Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Yeremia alimaanisha nini wakati alisema kwamba Raheli alilia watoto wake? 

Amekataa kufarijiwa juu ya wanawe, kwa sababu hawako tena.’”

Raheli alikufa mbele ya kufa kwa watoto wake wawili. Ndio sababu mambo yenye Yeremia aliandika miaka 1000 kisha Raheli kufa, yanaweza kuonekana kuwa haiko ya kweli.

Yosefu ndiye alikuwa mutoto wa kwanza wa Raheli. (Mwa. 30:22-24) Kisha, Raheli alizaa mutoto mwengine, ni kusema, Benyamini. Lakini Raheli alikufa wakati alikuwa anamuzaa Benyamini. Kwa hiyo, sababu gani andiko la Yeremia 31:15 linasema kwamba Raheli alilia watoto wake kwa sababu ‘hawakuwa tena’?

Ni vizuri kujua kwamba Yosefu, mutoto wa kwanza wa Raheli, alikuja kuzaa Manase na Efraimu. (Mwa. 41:50-52; 48:13-20) Baadaye, kabila la Efraimu lilikuja kuwa kabila kubwa na la maana zaidi kati ya makabila yote ya ufalme wa kaskazini wa Israeli na likakuja kuwakilisha makabila yote kumi. Tena, kabila la Benyamini, mwana wa pili wa Raheli, lilikuja kuwa sehemu ya ufalme wa kusini pamoja na Yuda. Kwa njia fulani, tunaweza kusema kwamba Raheli alifananisha wamama wote Waisraeli wa ufalme wa kaskazini na wa ufalme wa kusini.

Katika kipindi ambamo kitabu cha Yeremia kilikuwa kinaandikwa, ufalme wa kaskazini wa makabila kumi ulikuwa umeshambuliwa na Waashuru, na Waisraeli wengi walipelekwa katika inchi ya Waashuru. Hata hivyo, inawezekana kwamba wazao fulani wa Efraimu walikimbilia katika eneo la Yuda. Katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Wababiloni walishambulia ufalme wa kusini wa Yuda wenye makabila mbili. Inaonekana kwamba watu wengi kati ya wale wenye walikamatwa walikusanywa katika muji wa Rama, uliokuwa kwenye kilometre 8 kaskazini mwa Yerusalemu. (Yer. 40:1) Pengine wamoja waliuawa katika eneo hilo la Benyamini ambamo Raheli alizikwa. (1 Sam. 10:2) Kwa hiyo, kulia kwa Raheli juu ya watoto wake kunaweza kumaanisha kilio chake cha mufano juu ya Wabenyamini wote ao juu ya wale tu wa muji wa Rama. Ao tena, kilio hicho kinaweza kumaanisha kilio cha wamama wote Waisraeli ambao walilia kwa sababu ya kifo cha Waisraeli, ao kwa sababu ya kupelekwa kwa Waisraeli katika inchi zingine.

Iwe mafasirio ni gani, maneno ya Yeremia kuhusu Raheli anayelia watoto wake ilikuwa unabii kuhusu mambo yenye ingetokea miaka mingi kisha hapo, wakati uzima wa Yesu akiwa mutoto ungekuwa katika hatari. Mufalme Herode aliamuru kwamba watoto wote wanaume waliokuwa na miaka mbili ao chini katika muji wa Bethlehemu uliokuwa kusini mwa Yerusalemu wauawe. Kwa hiyo, watoto hao hawakuwa tena kwa sababu waliuawa. Wazia huzuni yenye wamama hao walikuwa nayo kwa sababu ya kupoteza watoto wao. Ni kama vile kilio chao kingeweza kusikiwa mbali sana kufika hata Rama, kaskazini mwa Yerusalemu.—Mt. 2:16-18.

Kwa hiyo, iwe wakati wa Yeremia ao wakati Yesu alikuwa mutoto, kilio cha Raheli juu ya watoto wake kilifananisha kabisa huzuni yenye wamama Wayahudi walikuwa nayo kwa sababu ya kifo cha watoto wao. Bila shaka, wale wenye wamekufa wako ‘katika inchi ya adui,’ ni kusema kifo, na wanaweza kuwekwa huru wakati watu wenye wamekufa watafufuliwa.—Yer. 31:16; 1 Kor. 15:26.