Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

“Kipindi cha Maana Sana”

“Kipindi cha Maana Sana”

KATIKA mwaka wa 1870, kikundi kidogo cha watu katika muji wa Pittsburgh (Allegheny), Pennsylvania, États-Unis, kilianza kuchunguza Maandiko pamoja. Watu hao walikuwa wanaongozwa na ndugu Charles Taze Russell. Walijifunza juu ya zabihu ya ukombozi ya Yesu, na mara moja wakatambua kwamba zabihu hiyo ni ya maana sana katika kusudi la Yehova. Walifurahi sana kuelewa kwamba zabihu ya ukombozi inatolea wanadamu nafasi ya kuokolewa, hata kwa wale wenye hawajasikia juu ya Yesu. Walichochewa kuonyesha shukrani yao kwa kufanya kila mwaka Ukumbusho wa kifo cha Yesu.​—1 Kor. 11:23-26.

Ndugu Russell aliendelea kuchapisha gazeti Le Phare de la Tour de Sion, lenye lilionyesha wazi kwamba zabihu ya ukombozi ndio njia kubwa zaidi yenye Mungu ametumia ili kutuonyesha upendo wake. Gazeti Munara wa Mulinzi lilisema kwamba kipindi cha Ukumbusho wa kifo cha Yesu ni “kipindi cha maana sana,” na lilitia wasomaji moyo wahuzurie Ukumbusho, iwe katika muji wa Pittsburgh, ao mahali pengine kwenye watu wanaweza kukusanyika katika vikundi. Gazeti hilo lilisema hivi: “Hata kama kutakuwa tu watu wawili ao watatu wenye kuwa katika imani moja,” ao mutu mumoja tu, “Bwana atakuwa pamoja nao mahali hapo.”

Kila mwaka, watu wengi sana walikuwa wanaenda Pittsburgh ili kuhuzuria Ukumbusho. Mwaliko wa Ukumbusho ulikuwa na maneno haya: “Mutakaribishwa kwa furaha kubwa.” Wanafunzi wa Biblia wenye walikuwa wanaishi Pittsburgh walipatia ndugu na dada zao wa kiroho nafasi ya kulala, na waliwapatia chakula. Katika mwaka wa 1886, Wanafunzi wa Biblia walifanya “Mukusanyiko wa Watu Wote” katika kipindi cha Ukumbusho. Mukusanyiko huo ulifanya siku nyingi. Gazeti Munara wa Mulinzi lilisema hivi: “Mukuje, nyinyi wenye mioyo yenye kujaa upendo kwa ajili ya Bwana, kwa ajili ya ndugu zake, na kwa ajili ya kweli.”

Muchoro huu unaonyesha namna mukate na divai vilipitishwa kwenye Ukumbusho katika jumba la Tabernacle de Londres

Kwa miaka mingi, wanafunzi wa Biblia wenye walikuwa wanaishi Pittsburgh, walikuwa wanafanya mikusanyiko kwa ajili ya wale wenye kuwa na imani katika zabihu ya ukombozi na ambao walikuwa wanafika katika muji huo ili kuhuzuria Ukumbusho. Hesabu ya Wanafunzi wa Biblia iliongezeka sana; kwa hiyo, katika dunia yote, watu wenye kuhuzuria Ukumbusho waliongezeka pia. Ndugu Ray Bopp wa eklezia (kutaniko) ya Chicago, anakumbuka kwamba katika miaka ya 1910, iliomba saa nyingi ili kupitisha mukate na divai kwa mamia ya watu wenye walihuzuria Ukumbusho, kwa sababu karibu wote walikuwa wanakula mukate na kunywa divai.

Ni mifano gani ilitumiwa kwenye Ukumbusho? Gazeti Munara wa Mulinzi lilionyesha kwamba wakati Yesu alianzisha Ukumbusho wa kifo chake alitumia divai, lakini kwa muda fulani, lilisema watu watumie maji (jus) ya matunda ya muzabibu yenye walitoka tu kuchuma ao yenye wametokotesha. Lilisema watu wafanye hivyo ili wasitie katika jaribu “wale walio zaifu katika mwili.” Hata hivyo, kulikuwa pia divai kwa ajili ya wale wenye waliona kwamba “divai yenye chachu ilipaswa kutumiwa.” Baadaye wanafunzi wa Biblia walielewa kwamba divai nyekundu yenye haikuongezwa kitu ndio inastahili ili kufananisha damu ya Yesu.

