Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Sababu gani Tunapaswa Kukumbuka Kifo cha Yesu?

Kifo cha Yesu kinawezesha watu kuwa na tumaini gani la wakati unaokuja?—Isaya 25:8; 33:24

Kifo cha Yesu ndilo tukio la maana sana katika historia; alikufa ili kurudisha maisha ya watu namna yalipaswa kuwa. Wakati mutu aliumbwa hangeweza kufanya mambo mabaya, kugonjwa, ao kufa. (Mwanzo 1:31) Lakini zambi iliingia katika dunia kupitia mutu mumoja, Adamu. Yesu alitoa uzima wake ili kutuokoa kutoka katika zambi na kifo.—Soma Mathayo 20:28; Waroma 6:23.

Mungu alituonyesha upendo mukubwa sana kwa kutuma Mwana wake duniani ili akufe kwa ajili yetu. (1 Yohana 4:9, 10) Yesu aliwaambia wafuasi wake wakumbuke kifo chake kupitia tukio lisilokuwa na mambo mengi lenye kutia ndani mukate na divai. Wakati tunafanya hivyo kila mwaka, tunaonyesha shukrani yetu kwa ajili ya upendo Mungu na Mwana wake walituonyesha.—Soma Luka 22:19, 20.

Ni nani wanastahili kula mukate na kunywa divai?

Wakati Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwa mara ya kwanza wakumbuke kifo chake, alisema juu ya agano, ao mapatano. (Mathayo 26:26-28) Agano hilo liliwawezesha wao na hesabu kidogo ya watu wengine kupata tumaini la kuwa wafalme na makuhani pamoja naye mbinguni. Mamilioni ya watu wanakumbuka kifo cha Yesu, lakini ni wale tu wenye kuwa katika agano hilo ndio wanakula mukate na kunywa divai.—Soma Ufunuo 5:10.

Kwa miaka karibu 2000, Yehova amekuwa akichagua watu wenye watakuwa wafalme. (Luka 12:32) Watu hao ni wachache kwa kuwalinganisha na wale wenye wataishi milele kwenye dunia.—Soma Ufunuo 7:4, 9, 17.