Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Namna gani wazee na watumishi wa huduma wanawekwa katika kila kutaniko?

Wakati wa mitume, mutume Paulo aliwaambia wazee wa kutaniko la Efeso hivi: ‘Mujiangalie ninyi wenyewe na kundi lote, ambalo roho takatifu imewaweka ninyi rasmi kuwa waangalizi kati yake, kulichunga kutaniko la Mungu, ambalo alilinunua kwa damu ya Mwana wake mwenyewe.’ (Mdo. 20:28) Roho takatifu inatimiza daraka gani leo katika kuweka wazee na watumishi wa huduma katika makutaniko?

Kwanza, roho takatifu iliongoza waandikaji wa Biblia ili waandike sifa zenye zinaombwa ili kustahili kuwa muzee ao mutumishi wa huduma. Andiko la 1 Timotheo 3:1-7 linataja mambo 16 hivi yenye ndugu anapaswa kutimiza ili astahili kuwa muzee wa kutaniko. Mambo mengine ambayo ndugu anapaswa kutimiza yanapatikana katika maandiko kama vile Tito 1:5-9 na Yakobo 3:17, 18. Mambo ambayo ndugu anapaswa kutimiza ili astahili kuwa mutumishi wa huduma inatajwa katika andiko la 1 Timotheo 3:8-10, 12, 13. Pili, wale wenye kupendekeza na kuweka ndugu kuwa wazee ao watumishi wa huduma wanasali ili roho ya Yehova iwaongoze wakati wanachunguza ikiwa ndugu anatimiza kwa kiasi fulani mambo ambayo Biblia inaomba. Tatu, ndugu ambaye anapendekezwa anapaswa kuonyesha tunda la roho takatifu ya Mungu katika maisha yake yote. (Gal. 5:22, 23) Kwa hiyo, roho takatifu ya Mungu ni ya lazima sana katika hatua zote zenye zinafanywa ili kuweka wazee na watumishi wa huduma.

Kwa kweli, ni nani anaweka wazee na watumishi wa huduma? Zamani, mapendekezo yote yalitumwa kwenye biro ya tawi. Huko, ndugu ambao waliwekwa na Baraza Linaloongoza walikuwa wanachunguza mapendekezo hayo na kuweka wazee na watumishi wa huduma. Kisha, biro ya tawi iliandikia wazee wa kutaniko ili kuwajulisha ndugu ambao wamekubaliwa kuwa wazee ao watumishi wa huduma. Kwa upande wao, wazee walijulisha ndugu ambao walikubaliwa, na waliwauliza ikiwa wako tayari kutumikia daraka hilo. Mwishowe, wazee walitangazia kutaniko.

Lakini, namna gani wazee na watumishi wa huduma walikuwa wanawekwa wakati wa mitume? Wakati fulani, mitume waliweka watu fulani ili kushugulikia mambo fulani. Kwa mufano, waliweka ndugu saba ili washugulikie ugawaji wa kila siku wa chakula kwa ajili ya wajane. (Mdo. 6:1-6) Hata hivyo, ndugu hao walikuwa wazee mbele wapewe daraka hilo.

Hata kama Biblia haitoe maelezo mengi kuhusu namna wazee na watumishi wa huduma walikuwa wanawekwa wakati wa mitume, kuna maandiko fulani yenye inaonyesha namna mambo ilikuwa inafanyika. Kwa mufano, Biblia inasema kwamba wakati Paulo na Barnaba  walikuwa wanarudia kutoka katika safari yao ya kwanza ya umisionere, ‘waliwaweka rasmi wanaume wazee kwa ajili yao katika kila kutaniko, wakatoa sala pamoja na kufunga, na kuwakabizi kwa Yehova ambaye walikuwa wamemwamini.’ (Mdo. 14:23) Kisha miaka fulani, mutume Paulo alimuandikia Tito aliyesafiri pamoja naye hivi: “Kwa sababu hii nilikuacha wewe Krete, ili uyarekebishe mambo yaliyokuwa na kasoro na uweke rasmi wanaume wazee katika jiji baada ya jiji, kama nilivyokupa maagizo.” (Tito 1:5) Inaonekana kwamba Timotheo, ambaye alisafiri sana na mutume Paulo, alipewa pia mamlaka ya kufanya hivyo. (1 Tim. 5:22) Ni wazi kwamba wakati huo, waangalizi wenye kusafiri ndio walikuwa na daraka la kuweka wazee na watumishi wa huduma, wala si mitume na wanaume wazee katika Yerusalemu.

