Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Sasa Ninyi Ni Watu wa Mungu”

“Sasa Ninyi Ni Watu wa Mungu”

‘Wakati mumoja ninyi mulikuwa si watu, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu.’1 PET. 2:10.

1, 2. Kulikuwa badiliko gani siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33, na ni nani walikuwa taifa mupya la Yehova? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

SIKU ya Pentekoste ya mwaka wa 33 ilikuwa siku ya maana sana katika historia ya watu wa Yehova duniani. Kulikuwa badiliko kubwa sana. Siku hiyo, kupitia roho yake takatifu, Yehova alitokeza taifa mupya, ni kusema, Israeli wa kiroho, ao “Israeli wa Mungu.” (Gal. 6:16) Tofauti na mambo yenye ilifanyika kuanzia wakati wa Abrahamu, watumishi wanaume wa Mungu hawakuwa na lazima ya kutahiriwa ili wajulikane kuwa watu wake. Ndiyo sababu, mutume Paulo aliandika hivi kuhusu kila Mukristo wa taifa hilo mupya: “Kutahiriwa kwake ni kule kwa moyo kupitia roho.”—Rom. 2:29.

2 Mitume na wafuasi wengine zaidi ya 100 wenye walikusanyika katika chumba cha juu huko Yerusalemu ndio walikuwa wa kwanza katika taifa hilo mupya la Mungu. (Mdo. 1:12-15) Watu hao walipokea roho takatifu, na hiyo iliwawezesha kuwa wana wa Mungu waliozaliwa kwa roho. (Rom. 8:15, 16; 2 Kor. 1:21) Hilo lilionyesha kwamba agano jipya limeanza kufanya kazi; Kristo ndiye mupatanishi wa agano hilo, na alifanya likubaliwe kupitia damu yake. (Lu. 22:20; soma Waebrania 9:15.) Kwa hiyo, wafuasi hao wakakuwa taifa mupya la Yehova, ni kusema, watu wake. Roho takatifu iliwawezesha kuhubiri katika luga mbalimbali za Wayahudi na watu wenye walikubali dini ya Kiyahudi ambao walitoka katika maeneo mbalimbali ya Utawala wote wa Roma na kuja  Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Majuma, ao Pentekoste. Watu hao walisikiliza na kuelewa katika luga zao ‘mambo makubwa ya Mungu’ yenye Wakristo wenye walizaliwa kwa roho walikuwa wanahubiri.—Mdo. 2:1-11.

TAIFA MUPYA LA MUNGU

3-5. (a) Siku ya Pentekoste, mutume Petro aliwaambia Wayahudi nini? (b) Taifa mupya la Yehova lilifikia namna gani kuongezeka katika miaka ya kwanza-kwanza?

3 Kupitia mutume Petro, Yehova alifungulia Wayahudi na watu wengine wenye walikubali dini ya Kiyahudi njia ya kuwa katika taifa mupya lenye lilitoka tu kuzaliwa, ni kusema, kutaniko la Kikristo. Siku ya Pentekoste, mutume Petro hakuogopa kuwaambia Wayahudi kwamba walipaswa kumukubali Yesu, ambaye ‘alifungwa kwenye muti.’ Walipaswa kufanya hivyo kwa sababu ‘Mungu alimufanya [Yesu kuwa] Bwana na pia Kristo.’ Wakati watu walimuuliza mutume Petro mambo yenye walipaswa kufanya, aliwaambia hivi: ‘Mutubu, na muache kila mumoja wenu abatizwe katika jina la Yesu Kristo kwa musamaha wa zambi zenu, nanyi mutapokea zawadi ya bure ya roho takatifu.’ (Mdo. 2:22, 23, 36-38) Siku hiyo, watu 3000 hivi waliongezwa kwenye taifa hilo mupya la Israeli wa kiroho. (Mdo. 2:41) Kisha hapo, mitume waliendelea kuhubiri kwa bidii, na kazi hiyo ilizaa matunda mengi. (Mdo. 6:7) Taifa hilo mupya liliendelea kuongezeka.

4 Kisha, habari njema iliwafikia pia Wasamaria, na matokeo yalikuwa mazuri. Filipo, mueneza-injili, alibatiza Wasamaria wengi, lakini wakati huo hawakupokea roho takatifu. Baraza linaloongoza lilituma mutume Petro na mutume Yohana huko Samaria; ‘wakaweka mikono yao juu yao [Wasamaria walioamini], nao wakaanza kupokea roho takatifu.’ (Mdo. 8:5, 6, 14-17) Kwa hiyo, Wasamaria hao wakaingizwa pia katika taifa hilo la watiwa-mafuta, ni kusema, Israeli wa kiroho.

