Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sikiliza na Uelewe Maana

Sikiliza na Uelewe Maana

‘Munisikilize, ninyi nyote, mupate [ao muelewe] maana.’ MK. 7:14.

1, 2. Sababu gani watu wengi hawakuelewa maana ya maneno ya Yesu?

MUTU mumoja anaweza kusikia sauti ya mutu mwenye kuzungumuza naye. Anaweza hata kusikia namna mutu huyo iko anazungumuza. Lakini, namna gani anaweza kufaidika ikiwa haelewe maana ya maneno ya mutu huyo? (1 Kor. 14:9) Vilevile, watu wengi walisikia mambo yenye Yesu alikuwa anasema. Alitumia usemi wenye kila mutu angeweza kuelewa. Hata hivyo, si wote walielewa maana ya maneno yake. Ndiyo sababu Yesu aliwaambia wasikilizaji wake hivi: ‘Munisikilize, ninyi nyote, mupate [ao muelewe] maana.’—Mk. 7:14.

2 Sababu gani watu wengi hawakuelewa maana ya maneno ya Yesu? Wamoja walikuwa na mawazo mabaya na nia mbaya. Yesu aliwaambia watu hao hivi: ‘Kwa ustadi munaweka kando amri ya Mungu kusudi mubaki na mapokeo yenu.’ (Mk. 7:9) Kwa kweli, watu hao hawakutaka hata kidogo kuelewa maana ya maneno ya Yesu. Hawakutaka kubadilisha tabia zao na maoni yao. Masikio yao ilikuwa inasikia, lakini mioyo yao ilikuwa yenye kufungwa kabisa. (Soma Mathayo 13:13-15.) Namna gani tunaweza kuhakikisha kwamba mioyo yetu inafunguliwa ili tuweze kufaidika na mafundisho ya Yesu?

 NAMNA TUNAWEZA KUFAIDIKA NA MAFUNDISHO YA YESU

3. Sababu gani wanafunzi wa Yesu walielewa maneno yake?

3 Tunapaswa kuiga unyenyekevu wa wanafunzi wa Yesu. Aliwaambia hivi: “Yenye furaha ni macho yenu kwa sababu hayo yanaona, na masikio yenu kwa sababu hayo yanasikia.” (Mt. 13:16) Sababu gani wanafunzi hao walielewa mambo yenye wengine hawakuelewa? Kwanza, hawakusita kuuliza maulizo na walitafuta kuelewa kabisa maana ya maneno ya Yesu. (Mt. 13:36; Mk. 7:17) Pili, walipenda kuongeza mambo mapya juu ya yale ambayo tayari walikuwa wameamini. (Soma Mathayo 13:11, 12.) Tatu, walipenda kutumikisha katika maisha yao mambo yenye walisikia na kuelewa, na walipenda pia kuyatumia ili kusaidia wengine.—Mt. 13:51, 52.

4. Tunapaswa kufuata hatua gani tatu ili kuelewa mifano yenye Yesu alitumia?

4 Ikiwa tunataka kuelewa mifano yenye Yesu alitumia, tunapaswa kuiga wanafunzi wake waaminifu. Hatua tatu zinaweza kutusaidia kufanya hivyo. Kwanza, tunapaswa kuchukua wakati wa kujifunza na kufikiri sana juu ya maneno ya Yesu, kutafuta habari katika vichapo vyetu, na kuuliza maulizo yanayofaa. Kufanya hivyo kunatusaidia kupata ujuzi. (Met. 2:4, 5) Pili, tunapaswa kupatanisha mambo yenye tumejifunza na yale tulikuwa tunajua, na tunapaswa kutambua faida yenye tunapata kwa kufanya hivyo. Kufanya hivyo kunatusaidia kupata uelewaji. (Met. 2:2, 3) Tatu, tunapaswa kutumikisha katika maisha yetu mambo yenye tumejifunza. Kufanya hivyo kunaonyesha kwamba tuko na hekima.—Met. 2:6, 7.