Kulingana na muongozo huo wenye kupatikana katika Biblia, Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova limerekebisha namna wazee na watumishi wa huduma wanapaswa kuwekwa. Kuanzia tarehe 1 Mwezi wa 9, 2014, wazee na watumishi wa huduma wanawekwa katika makutaniko kwa njia hii: Kila mwangalizi wa muzunguko anachunguza kwa uangalifu mapendekezo yote ambayo wazee wanafanya katika muzunguko wake. Wakati anatembelea makutaniko, anajikaza kujua vizuri ndugu ambao wamependekezwa, kwa mufano, anahubiri pamoja nao ikiwezekana. Kisha kuchunguza mapendekezo hayo pamoja na baraza la wazee, mwangalizi wa muzunguko anaweka wazee na watumishi wa huduma katika makutaniko ya muzunguko wake. Kwa kufanya hivyo, tunafuata kabisa mufano wa wakati wa mitume.

Wazee wanachunguza pamoja na mwangalizi wa muzunguko ili kuona ikiwa ndugu fulani anatimiza mambo yenye Maandiko inaomba(Malawi)

Ni nani wanashugulikia hatua mbalimbali zenye zinafanywa ili kuweka wazee na watumishi wa huduma? Kama kawaida, ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ iko na daraka kubwa la kulisha watumishi wa nyumbani. (Mt. 24:45-47) Anachunguza Maandiko kwa kufuata muongozo wa roho takatifu ili kuonyesha namna ya kutumia kanuni za Biblia zenye zinaonyesha namna kutaniko la duniani pote limepangwa. Mutumwa mwaminifu anaweka pia waangalizi wa muzunguko na ndugu wa Halmashauri ya Tawi. Kisha, kila biro ya tawi inatoa musaada wenye kufaa ili kufuata muongozo ambao umepewa. Kila baraza la wazee lina daraka la kuchunguza Maandiko kwa uangalifu ili kuona ikiwa ndugu wenye wanapendekeza wanatimiza mambo ambayo yanaombwa ili wakuwe wazee ao watumishi wa huduma katika kutaniko la Mungu. Mbele ya kuweka wazee na watumishi wa huduma, kila mwangalizi wa muzunguko iko na daraka kubwa la kusali na kuchunguza kwa uangalifu mapendekezo yenye wazee wanafanya.

Kujua namna wazee na watumishi wa huduma wanawekwa katika makutaniko kunatusaidia tuelewe vizuri zaidi kazi ya roho takatifu katika hatua zote zenye zinafanywa. Kwa hiyo, tutumainie sana na kuheshimu wale wote ambao wamewekwa katika kutaniko la Kikristo.—Ebr. 13:7, 17.

 Mashahidi wawili wenye wanazungumuziwa katika Ufunuo sura 11 ni nani?

Andiko la Ufunuo 11:3 linazungumuzia mashahidi wawili wenye wangetoa ushahidi kwa muda wa siku 1260. Kisha, mistari yenye inafuata inasema kwamba munyama mwitu ‘angewashinda na kuwaua.’ Lakini kisha “siku tatu na nusu,” mashahidi hao wawili wangefufuliwa, na jambo hilo lingeogopesha wale wenye walikuwa wanawatazama.—Ufu. 11:7, 11.