Mutume Petro alimuhubiria Kornelio na watu wa nyumba yake

(Ona fungu la 5))

5 Katika mwaka wa 36, Mungu alitumia pia mutume Petro ili kuingiza watu wengine katika taifa hilo mupya. Mutume Petro alimuhubiria Kornelio (mukubwa wa kikundi fulani cha maaskari wa Roma) pamoja na watu wa familia yake na marafiki wake. (Mdo. 10:22, 24, 34, 35) Biblia inasema hivi: “Petro alipokuwa bado akisema . . . , roho takatifu ikawaangukia [watu wasio-Wayahudi] wote waliokuwa wakisikia lile neno. Na waaminifu waliokuwa wamekuja pamoja na Petro ambao walikuwa kati ya wale waliotahiriwa wakashangaa, kwa sababu zawadi ya bure ya roho takatifu ilikuwa ikimiminwa pia juu ya watu wa mataifa.” (Mdo. 10:44, 45) Kwa hiyo, hata watu wa mataifa wasiotahiriwa wenye waliamini, walipewa pendeleo la kuingia katika taifa mupya la kiroho.

“WATU KWA AJILI YA JINA LAKE”

6, 7. Ni katika njia gani Wakristo wa taifa mupya walipaswa kutenda kama “watu kwa ajili ya jina [la Yehova],” na walifanya hivyo kwa kadiri gani?

6 Katika mwaka wa 49, baraza linaloongoza lilifanya mukutano. Kwenye mukutano huo, mwanafunzi Yakobo alisema hivi: “Simioni [Petro] ameeleza kikamili jinsi Mungu kwa mara ya kwanza alivyoelekeza uangalifu wake  kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.” (Mdo. 15:14) Watu hao wenye waliitwa kwa jina la Yehova walikuwa ni Wayahudi na watu wa mataifa wenye waliamini. (Rom. 11:25, 26a) Kisha, mutume Petro aliandika hivi: ‘Wakati mumoja ninyi mulikuwa si watu, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu.’ Katika barua hiyo mutume Petro alikazia daraka lao. Aliwaambia hivi: ‘Ninyi ni jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa kuwa mali ya pekee, ili mutangaze kotekote sifa bora zake Yeye aliyewaita ninyi kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.’ (1 Pet. 2:9, 10) Daraka lao lilikuwa ni kujulisha sifa za Yule mwenye aliwachagua na kutangaza kotekote jina lake. Kwa hiyo, walipaswa kuwa mashahidi wenye bidii wa Yehova, Mutawala Mukubwa.

7 Kama vile Yehova alitumia Waisraeli wa kimwili, leo, Waisraeli wa kiroho ndio watu wenye Yehova anatumia, na anawaita “watu ambao nimejifanyia, ili wasimulie [ao watangaze] sifa zangu.” (Isa. 43:21) Ili kuonyesha kwamba miungu yote yenye watu walikuwa wanaabudu wakati huo ilikuwa ya uongo, Wakristo hao wa kwanza-kwanza walitangaza kwa bidii kwamba Yehova tu ndiye Mungu wa kweli. (1 Tes. 1:9) Walitoa ushahidi juu ya Yehova na juu ya Yesu ‘katika Yerusalemu na pia katika Yudea yote na Samaria na mupaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.’—Mdo. 1:8; Kol. 1:23.

8. Wakati wa mitume, ni onyo gani mutume Paulo aliwatolea watu wa Mungu?

8 Mukristo mumoja mwenye bidii kati ya “watu kwa ajili ya jina [la Yehova]” alikuwa mutume Paulo. Wakati alikuwa mbele ya wanafilozofia wapagani, alitetea bila kuogopa utawala mukubwa wa Yehova, ambaye ni “Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo, akiwa, kama Huyu alivyo, Bwana wa mbingu na dunia.” (Mdo. 17:18, 23-25) Mwishoni mwa safari yake ya tatu ya umisionere, mutume Paulo aliwaonya watu hao wenye waliitwa kwa jina la Mungu. Aliwaambia hivi: “Ninajua kwamba baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wenye kukandamiza wataingia katikati yenu nao hawatalitendea kundi kwa wororo, na kutoka katikati yenu ninyi wenyewe watu watasimama na kusema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.” (Mdo. 20:29, 30) Uasi-imani huo wenye ulitabiriwa ulianza kuonekana wazi katika kipindi cha mwisho cha wakati wa mitume na kuendelea.—1 Yoh. 2:18, 19.