5. Toa mufano wenye kuonyesha tofauti kati ya ujuzi, uelewaji, na hekima.

5 Kuna tofauti gani kati ya ujuzi, uelewaji, na hekima? Ili kuelewa, tuchukue mufano huu: Wazia unasimama katikati ya barabara na unaona motokari inakuja kwenye unasimama. Kwanza, unatambua kwamba ni motokari; huo ni ujuzi. Kisha, unaelewa kwamba motokari hiyo itakugonga ikiwa hautoke mahali hapo; huo ni uelewaji! Kwa hiyo unatoka haraka; hiyo ni hekima! Ndiyo sababu Biblia inakazia kwamba tunapaswa ‘kulinda hekima inayotumika.’ Kufanya hivyo kutatusaidia kupata uzima!—Met. 3:21, 22; 1 Tim. 4:16.

6. Wakati wa kuchunguza mifano saba yenye Yesu alitumia, tutajiuliza maulizo gani ine? (Ona pia kisanduku box.)

6 Katika habari hii na ile yenye kufuata, tutachunguza mifano saba yenye Yesu alitumia. Wakati wa kuchunguza mifano hiyo, tutajiuliza maulizo haya: Mufano huu unamaanisha nini? (Hilo linatusaidia kupata ujuzi.) Sababu gani Yesu alitumia mufano huu? (Hilo linatuletea uelewaji.) Namna gani tunaweza kutumia katika maisha yetu mambo yenye tunajifunza katika mufano huu, na namna gani tunaweza kuyatumia ili kusaidia wengine? (Hiyo ni hekima.) Mufano huu unatufundisha nini juu ya Yehova na juu ya Yesu?

MUFANO WA MBEGU YA HARADALI

7. Mufano wa Yesu wa mbegu ya haradali unamaanisha nini?

7 Soma Mathayo 13:31, 32. Mufano wa Yesu wa mbegu ya haradali unamaanisha nini? Mbegu ya haradali inafananisha ujumbe wa Ufalme wenye tunahubiri na pia kutaniko la Kikristo. Kama vile mbegu ya haradali ni “mbegu ndogo zaidi kuliko zote,” kutaniko la Kikristo halikuwa na watu wengi wakati lilianza katika mwaka wa 33. Lakini kisha miaka kidogo, kutaniko liliongezeka mbio sana kwa njia yenye kushangaza. (Kol. 1:23) Ongezeko hilo ni lenye faida kwa sababu Yesu alisema kwamba ‘ndege wa mbinguni wangepata makao katikati ya matawi yake.’ Ndege hao wa mufano wanafananisha watu wenye moyo muzuri ambao wanapata chakula cha kiroho, kivuli, na makao katika kutaniko la Kikristo.—Linganisha na Ezekieli 17:23.

8. Sababu gani Yesu alitumia mufano wa mbegu ya haradali?

8 Sababu gani Yesu alitumia mufano huu? Alitumia mufano wa mbegu ya  haradali ambayo inakomaa kwa njia yenye kushangaza ili kuonyesha kwamba Ufalme wa Mungu uko na uwezo wa kupanuka, kutoa ulinzi, na hakuna kitu kinaweza kuuzuia. Tangu mwaka wa 1914, sehemu yenye kuonekana ya tengenezo la Mungu imeongezeka kwa njia yenye kushangaza sana! (Isa. 60:22) Wale wenye kujiunga na tengenezo hilo wanapata ulinzi wa kiroho. (Met. 2:7; Isa. 32:1, 2) Tena, imeonekana kwamba hakuna kitu kinaweza kuzuia faida za Ufalme ziendelee.—Isa. 54:17.

9. (a) Mufano wa mbegu ya haradali unaweza kutufundisha nini? (b) Mufano huo unatufundisha nini juu ya Yehova na juu ya Yesu?