Mashahidi hao wawili ni nani? Mafasirio zaidi yenye sura ya 11 ya kitabu cha Ufunuo inatoa inatusaidia kuwajua. Kwanza, sura hiyo inasema kwamba “wanafananishwa na ile mizeituni miwili na vile vinara viwili vya taa.” (Ufu. 11:4) Maneno hayo yanatukumbusha kile kinara na ile mizeituni miwili ya unabii wa Zekaria. Miti hiyo ya mizeituni ilikuwa inafananisha “wale watiwa-mafuta wawili,” ni kusema, Zerubabeli na Yoshua Kuhani Mukubwa, wenye walikuwa ‘wanasimama kando ya Bwana wa dunia yote.’ (Zek. 4:1-3, 14) Pili, sura hiyo inasema kwamba mashahidi hao wawili wanafanya miujiza kama ile Musa na Eliya walifanya.—Linganisha andiko la Ufunuo 11:5, 6 na Hesabu 16:1-7, 28-35 na 1 Wafalme 17:1; 18:41-45.

Maandiko hayo inapatana namna gani? Kila andiko linazungumuzia watiwa-mafuta wa Mungu wenye waliongoza watu wa Mungu wakati wa majaribu makali. Kwa hiyo, unabii wa Ufunuo sura 11 ulitimia wakati Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mbinguni katika mwaka wa 1914, wakati ndugu watiwa-mafuta wenye walikuwa wanaongoza watu wa Mungu walihubiri wakiwa “wamevikwa nguo za magunia” kwa muda wa miaka tatu na nusu.

Wakati watiwa-mafuta hao wenye kuvaa nguo za magunia walifikia mwisho wa kazi yao ya kuhubiri, waliuawa kwa njia ya mufano wakati walitupwa katika gereza. Walitupwa humo kwa muda mufupi, ni kusema, muda wa siku tatu na nusu za mufano. Maadui wa watu wa Mungu walifikiri kwamba kazi yao imekufa. Kwa hiyo, walifurahi sana.—Ufu. 11:8-10.

Hata hivyo, kulingana na maneno ya unabii huo, mashahidi hao wawili walifufuliwa kisha siku tatu na nusu. Wakristo hao watiwa-mafuta waliachiliwa huru; lakini pia, kupitia Yesu Kristo, Bwana wao, Mungu aliwapatia wale wenye walibakia waaminifu pendeleo la pekee. Katika mwaka wa 1919, wao pamoja na wengine Wakristo watiwa-mafuta waliwekwa kuwa ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ ili kushugulikia mahitaji ya kiroho ya watu wa Mungu katika siku hizi za mwisho.—Mt. 24:45-47; Ufu. 11:11, 12.

Jambo la kufurahisha ni kwamba, andiko la Ufunuo 11:1, 2 linapatanisha matukio hayo na wakati hekalu la kiroho lilipaswa kupimwa ao kuchunguzwa. Kitabu cha Malaki sura ya 3 kinazungumuzia uchunguzi kama huo wa hekalu la kiroho, na pia wakati wa kusafishwa kwa hekalu hilo. (Mal. 3:1-4) Kazi ya uchunguzi na ya kusafisha hekalu hilo ilichukua muda gani? Ilifanyika kuanzia mwaka wa 1914 mupaka miezi ya kwanza-kwanza ya mwaka wa 1919. Muda huo ulikamata siku 1260 (miezi 42) ao siku tatu na nusu za mufano zenye zinatajwa katika Ufunuo sura ya 11.

Tunafurahi sana kuona namna Yehova alichukua mupango huo wa kiroho ili kusafisha watu wake kwa ajili ya kazi njema! (Tito. 2:14) Zaidi ya hilo, tunapendezwa na mufano wenye Wakristo watiwa-mafuta waaminifu walituachia; waliongoza watu wa Mungu wakati huo wa majaribu makali, na kwa hiyo wakakuwa wale mashahidi wawili wa mufano. *

^ fu. 18 Ili kupata habari zaidi, ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2013, ukurasa wa 22, fungu la 12..