9. Kisha mitume kufa, ni jambo gani liliwapata “watu kwa ajili ya jina [la Yehova]”?

9 Kisha mitume kufa, uasi-imani huo uliongezeka sana na ukatokeza makanisa mengi yanayojiita kuwa ya Kikristo. Kuliko kuonyesha kwamba walikuwa “watu kwa ajili ya jina [la Yehova],” waasi-imani hao waliondoa hata jina la Mungu katika tafsiri zao za Biblia. Walianza kufuata desturi za kipagani na walimushushia Mungu heshima kupitia mafundisho yao ya uongo, “vita vitakatifu,” na mwenendo wao muchafu. Kwa hiyo, kwa muda wa miaka mingi, Yehova alikuwa na waabudu waaminifu wadogo sana duniani, lakini walikuwa hawajapangwa vizuri ili wakuwe “watu kwa ajili ya jina lake.”

YEHOVA ANAKUWA TENA NA WAABUDU WA KWELI WENYE KUPANGWA VIZURI

10, 11. (a) Katika mufano wa ngano na magugu, Yesu alitabiri nini? (b) Namna gani mufano huo ulitimia kisha mwaka wa 1914, na hilo lilikuwa na matokeo gani?

10 Katika mufano wa ngano na magugu, Yesu alitabiri giza la kiroho lenye lingetokea kwa sababu ya uasi-imani. Alisema kwamba “watu wakiwa wamelala usingizi,” Ibilisi angepanda magugu katikati ya ngano yenye Mwana wa binadamu alipanda. Ngano na magugu vingekomaa pamoja mupaka ‘umalizio wa mufumo wa mambo.’ Yesu alieleza kwamba “mbegu nzuri” ni “wana wa Ufalme” na kwamba “magugu” ni “wana wa yule  mwovu.” Wakati wa mwisho, Mwana wa binadamu angetuma “wavunaji” wake, ni kusema malaika, ili watenganishe ngano na magugu ya mufano. Kisha, wana wa Ufalme wangekusanywa. (Mt. 13:24-30, 36-43) Jambo hilo lilitimia namna gani, na namna gani hilo lilisaidia ili Yehova akuwe tena na waabudu wa kweli wenye kupangwa hapa duniani?

11 ‘Umalizio wa mufumo wa mambo’ ulianza katika mwaka wa 1914. Wakati wa vita yenye ilitokea mwaka huo, Wakristo watiwa-mafuta, ni kusema, “wana wa Ufalme” karibu 5000 walikuwa wafungwa kwa njia ya kiroho katika Babiloni Mukubwa. Katika mwaka wa 1919, Yehova aliwakomboa. Kwa kufanya hivyo, alionyesha wazi tofauti kati yao na “magugu,” ao watu wanaojidai kuwa Wakristo. Alikusanya “wana wa Ufalme” na kuwapanga; kufanya hivyo kulitimiza unabii wa Isaya wenye unasema hivi: ‘Je, inchi itazaliwa kwa uchungu katika siku moja? Ao, je, taifa litazaliwa wakati uleule mumoja? Kwa maana Sayuni ameshikwa na uchungu wa kuzaa, naye vilevile amezaa wanawe.’ (Isa. 66:8) Sayuni, ni kusema, tengenezo la Yehova la viumbe wa kiroho, lilitokeza wana waliotiwa mafuta kwa roho na likawafanya kuwa taifa.

12. Namna gani leo Wakristo watiwa-mafuta wanaonyesha kwamba wao ni “watu kwa ajili ya jina [la Yehova]”?

12 Kama vile Wakristo wa kwanza-kwanza, “wana wa Ufalme” waliotiwa mafuta walipaswa kuwa mashahidi wa Yehova. (Soma Isaya 43:1, 10, 11.) Kwa hiyo, walipaswa kuwa tofauti kupitia mwenendo wao na kazi yao ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme . . . ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote.” (Mt. 24:14; Flp. 2:15) Kwa kufanya hivyo, walisaidia mamilioni ya watu kuwa marafiki wa Yehova.—Soma Danieli 12:3.

TUNATAKA ‘KUENDA PAMOJA NANYI’

13, 14. Watu ambao si Waisraeli wa kiroho wanapaswa kufanya nini ili kumuabudu Yehova kwa njia inayofaa, na namna gani Biblia ilitabiri jambo hilo?

13 Katika habari yenye ilitangulia tuliona kwamba katika Israeli ya zamani, wakaaji wageni walipewa nafasi ya kumuabudu Yehova kwa njia inayofaa. Lakini, oui  wakaaji hao wageni walipaswa kujiunga na watu wenye Yehova alifanya nao agano. (1 Fal. 8:41-43) Leo pia, Watu ambao si Waisraeli wa kiroho wanapaswa kumuabu Yehova pamoja na “wana wa Ufalme” ao Mashahidi wa Yehova watiwa-mafuta.