9 Mufano wa mbegu ya haradali unaweza kutufundisha nini? Pengine tunaishi katika eneo lenye kuwa na Mashahidi wachache ao lenye halina matokeo mengi katika kazi ya kuhubiri. Lakini, kukumbuka kwamba hakuna kitu kinaweza kuzuia Ufalme wa Mungu kutatupatia nguvu ya kuendelea kuhubiri. Kwa mufano, wakati Ndugu Edwin Skinner alifika katika inchi ya India katika mwaka wa 1926, kulikuwa Mashahidi wadogo sana. Mwanzoni, hakukuwa maendeleo mengi, na ilisemwa kwamba kazi ya kuhubiri “ilikuwa inaendelea polepole sana.” Lakini aliendelea kuhubiri na akaona namna ujumbe wa Ufalme unaendelea ijapokuwa vipingamizi vingi. Leo katika inchi hiyo kuna Mashahidi wenye bidii zaidi ya 37000, na watu zaidi ya 108000 walihuzuria Ukumbusho katika mwaka wa 2013. Tufikirie mufano mwingine wenye unaonyesha namna Ufalme ulipanuka kwa njia yenye kushangaza. Katika mwaka huohuo wa 1926, kazi ya kuhubiri ilikuwa tu imeanza katika inchi ya Zambia. Lakini, leo wahubiri zaidi ya 170000 wanahubiri katika inchi hiyo, na watu 763915 walihuzuria Ukumbusho katika mwaka wa 2013. Hilo linaonyesha kwamba mutu mumoja kati ya kila watu 18 alihuzuria Ukumbusho katika inchi ya Zambia. Hilo ni ongezeko kubwa kabisa!

MUFANO WA CHACHU

10. Mufano wa chachu unamaanisha nini?

10 Soma Mathayo 13:33. Mufano wa chachu unamaanisha nini? Mufano huo unahusu pia ujumbe wa Ufalme na matokeo ya ujumbe huo. “Tonge lote” la unga linafananisha mataifa yote, na kuenea kwa chachu  katika tonge kunafananisha kuenea kwa ujumbe wa Ufalme kupitia kazi ya kuhubiri. Kukomaa kwa mbegu ya haradali kunaonekana wazi; lakini kuenea kwa chachu hakukuonekana wazi mwanzoni. Matokeo yalionekana kisha muda fulani.

11. Sababu gani Yesu alitumia mufano wa chachu?

11 Sababu gani Yesu alitumia mufano huo? Alitaka kuonyesha kwamba ujumbe wa Ufalme uko na uwezo wa kuenea sana na kutokeza mabadiliko. Ujumbe wa Ufalme umefika mupaka “sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Hata hivyo, mabadiliko yenye ujumbe huo umetokeza hayaonekane wazi mwanzoni, lakini yanafanyika. Mabadiliko yanafanyika kwa sababu watu wengi wanakubali ujumbe wa Ufalme na wanaacha ujumbe huo ubadilishe mwenendo wao.—Rom. 12:2; Efe. 4:22, 23.

12, 13. Toa mifano yenye kuonyesha namna ujumbe wa Ufalme umeenea kama vile Yesu alionyesha katika mufano wake wa chachu.