Karatasi hii na kalamu vilipitishwa katika vyumba vya wafungwa ili kuandika hesabu ya watu wenye walihuzuria Ukumbusho katika gereza moja la Nikaragua

Kukumbuka kifo cha Yesu kuliwatolea watu nafasi ya kufikiri sana. Lakini katika makutaniko fulani, watu walikuwa wenye huzuni sana, na kisha tu Ukumbusho, wote walitoka bila kusema maneno mengi. Hata hivyo, kitabu chenye kichwa Jehovah, cha mwaka wa 1934, kilisema kwamba wakati wa Ukumbusho, watu hawapaswe kuwa na “huzuni” kwa sababu ya kifo cha Yesu chenye maumivu makali, lakini wanapaswa kuwa na “furaha,” kwa sababu yeye ni Mufalme mwenye kutawala tangu mwaka wa 1914.

Ndugu hawa wanakusanyika ili kufanya Ukumbusho katika kambi ya kazi ngumu ya Mordvinia, Urusi, katika mwaka wa 1957

Katika mwaka wa 1935 maana ya maneno ‘mukutano mukubwa(UV), ao ‘umati mukubwa’ yenye kupatikana katika andiko la Ufunuo 7:9 ilielezwa wazi, na hiyo ilikuwa mabadiliko makubwa sana kwa wale wenye kuhuzuria Ukumbusho. Mbele ya mwaka huo, watumishi wa Yehova walijua kwamba mukutano mukubwa ni Wakristo wenye wamejitoa kwa Yehova, kakini wenye hawakuwa na bidii. Lakini katika mwaka wa 1935, ilionyeshwa wazi kwamba mukutano mukubwa, ni watumishi waaminifu wa Yehova wenye kuwa na tumaini la kuishi katika Paradiso hapa duniani. Kisha kusikia mafasirio hayo mapya, na kisha kujichunguza vizuri, ndugu Russell Poggensee, alisema hivi: “Kupitia roho yake takatifu, Yehova alikuwa hajaamusha ndani yangu tumaini la kuenda mbinguni.” Ndugu Poggensee, na ndugu wengine wengi waaminifu, waliacha kula mukate na kunywa divai wakati wa Ukumbusho, lakini waliendelea kuhuzuria.

Kampanye zenye zilikuwa zinafanyika katika kipindi hicho “cha maana sana,” ziliwatolea wote nafasi ya kuonyesha shukrani kwa ajili ya zabihu ya ukombozi. Katika mwaka wa 1932, kichapo le Bulletin kilitia Wakristo moyo wasikuwe “watakatifu wa Ukumbusho,” ni kusema, watu wenye kula mukate na kunywa divai lakini bila kuwa “wafanyakazi wa kweli,” ao wahubiri wa ujumbe wa kweli. Katika mwaka wa 1934, kichapo hicho kilitia Wakristo moyo wakuwe “mapainia wasaidizi.” Kiliuliza hivi: “Kutakuwa mapainia wasaidizi 1 000 katika kipindi cha Ukumbusho?” Kichapo Informateur kilisema pia hivi kuhusu Wakristo watiwa-mafuta: “Watakuwa na furaha kabisa ikiwa tu wanatoa ushahidi juu ya Ufalme.” Wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi duniani wangepata pia furaha nyingi kwa kutoa ushahidi. *

Wakati alikuwa mufungwa, Harold King alitunga mashairi na nyimbo kwa ajili ya Ukumbusho

Watu wote wa Yehova wanaona kwamba siku ya Ukumbusho ndio siku takatifu zaidi katika mwaka. Wanafanya Ukumbusho hata katika hali ngumu. Katika mwaka wa 1930, dada Pearl English pamoja na Ora, dada yake, walitembea kilometre 80 hivi ili kuhuzuria Ukumbusho. Misionere mumoja anayeitwa Harold King, alikuwa anafungwa peke yake katika chumba cha gereza moja ya Uchina. Wakati huo, alitunga mashairi ( poèmes) na nyimbo kwa ajili ya Ukumbusho, na akatumia muchele na zabibu nyeusi ili kutengeneza mukate na divai. Kuanzia Mashariki mwa Ulaya mupaka Amerika ya Kati na katika Afrika, ndugu na dada walijikaza ili kukumbuka kifo cha Yesu, hata kama kazi yao ilikuwa imekatazwa ao walikuwa wanaishi nyakati za vita. Hata kama tuko wapi, ao tuko katika hali gani, tunakusanyika pamoja ili kuheshimu Yehova Mungu na Yesu Kristo katika kipindi hicho cha maana sana, ni kusema, kipindi cha Ukumbusho.

^ fu. 10 Kisha muda fulani, kichapo le Bulletin kiliitwa Informateur; leo kinaitwa Huduma Yetu ya Ufalme.