Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Zamani katika vichapo vyetu, tulizoea kutumia vifananishi na vifananishwa, lakini katika miaka ya hivi karibuni hatuzoee tena kufanya hivyo. Sababu gani?

Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 9, 1950 ulifasiria “kifananishi” na “kifananishwa.” Ulisema kwamba kifananishi ni mufano wa jambo fulani lenye litafanyika wakati unaokuja. Ulisema pia kwamba kifananishwa ni ukweli wa jambo hilo. Kifananishi kinaweza kuitwa kivuli; na kifananishwa kinaweza kuitwa jambo halisi ao ukweli wa mambo.

Zamani vichapo vyetu vilionyesha kwamba wanaume na wanawake waaminifu kama vile Debora, Elihu, Yeftha, Ayubu, Rahabu, Rebeka, na wengine wengi, walikuwa vifananishi, ao vivuli vya watiwa-mafuta ao ‘umati [mukutano] mukubwa.’ (Ufu. 7:9) Kwa mufano, tulifikiri kwamba Yeftha, Ayubu, na Rebeka walifananisha watiwa-mafuta na kwamba Debora na Rahabu walifananisha mukutano mukubwa. Lakini, katika miaka ya hivi karibuni, hatufikiri tena hivyo. Sababu gani?

KIFANANISHI

Zabihu ya pasaka ambayo ilitolewa katika Israeli ya zamani ilikuwa kifananishi.—Hes. 9:22

KIFANANISHWA

Paulo alitaja Yesu kuwa “pasaka yetu.” —1 Kor. 5:7

Maandiko yanaonyesha kwamba watu fulani wenye kuzungumuziwa katika Biblia walikuwa vifananishi vya mambo fulani makubwa zaidi. Katika andiko la Wagalatia 4:21-31, mutume Paulo anataja ‘tukio la mufano’ lenye kuhusu wanawake wawili. Hagari, kijakazi wa Abrahamu, alifananisha taifa la Israeli, ambalo lilipatanishwa na Yehova kupitia Sheria ya Musa. Lakini Sara, ‘mwanamuke huru,’ alifananisha mwanamuke wa Mungu, ni kusema, sehemu ya mbinguni ya tengenezo lake. Katika barua yake kwa Waebrania, mutume Paulo anafananisha Melkizedeki, kuhani-mufalme, na Yesu kwa kuonyesha mambo yenye kufanana kati yao. (Ebr. 6:20; 7:1-3) Zaidi ya hilo, mutume Paulo analinganisha Isaya na Yesu, na analinganisha watoto wa Isaya na wafuasi watiwa-mafuta wa Yesu. (Ebr. 2:13, 14) Mutume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili aandike maneno hayo; kwa hiyo, tunaamini kabisa mambo yenye anasema kuhusu vifananishi hivyo.

Lakini, hata kama Biblia inaonyesha kwamba mutu fulani ni kifananishi cha mutu mwengine, hatupaswe kusema mara moja kwamba kila jambo katika maisha ya mutu huyo linafananisha jambo fulani kubwa zaidi. Kwa mufano, hata kama anasema kwamba Melkizedeki anafananisha Yesu, mutume Paulo haseme jambo fulani kuhusu wakati Melkizedeki alimuletea Abrahamu mukate na divai ili afurahi kisha Abrahamu kupata ushindi juu ya wafalme ine. Kwa hiyo, hakuna andiko lenye linafasiria maana ya tukio hilo.—Mwa. 14:1, 18.

Kwa miaka mingi kisha kifo cha Yesu, waandikaji wengi waliangukia katika mutego wa kufananisha kila jambo katika Biblia. Kuhusiana na mafundisho ya Origène, Ambroise, na Jérôme, kitabu The International Standard Bible Encyclopaedia kinasema hivi: “Walitafuta kujua vifananishi, na kwa kweli walivipata katika kila tukio linalozungumuziwa katika Biblia, hata katika jambo lisilo la lazima. Waliona kwamba hata hali ya kawaida zaidi ilificha kweli fulani ya maana sana . . . , wamejikaza hata kufananisha samaki 153 zenye wanafunzi walinasa usiku ambao Mukombozi aliyefufuliwa aliwatokea!”

