Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA | UNAWEZA KUWA RAFIKI YA MUNGU

Unajua Jina la Mungu na Unalitumia?

Unajua Jina la Mungu na Unalitumia?

Unaweza kukumbuka rafiki yako fulani mwenye haujue jina lake? Labda hapana. Mwanamuke mumoja wa Bulgaria anayeitwa Irina alisema, “Haiwezekane mutu kufanya urafiki na Mungu ikiwa hajue jina lake.” Jambo la kufurahisha ni hili: kama vile tulisema katika habari iliyotangulia, Mungu anataka ufanye urafiki na yeye. Kwa hiyo, kupitia Biblia, yeye mwenyewe amejitambulisha kwako kwa kusema hivi: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu.”—Isaya 42:8.

Kupitia Biblia, Mungu mwenyewe amejitambulisha kwako kwa kusema hivi: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu.”—Isaya 42:8

Yehova anaona kuwa ni jambo la maana ujue jina lake na kulitumia? Waza juu ya jambo hili: Jina la Mungu, lililoandikwa kwa herufi ine za Kiebrania zinazojulikana kuwa Tetragramu, linaonekana katika maandishi ya kwanza ya Maandiko ya Kiebrania karibu mara 7000. Jina hilo linapatikana mara nyingi katika Biblia kuliko majina mengine yote. Hilo linaonyesha kabisa kuwa Yehova anataka tujue jina lake na kulitumia. *

Mara nyingi watu wawili wanaanza urafiki kwa kuambiana kwanza majina. Wewe unajua jina la Mungu?

Hata hivyo, watu fulani wanaweza kuwaza kama kutumia jina la Mungu ni kukosa heshima kwa sababu yeye ni mutakatifu na mweza-yote. Kwa kweli, inaweza kuwa vibaya kutumia jina la Mungu kwa njia isiyofaa, kama vile hauwezi kutumia jina la rafiki yako wa karibu kwa njia isiyofaa. Hata hivyo, Yehova anataka watu wanaomupenda waheshimu jina lake na walijulishe watu wengine. (Zaburi 69:30, 31; 96:2, 8) Kumbuka, Yesu alifundisha wafuasi wake wasali hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litakaswe.’ Sisi pia tunaweza kulitakasa jina la Mungu kwa kulijulisha watu wengine. Kwa kufanya hivyo tunakuwa marafiki wa Mungu.—Mathayo 6:9.

Biblia inaonyesha kuwa Mungu anapendezwa sana na “wale wanaolifikiria [ao labda “wanaopenda”] jina lake.” (Malaki 3:16) Juu ya watu kama hao, Yehova anaahidi hivi: ‘Nitamulinda kwa sababu amelijua jina langu. Ataniitia, nami nitamujibu. Nitakuwa pamoja naye katika taabu.’ (Zaburi 91:14, 15) Kujua jina la Yehova na kulitumia ni jambo la maana ikiwa tunataka kufanya urafiki naye.

^ fu. 4 Jambo la kuhuzunisha ni hili: tafsiri nyingi za Biblia hazitumie jina la Mungu, hata ikiwa jina hilo linaonekana mara nyingi katika Maandiko ya Kiebrania, yenye watu wengi wanaita Agano la Kale. Lakini, mahali pa jina hilo tafsiri hizo zimetia majina ya cheo ao ya heshima kama vile “Bwana” ao “Mungu.” Ili kupata maelezo mengine juu ya habari hii, soma ukurasa wa 195-197 wa kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.