12 Mara nyingi matokeo ya kazi ya kuhubiri inaonekana kisha miaka mingi. Kwa mufano, katika mwaka wa 1982, ndugu Franz na dada Margit bibi yake, walikuwa wanatumikia kwenye biro ya tawi ya Brazili, na leo wanatumikia kwenye biro ya tawi ya inchi ingine. Wakati huo, walihubiri katika muji fulani mudogo. Kati ya wanafunzi wao wa Biblia kulikuwa mama mumoja pamoja na watoto wake ine. Mutoto wake mukubwa mwanaume, ambaye wakati huo alikuwa na miaka 12, alikuwa mwenye haya sana, na kila mara alijificha mbele funzo lianze. Wakati ndugu huyo na bibi yake walipewa mugawo mwingine, hawakuweza kuendelea kujifunza na familia hiyo. Lakini kisha miaka 25 walitembelea tena muji huo. Walikuta nini wakati walifika huko? Walikuta kutaniko la wahubiri 69, na 13 kati yao walikuwa mapainia wa kawaida. Wote walikuwa wanakusanyika katika Jumba mupya la Ufalme. Halafu ule mutoto mwenye alikuwa mwenye haya sana? Sasa yeye ni muratibu wa baraza la wazee! Kama vile chachu yenye Yesu alitumia katika mufano wake, ujumbe wa Ufalme ulienea na kubadilisha maisha ya watu wengi; jambo hilo lilifurahisha sana ndugu huyo na bibi yake!

13 Ujumbe wa Ufalme uko na uwezo usioonekana wa kubadilisha maisha ya watu, na jambo hilo limeonekana wazi katika inchi ambamo kazi yetu ya kuhubiri imekatazwa. Ni vigumu sana kujua namna ujumbe wa Ufalme umeenea katika inchi kama hizo, lakini matokeo yanatushangaza sana. Tuchukue mufano wa inchi ya Kuba. Ujumbe wa Ufalme ulifika katika inchi hiyo katika mwaka wa 1910, na Ndugu Russell akaitembelea katika mwaka wa 1913. Hata hivyo, mwanzoni hakukuwa maendeleo mengi. Tuseme nini leo? Leo kuna wahubiri wa habari njema zaidi ya 96000, na watu 229726 walihuzuria Ukumbusho katika mwaka wa 2013; ni kusema, mutu mumoja kati ya kila watu 48 wa inchi hiyo alihuzuria Ukumbusho. Hata katika inchi ambamo kazi yetu haikatazwe, ujumbe wa Ufalme umefika katika maeneo ambamo Mashahidi wa inchi hizo walifikiri kwamba hakuna ushahidi wenye kutolewa. *Mhu. 8:7; 11:5.

14, 15. (a) Tunaweza kufaidika namna gani na mambo yenye Yesu alifundisha katika mufano wake wa chachu? (b) Mufano huo unatufundisha nini juu ya Yehova na juu ya Yesu?

14 Tunaweza kufaidika namna gani na mambo yenye Yesu alifundisha katika mufano wake wa chachu? Wakati tunafikiri sana juu ya  mufano huo, tunaelewa kwamba hatupaswe kuhangaika sana wakati tunafikiria namna ujumbe wa Ufalme utafikia mamilioni ya watu ambao hawajausikia. Yehova iko na uwezo juu ya mambo yote. Lakini, sisi tuko na daraka gani? Neno la Mungu linajibu hivi: ‘Asubuhi panda mbegu zako na mupaka jioni usiache mukono wako upumuzike; kwa maana haujue ni wapi hii itafanikiwa, hapa ao pale, ao ikiwa zote mbili zitakuwa njema.’ (Mhu. 11:6) Bila shaka, hatutasahau kusali ili Yehova abariki kazi ya kuhubiri, zaidi sana katika inchi ambamo kazi yetu imekatazwa.—Efe. 6:18-20.

15 Tena, hatupaswe kuvunjika moyo ikiwa tunaona kwamba leo kazi yetu ya kuhubiri haina matokeo. Hatupaswe hata kidogo kuzarau “siku ya mambo madogo.” (Zek. 4:10) Kisha muda fulani, matokeo yanaweza kuwa mengi zaidi na tena ya ajabu kuliko yale yenye tuliwazia!—Zab. 40:5; Zek. 4:7.

