Yakobo waliishi katika inchi ya Misri miaka 200 hivi, katika eneo la muto Nile lenye linaitwa Gosheni. (Mwa. 45:9, 10) Inaonekana kwamba kwa muda wa miaka karibu 100, waliishi kwa amani na Wamisri; walikuwa wanaishi katika miji midogo-midogo na kulisha mifugo yao. Farao, ambaye alimujua Yosefu na ambaye alimufurahia, aliwakaribisha kwa uchangamufu. (Mwa. 47:1-6) Wamisri walikuwa wanachukia sana wachungaji wa kondoo. (Mwa. 46:31-34) Hata hivyo, walipaswa kuvumilia Waisraeli waishi pamoja nao.

5, 6. (a) Namna gani hali ya watu wa Mungu ilibadilika katika inchi ya Misri? (b) Sababu gani Musa hakuuawa, na Yehova alifanya nini kwa ajili ya watu wake?

5 Lakini, hali ya watu wa Mungu ingebadilika kabisa. ‘Baada ya muda, mufalme mupya ambaye hakumujua Yosefu akainuka juu ya Misri. Naye akawaambia watu wake: Tazama! Watu wa wana wa Israeli ni wengi zaidi na wenye nguvu kuliko sisi. Kwa hiyo, Wamisri wakawatumikisha wana wa Israeli chini ya uonevu. Nao wakazidi kuyafanya maisha yao yakuwe machungu kwa utumwa mugumu wa kutengeneza saruji ya udongo na matofali na kwa kila namna ya utumwa shambani. Ndiyo, kila namna ya utumwa wao ambao kwa huo waliwatumia wakiwa watumwa chini ya uonevu.’—Kut. 1:8, 9, 13, 14.

6 Farao aliamuru hata kwamba watoto wote wanaume Waebrania wauawe wakati wa kuzaliwa. (Kut. 1:15, 16) Ni wakati huo ndio Musa alizaliwa. Wakati alikuwa na miezi tatu, mama yake alimuficha katika matete ya muto Nile. Kisha binti ya Farao alimupata hapo, akamuchukua, na kumufanya kuwa mutoto wake. Jambo la kufurahisha ni kwamba, katika miaka yake ya kwanza-kwanza, Musa alilelewa na Yokebedi, mama yake muaminifu, na akakuwa mutumishi mwaminifu wa Yehova. (Kut. 2:1-10; Ebr. 11:23-25) Yehova ‘aliona’ mateso ya watu wake na akaamua kutumia Musa ili kuwakomboa kutoka mikono ya wale wenye walikuwa wanawatesa. (Kut. 2:24, 25; 3:9, 10)  Kwa hiyo, wangekuwa watu ‘waliokombolewa’ na Yehova.—Kut. 15:13; soma Kumbukumbu la Torati 15:15.

WANAKUWA TAIFA

7, 8. Namna gani watu wa Yehova walifikia kuwa taifa takatifu?

7 Hata kama Yehova alikuwa hajafanya Waisraeli kuwa taifa, aliwaona kuwa watu wake. Ndiyo sababu, Musa na Haruni walitumwa ili kumuambia Farao hivi: “Hivi ndivyo Yehova Mungu wa Israeli amesema, ‘Uwaruhusu watu wangu waende zao, wakanifanyie sherehe nyikani [ao katika jangwa].’”—Kut. 5:1.

8 Ili Waisraeli wakombolewe kutoka katika utumwa wa Misri, iliomba inchi ya Misri ipigwe kwa mapigo kumi, na Farao na majeshi yake wauawe katika Bahari Nyekundu. (Kut. 15:1-4) Karibu miezi tatu kisha hapo, Yehova alifanya agano pamoja na Waisraeli kwenye Mulima Sinai na akawatolea ahadi hii: ‘Ikiwa mutaitii sauti yangu kabisa na kulishika kwa kweli agano langu, ndipo hakika mutakapokuwa mali yangu ya pekee kutoka kati ya vikundi vingine vyote vya watu, na taifa takatifu.’—Kut. 19:5, 6.

9, 10. (a) Kulingana na Kumbukumbu la Torati 4:5-8, namna gani sheria ilitofautisha Waisraeli na watu wa mataifa mengine? (b) Namna gani Waisraeli wangeonyesha kwamba wao ni “kikundi cha watu kilicho kitakatifu kwa Yehova”?

9 Wakati walikuwa katika inchi ya Misri, Waebrania walipangwa kikabila na walikuwa wanasimamiwa na baba wa familia, ao wazee wa ukoo. Wakati huo, walikuwa hawajafanywa kuwa watumwa. Baba hao wa familia, kama vile watumishi wengine wa Yehova wenye waliishi mbele yao, walikuwa na daraka la viongozi, waamuzi, na makuhani kwa ajili ya nyumba zao. (Mwa. 8:20; 18:19; Ayu. 1:4, 5) Hata hivyo, kupitia Musa, Yehova aliwapatia Waisraeli sheria yenye ingewatofautisha na watu wa mataifa mengine. (Soma Kumbukumbu la Torati 4:5-8; Zab. 147:19, 20.) Sheria ilianzisha mupango wa kuweka makuhani kwa ajili ya taifa, na ‘wazee’ ambao waliheshimiwa kwa sababu ya ujuzi na hekima yao walipewa daraka la kuwa waamuzi. (Kum. 25:7, 8) Sheria ilitoa maagizo juu ya mambo ya ibada na juu ya maisha ya kila siku kwa ajili ya taifa hilo mupya.