14 Katika siku hizi za mwisho, watu wengi sana wanajiunga na watu wa Yehova ili kumuabudu; jambo hilo lilitabiriwa na manabii wawili wa zamani. Kwa mufano, nabii Isaya alitabiri hivi: ‘Vikundi vingi vya watu hakika vitaenda na kusema: Njooni, twendeni juu kwenye mulima wa Yehova, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Naye atatufundisha njia zake, nasi tutatembea katika mapito yake. Kwa maana sheria itatoka katika Sayuni, na neno la Yehova katika Yerusalemu.’ (Isa. 2:2, 3) Vilevile, nabii Zekaria alitabiri kwamba ‘vikundi vingi vya watu na mataifa yenye nguvu watakuja kumutafuta Yehova wa majeshi katika Yerusalemu na kuutuliza uso wa Yehova [ao kutafuta kibali cha Yehova].’ Alionyesha kwamba ni ‘watu kumi kutoka katika luga zote za mataifa’ wenye, kwa njia ya mufano, wangekamata nguo ya Israeli wa kiroho, na kusema hivi: ‘[Tunataka] kuenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu iko pamoja nanyi.’—Zek. 8:20-23.

15. “Kondo wengine” ‘wanaenda pamoja’ na Waisraeli wa kiroho katika kazi gani?

15 “Kondoo wengine” ‘wanaenda pamoja’ na Waisraeli wa kiroho katika kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme. (Mk. 13:10) Wanakuwa sehemu ya watu wa Mungu, ni kusema, “kundi moja” pamoja na Wakristo watiwa-mafuta, na wanaongozwa na Yesu Kristo, ‘muchungaji mwema.’—Soma Yohana 10:14-16.

TAFUTA ULINZI KATIKATI YA WATU WA MUNGU

16. Yehova ataanzisha namna gani sehemu ya mwisho ya ‘ziki kubwa’?

16 Kisha Babiloni Mukubwa kuharibiwa, watu wa Yehova watashambuliwa. Wakati huo tutakuwa na lazima ya ulinzi wenye Yehova atatolea watumishi wake. Kwa sababu shambulio hilo litaanzisha sehemu ya mwisho ya ‘ziki kubwa,’ ni Yehova mwenyewe ndiye atatokeza shambulio hilo na ni yeye ndiye atachagua wakati kwa ajili ya shambulio hilo. (Mt. 24:21; Eze. 38:2-4) Wakati huo, Gogu atashambulia “watu waliokusanywa pamoja kutoka katika mataifa,” ni kusema, watu wa Yehova. (Eze. 38:10-12) Shambulio hilo litaonyesha kwamba Yehova anataka kuleta hukumu juu ya Gogu pamoja na wale wenye wanamuunga mukono. Yehova atatukuza utawala wake mukubwa na atalitakasa jina lake, kwa sababu anasema hivi: ‘Nami hakika . . . nitajijulisha mwenyewe mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’—Eze. 38:18-23.

Wakati wa ‘ziki kubwa,’ tutakuwa na lazima ya kushikamana na kutaniko letu(Ona fungu la 16 mupaka 18)

17, 18. (a) Tutapata maagizo gani wakati Gogu atashambulia watu wa Yehova? (b) Tunapaswa kufanya nini ikiwa tunataka Yehova atulinde?

17 Wakati Gogu ataanza shambulio hilo, Yehova ataambia watu wake hivi: ‘Muende, watu wangu, ingia katika vyumba vyako vya ndani, na ufunge milango nyuma yako. Ujifiche kwa kitambo [ao muda] kidogo mupaka hukumu itakapopita.’ (Isa. 26:20) Wakati huo mugumu, Yehova atatupatia maagizo yenye itatusaidia kuokoa uzima wetu, na inawezekana ‘vyumba vya ndani’ vitakuwa ni makutaniko yetu.

18 Kwa hiyo, ikiwa tunataka Yehova atulinde wakati wa ziki kubwa, tunapaswa kukubali kwamba Yehova iko na watu wake duniani, na kwamba watu hao wanapangwa katika makutaniko. Tunapaswa kuendelea kujiunga na watu wa Yehova na kushikamana sana na kutaniko letu. Kwa moyo wote, tutangaze kama mutunga-zaburi hivi: “Wokovu ni wa Yehova. Baraka yako iko juu ya watu wako.”—Zab. 3:8.