MUFANO WA MUFANYABIASHARA MWENYE KUSAFIRI NA WA HAZINA ILIYOFICHWA

16. Mufano wa mufanyabiashara mwenye kusafiri na ule wa hazina iliyofichwa unamaanisha nini?

16 Soma Mathayo 13:44-46. Mufano wa mufanyabiashara mwenye kusafiri na ule wa hazina iliyofichwa unamaanisha nini? Wakati wa Yesu, wafanyabiashara fulani walikuwa wanasafiri mupaka sehemu za mbali, kama vile kwenye Bahari ya India ili kutafuta lulu iliyo nzuri zaidi. Mufanyabiashara mwenye kuzungumuziwa katika mufano huo anafananisha watu wenye moyo muzuri wenye wanafanya yao yote ili kutosheleza mahitaji yao ya kiroho. ‘Lulu moja ya samani kubwa,’ inafananisha kweli ya Ufalme yenye bei kubwa sana. Wakati mufanyabiashara huyo alitambua kwamba lulu hiyo ni ya lazima sana, alikuwa tayari kuuzisha “mara moja” vitu vyote vyenye alikuwa navyo ili kuinunua. Yesu alizungumuzia pia mwanaume fulani mwenye alikuwa anatumika katika shamba na ambaye alipata hazina “iliyofichwa.” Tofauti na mufanyabiashara, mwanaume huyo hakuwa anatafuta hazina. Lakini, kama vile mufanyabiashara alifanya, mwanaume huyo pia alikuwa tayari kuuzisha ‘vitu vyote alivyokuwa navyo’ ili hazina hiyo ikuwe yake.

17. Sababu gani Yesu alitumia mufano wa mufanyabiashara mwenye kusafiri na ule wa hazina iliyofichwa?

17 Sababu gani Yesu alitumia mifano hiyo mbili? Alipenda kuonyesha kwamba watu wanapata kweli kwa njia tofauti. Wamoja wanaitafuta na wamefanya yao yote ili kuipata. Wengine wameipata bila hata kuitafuta; pengine mutu fulani alikuja kuwahubiria. Hata hivyo, katika mifano hiyo mbili, kila mutu alitambua kwamba kitu chenye alivumbua ni cha lazima sana na alikuwa tayari kujitoa kabisa ili kikuwe chake.

18. (a) Tunaweza kufaidika namna gani na mifano hiyo mbili? (b) Mifano hiyo inatufundisha nini juu ya Yehova na juu ya Yesu?

18 Tunaweza kufaidika namna gani na mifano hiyo mbili? (Mt. 6:19-21) Ujiulize hivi: ‘Mimi niko tayari kutenda kama wanaume hao wawili? Mimi pia ninaona kwamba kweli ni ya lazima sana? Niko tayari kujitoa kabisa ili niendelee kushikamana nayo, ao ninaacha mambo mengine, kama vile kuhangaikia sana maisha ya kila siku, yanikengeushe?’ (Mt. 6:22-24, 33; Lu. 5:27, 28; Flp. 3:8) Ikiwa tunafurahi sana kwa sababu tumepata kweli, itakuwa mwepesi kuendelea kuitia pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu.

19. Tutachunguza nini katika habari yenye inafuata?

19 Tuonyeshe basi kwamba tumesikia na kuelewa maana ya mifano hiyo ambayo inahusu Ufalme. Kumbuka kwamba haitoshe kujua tu maana, lakini inaomba kutumikisha mambo yenye mifano hiyo inatufundisha. Katika habari yenye inafuata, tutachunguza mifano ingine tatu na tutaona mambo yenye mifano hiyo inaweza kutufundisha.

^ fu. 13 Mambo kama hayo yalifanyika katika inchi kama vile Argentina (Kitabu cha Mwaka wa 2001, ukurasa wa 186, cha Kifaransa); Ujerumani Mashariki (Kitabu cha Mwaka wa 1999, ukurasa wa 83, cha Kifaransa); Papouasie Nouvelle Guinée (Kitabu cha Mwaka wa 2005, ukurasa wa 63); na katika Kisiwa cha Robinson Crusoe (Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 6, 2000, ukurasa wa 9).