Augustin d’Hippone alieleza mambo mengi kuhusu habari yenye kuonyesha kwamba Yesu alitumia mikate tano ya shayiri na samaki mbili ili kukulisha karibu wanaume 5000. Shayiri ilionwa kuwa ya hali ya chini kwa kuilinganisha na ngano; kwa hiyo, Augustin alisema kwamba mikate tano ya shayiri inapaswa kufananisha vitabu tano vya Musa (“shayiri” hiyo ya hali ya chini ilifananisha “Agano la Kale” ambalo lilionwa kuwa halina maana). Samaki mbili zilifananisha nini? Mambo fulani ilimuchochea Augustin afananishe samaki hizo na mufalme na kuhani. Mutu mwengine mwenye elimu ya Biblia ambaye alipenda sana kutafuta vifananishi na vifananishwa alisema kwamba tendo la Yakobo la kununua haki ya muzaliwa wa kwanza ya Esau kupitia bakuli la chakula chekundu, lilifananisha tendo lenye Yesu alifanya kupitia damu yake nyekundu ili awezeshe wanadamu kuenda mbinguni!

Ikiwa unaona kwamba ni vigumu kuamini mafasirio hayo, unaweza kujua ni sababu gani. Wanadamu hawawezi kujua kabisa ni habari gani za Biblia zenye kufananisha na zenye hazifananishe mambo ya wakati unaokuja. Kwa hiyo, wakati Maandiko yanasema kwamba mutu, tukio, ao kitu fulani kinafananisha jambo fulani, tunapaswa kukubali mambo hayo. Pia, tunapaswa kuepuka kuonyesha kwamba mutu ao habari fulani ya Biblia inafananisha mambo ya wakati unaokuja ikiwa hakuna andiko fulani lenye kuonyesha sababu za kufanya hivyo.

Namna gani basi tunaweza kufaidika na matukio na mifano yenye kuzungumuziwa katika Biblia? Katika andiko la Waroma 15:4, mutume Paulo aliandika hivi: “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutokana na Maandiko tuwe na tumaini.” Mutume Paulo alikuwa anaonyesha kwamba matukio yenye kupatikana katika Biblia yangeweza kuwafundisha ndugu zake watiwa-mafuta wa siku zake mambo ya maana sana. Hata hivyo, watu wa Mungu wa wakati wote, iwe ni watiwa-mafuta ao “kondoo wengine,” iwe wanaishi katika “siku za mwisho” ao hapana, wanaweza kufaidika na wamefaidika na mambo yenye wanajifunza katika “mambo yote yaliyoandikwa zamani.”—Yoh. 10:16; 2 Tim. 3:1.

Kuliko kuona kwamba habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia zinahusu tu kikundi kimoja, ni kusema, kikundi cha Wakristo watiwa-mafuta ao mukutano mukubwa, na katika kipindi fulani tu cha wakati, watu wa Mungu wa vikundi vyote viwili na wa wakati wote wamefaidika na mambo yenye habari hizo zinatufundisha. Kwa mufano, hatuwezi kusema kwamba kitabu cha Ayubu kinahusu tu Wakristo watiwa-mafuta wenye walivumilia majaribu wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu. Watumishi wengi wa Mungu, wanaume na wanawake, watiwa-mafuta na wa mukutano mukubwa, wamepambana na majaribu kama ya Ayubu, na ‘wameona matokeo ambayo Yehova alileta, kwamba Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema.’—Yak. 5:11.

Leo, katika makutaniko yetu, kuna wanawake waaminifu kama Debora, wazee vijana wenye hekima kama Elihu, mapainia wenye bidii kama Yeftha, na wanaume na wanawake waaminifu wenye uvumilivu kama Ayubu. Tuko wenye shukrani sana kwa Yehova kwa sababu alichunga “mambo yote yaliyoandikwa zamani,” ili “kupitia faraja kutokana na Maandiko tuwe na tumaini”!

Kwa hiyo, katika miaka ya hivi karibuni vichapo vyetu vimekazia mambo yenye tunaweza kujifunza katika habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia kuliko kutafuta kujua vifananishi na vifananishwa kuhusu habari fulani.

Zabihu ya pasaka ambayo ilitolewa katika Israeli ya zamani ilikuwa kifananishi.—Hes. 9:2