Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu habari za hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Ikiwa ni hivyo, jaribu kujibu maulizo haya:

Wakristo wanaweza kuchoma maiti?

Kuhusu jambo hilo kila Mukristo anapaswa kuamua yeye mwenyewe. Hata kama Biblia haizungumuzie waziwazi jambo hilo, inaonyesha kwamba maiti ya Mufalme Sauli na ya Yonathani mutoto wake ilichomwa mbele ya kuzikwa. (1 Sam. 31:2, 8-13)—15/06, ukurasa wa 7.

Tunajua namna gani kwamba Mungu hafanye mambo mabaya yatufikie?

Mungu ni muadilifu katika njia zake zote. Anatenda kwa haki, ni muaminifu, na ni munyoofu. Pia Yehova ni mwenye upendo mwororo na ni mwenye rehema. (Kum. 32:4; Zab. 145:17; Yak. 5:11)—01/07, ukurasa wa 4.

Wahubiri wenye wanahamia katika maeneo yaliyo na lazima kubwa wanaweza kupambana na magumu gani?

Wanaweza kupambana na magumu ya aina tatu: (1) hali mupya ya maisha, (2) kuwa mbali na familia, na (3) kupata marafiki. Ndugu na dada wengi wenye wamepambana na magumu hayo wamepata baraka nyingi.—15/07, ukurasa wa 4-5.

Sababu gani ndugu za Yosefu walimuchukia?

Sababu moja ni kwamba Yakobo alimupenda sana Yosefu kuliko ndugu zake, akamupatia nguo nzuri sana. Kwa hiyo, ndugu za Yosefu wakakuwa na wivu na wakamuuzisha ili akuwe mutumwa.—01/08, ukurasa wa 11-13.

Sababu gani trakte zetu mupya zinaleta matokeo mazuri na ni mwepesi kutumia?

Trakte hizo zote zina mupangilio wa namna moja. Kila trakte inatupatia nafasi ya kusoma andiko la Biblia na kuuliza musikilizaji ulizo. Iwe jibu la musikilizaji ni “ndiyo,” “hapana,” ao “pengine,” tunaweza kufungua trakte na kumuonyesha jibu la Biblia. Tunaweza pia kuuliza ulizo la kuzungumuzia wakati wa kumurudilia mutu.—15/08, ukurasa wa 13-14.

Peshitta ya Kisiria ni nini?

Kisiria, luga yenye inatokana na Kiaramu, ilianza kutumiwa sana katika miaka ya 100 ao 200 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Inaonekana kwamba Kisiria ndio luga ya kwanza yenye ilitumiwa ili kutafsiri sehemu fulani za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Biblia katika luga ya Kisiria ndio ilikuja kujulikana kuwa Peshitta.——01/09, ukurasa wa 13-14.

Wazazi Wakristo wanaweza kufanya nini ili wakuwe wachungaji wa watoto wao?

Ili kujua vizuri watoto wao, wazazi wanapaswa kuwasikiliza. Ni lazima kuwalisha kiroho. Ni lazima pia kuwaongoza kwa upendo, zaidi sana wakati wanakuwa na mashaka juu ya mafundisho fulani ya Biblia.—15/09, ukurasa wa 18-21.

Ni mambo gani hayatakuwa tena wakati Ufalme wa Mungu utaanza kutawala juu ya dunia?

Magonjwa, kifo, kukosa kazi, vita, njaa, na umaskini havitakuwa tena.—01/10, ukurasa wa 6-7.

Katika Biblia, ni agano gani linawezesha wanadamu fulani kutawala pamoja na Yesu?

Kisha kufanya Pasaka ya mwisho pamoja na mitume wake, Yesu alifanya agano pamoja na wanafunzi wake waaminifu; agano hilo linaitwa agano la Ufalme. (Lu. 22:28-30) Agano hilo liliwahakikishia kwamba watatawala pamoja na Yesu mbinguni.—15/10, ukurasa wa 16-17.

Toa mifano mbili ya Biblia yenye inaonyesha kwamba Shetani ni mutu kabisa.

Maandiko yanasema kwamba Shetani alizungumuza na Yesu ili kumujaribu. Tena, wakati wa Ayubu, Shetani alizungumuza na Mungu. Mifano hiyo inaonyesha kwamba Shetani ni mutu kabisa.— 01/11, ukurasa wa 4-5.

Kulingana na andiko la Matendo 15:14, “watu kwa ajili ya jina lake,” ambao Yakobo anataja ni nani?

Watu hao ni Wayahudi na Watu wa Mataifa wenye waliamini na ambao Mungu alifanya kuwa jamii iliyochaguliwa ili “watangaze kotekote sifa bora” zake Yeye aliyewaita. (1 Pet. 2:9, 10)—15/11, ukurasa wa 24-25.

Muji wa Timgad ulikuwa wapi, na wakaaji wa muji huo walikuwa na mwenendo gani?

Timgad ulikuwa muji wa Waroma uliokuwa Kaskazini mwa Afrika (katika inchi ya Algeria leo). Chombo fulani chenye kilichimbuliwa kinaonyesha mambo yenye wakaaji wa muji huo waliamini; kwenye chombo hicho kumeandikwa hivi: “Kuwinda, Kunawa, Kucheza, Kucheka—Hayo Ndiyo Maisha!” Mwenendo huo unafanana na ule wenye kuzungumuziwa katika andiko la 1 Wakorintho 15:32.—01/12, ukurasa wa 8-10.