10 Mbele tu Waisraeli waingie katika Inchi ya Ahadi, Yehova aliwakumbusha sheria zake; kupitia Musa aliwaambia hivi: ‘Naye Yehova, amekufanya useme leo kwamba utakuwa kikundi cha watu wake, mali [yake] ya pekee, kama vile alivyokuahidi, na kwamba utashika amri zake zote na kwamba atakuweka wewe juu kuliko mataifa mengine yote ambayo ameyafanya, hilo likitokeza sifa na heshima na uzuri, huku ukijisibitisha kuwa kikundi cha watu kilicho kitakatifu kwa Yehova Mungu wako.’—Kum. 26:18, 19.

WAKAAJI WAGENI WANAKARIBISHWA

11-13. (a) Ni nani walijiunga na watu wenye Mungu alichagua? (b) Mutu mwenye hakuwa Muisraeli na mwenye alitaka kuwa muabudu wa Yehova alipaswa kufanya nini?

11 Hata kama Yehova alikuwa amechagua taifa moja tu hapa duniani, alikubali watu wa mataifa mengine waishi katikati ya watu wake. Wakati Yehova aliwakomboa watu wake kutoka Misri, aliruhusu “jamii kubwa iliyochangamana” ya watu wenye hawakuwa Waisraeli, kama vile Wamisri, waende pamoja na watu wake. (Kut. 12:38) Wakati wa pigo la saba, watu fulani “kati ya watumishi wa Farao” waliogopa neno la Yehova na bila shaka, wakajiunga na jamii kubwa iliyochangamana ya watu wenye walitoka Misri pamoja na Waisraeli.—Kut. 9:20.

12 Mbele tu Waisraeli wavuke muto Yordani na kuingia katika inchi ya Kanaani, Musa aliwaambia kwamba walipaswa ‘kumupenda mukaaji mugeni’ aliyekuwa katikati yao. (Kum. 10:17-19) Watu wenye Mungu alichagua walipaswa kukubali katikati yao wakaaji wageni wenye walikuwa tayari  kushika sheria za musingi zenye zilitolewa kupitia Musa. (Law. 24:22) Wakaaji wageni fulani walifikia kuwa waabudu wa Yehova; walijisikia kama Ruthu, Mumoabu, ambaye alimuambia Naomi hivi: “Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako Mungu wangu.” (Rut. 1:16) Wakaaji hao wageni ndio walikubali dini ya Kiyahudi, na wanaume wao walikubali kutahiriwa. (Kut. 12:48, 49) Yehova aliwakaribisha na kuwaona kama watu wake wenye alichagua.—Hes. 15:14, 15.

Waisraeli waliwapenda wakaaji wageni(Ona fungu la 11 mupaka 13)

13 Wakati hekalu la Sulemani lilitolewa kwa Yehova, mipango ilichukuliwa kwa ajili ya waabudu wenye hawakuwa Waisraeli; tunajua jambo hilo kupitia sala hii ya Sulemani: ‘Kwa mugeni ambaye si sehemu ya watu wako Israeli na ambaye anatoka katika inchi ya mbali kwa sababu ya jina lako kubwa na mukono wako wenye nguvu na mukono wako ulionyooshwa, nao kwa kweli wakuje na kusali kuelekea nyumba hii, basi na usikilize ukiwa mbinguni, katika makao yako yaliyofanywa imara, nawe ufanye kulingana na yote ambayo mugeni huyo anakuomba; kusudi watu wote wa dunia wapate kulijua jina lako nao wakuogope kama vile watu wako Israeli wanavyokuogopa, na ili wajue kwamba jina lako limeitwa juu ya nyumba hii ambayo nimeijenga.’ (2 Nya. 6:32, 33) Hata wakati Yesu alikuwa hapa duniani, mutu yeyote mwenye hakuwa Muisraeli na mwenye alitaka kuwa muabudu wa Yehova, alipaswa kujiunga na watu wenye Mungu alifanya nao agano.—Yoh. 12:20; Mdo. 8:27.

TAIFA LA MASHAHIDI

14-16. (a) Ni katika njia gani Waisraeli walipaswa kuwa taifa la mashahidi wa Yehova? (b) Watu wa Yehova katika siku zetu wanapaswa kufanya nini?

14 Waisraeli waliabudu Yehova, Mungu wao, lakini mataifa mengine yaliabudu miungu yao. Wakati wa nabii Isaya, Yehova alilinganisha hali hiyo na mambo yenye inafanyika kwenye tribinali. Alijaribu miungu ya mataifa kwa kuiomba itokeze mashahidi wenye watashuhudia ikiwa ni miungu ya kweli. Alisema hivi: ‘Mataifa yote na yakusanywe mahali pamoja, na vikundi vya mataifa vikusanywe pamoja. Ni nani kati [ya miungu] yao anayeweza kutangaza haya? Ao, je, wanaweza kutufanya tusikie mambo ya kwanza? Na watoe mashahidi wao, ili watangazwe kuwa waadilifu, ao wasikie na kusema, Ni kweli!’—Isa. 43:9.

15 Miungu ya mataifa haikuwa na uwezo wa kutoa ushuhuda kwamba ni ya kweli. Ilikuwa tu masanamu; haingeweza kusema na ilihitaji kubebwa. (Isa. 46:5-7) Lakini, Yehova aliwaambia Waisraeli hivi: ‘Ninyi ni mashahidi wangu, mutumishi wangu ambaye nimemuchagua, ili mujue na kuwa na imani katika mimi, na ili muelewe kwamba mimi ni Yeye yuleyule. Kabla yangu hakuna Mungu yeyote aliyefanyizwa, na baada yangu hapakuendelea kuwa yeyote. Mimi—mimi ni Yehova, na zaidi ya mimi hakuna mwokozi. Basi ninyi ni mashahidi wangu, nami ni Mungu.’—Isa. 43:10-12.

16 Kama vile mashahidi kwenye tribinali wanafanya, watu wa Yehova walipaswa kutangaza kwamba Yehova ndiye Mungu wa pekee wa kweli. Aliwaita “watu ambao nimejifanyia, ili wasimulie [ao watangaze] sifa zangu.” (Isa. 43:21) Walikuwa watu wenye waliitwa kwa jina la Yehova. Kisha Yehova kuwakomboa kutoka katika utumwa wa Misri, walipaswa kutetea utawala wake mbele ya watu wa mataifa mengine duniani. Walipaswa kuishi kulingana na maneno haya yenye nabii Mika alisema juu ya watu wa Mungu katika siku zetu: ‘Vikundi vyote vya watu vitatembea kila kimoja katika jina la mungu wake; bali sisi tutatembea katika jina la Yehova Mungu wetu mupaka wakati usio na kipimo, naam, milele.’—Mika. 4:5.

WANAMUASI YEHOVA

17. Kulingana na Yehova, namna gani taifa la Israeli lilibadilika na kuwa ‘muzabibu unaoharibika’?

17 Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, Waisraeli hawakubaki waaminifu kwa Yehova Mungu wao. Walishawishiwa na mataifa yenye ilikuwa inaabudu miungu ambayo ilifanywa kwa majiwe ao miti. Katika miaka ya 700 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, nabii Hosea aliandika hivi: ‘Israeli ni muzabibu unaoharibika . . . amezidisha mazabahu zake . . . moyo wao umekuwa na unafiki; sasa watapatikana na hatia.’ (Hos. 10:1, 2) Miaka 150 hivi kisha hapo, nabii Yeremia aliandika juu ya waabudu hao wenye hawakubakia waaminifu kwa Mungu. Aliandika hivi: ‘Lakini mimi nilikuwa nimekupanda kama muzabibu bora mwekundu, wote ukiwa mbegu ya kweli. Basi ni jinsi gani umebadilika kunielekea ukawa machipukizi yaliyoharibika ya muzabibu wa kigeni? . . . Iko wapi miungu yako ambayo umejifanyia? Na isimame ikiwa inaweza kukuokoa wakati wa musiba wako . . . watu wangu mwenyewe wamenisahau mimi.’—Yer. 2:21, 28, 32.

18, 19. (a) Namna gani Yehova alitabiri kwamba atatokeza taifa mupya kwa ajili ya jina lake? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye inafuata?

18 Waisraeli wangezaa matunda mazuri kwa kuendelea kumutolea Yehova ibada safi na kuendelea kuwa mashahidi wake waaminifu. Lakini, kuliko kufanya hivyo, waliendelea kuabudu sanamu, na kwa hiyo, wakazaa matunda mabaya. Ndiyo sababu Yesu aliwaambia viongozi Wayahudi wanafiki wa wakati wake hivi: “Ufalme wa Mungu utachukuliwa kutoka kwenu na kupewa taifa lenye kuzaa matunda yake.” (Mt. 21:43) Ni wale tu wenye walikuwa katika “agano jipya,” lenye Yehova alitabiri kupitia nabii wake Yeremia, ndio wangekuwa sehemu ya taifa hilo mupya, ni kusema, Israeli wa kiroho. Kuhusu Waisraeli wa kiroho ambao wangekuwa katika agano hilo jipya, Yehova alitabiri hivi: “Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”—Yer. 31:31-33.

19 Kisha Waisraeli wa kimwili kukosa uaminifu kwa Mungu, Yehova alichagua Israeli wa kiroho, kama vile tumekwisha kuona. Jambo hilo lilifanyika wakati wa mitume. Lakini, ni nani walio watu wa Yehova duniani leo? Namna gani watu wenye mioyo mizuri wanaweza kutambua waabudu wa kweli? Tutajibu maulizo hayo katika habari yenye inafuata.