Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uendelee Kutegemeza Ndugu za Kristo kwa Uaminifu

Uendelee Kutegemeza Ndugu za Kristo kwa Uaminifu

Kwa kadiri ambayo mulimutendea hilo mumoja wa walio wadogo zaidi wa ndugu zangu hawa, mulinitendea mimi.’—MT. 25:40.

1, 2. (a) Yesu alizungumuzia mufano gani pamoja na marafiki wake wa sana? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Tutajifunza mambo gani katika mufano wa kondoo na mbuzi?

YESU amemaliza kuzungumuza na mutume Petro, Andrea, Yakobo, na Yohana, marafiki wake wa sana. Wametoka tu kumusikiliza wakati alikuwa anazungumuzia mufano wa mutumwa mwaminifu na mwenye busara, mabikira kumi, na mufano wa talanta. Yesu anamalizia mazungumuzo yake kwa kuwatolea mufano mwingine. Katika mufano huo, anazungumuzia wakati “Mwana wa binadamu” atahukumu “mataifa yote.” Bila shaka, mufano huo uliwavutia sana wanafunzi wa Yesu! Katika mufano huo, Yesu anakazia vikundi viwili; kikundi kimoja ni kondoo na kingine ni mbuzi. Kisha, anazungumuzia kikundi cha tatu ambacho ni cha maana na anaonyesha kwamba kikundi hicho ni “ndugu” za ‘Mufalme.’—Soma Mathayo 25:31-46.

2 Kwa muda wa miaka mingi mufano huo umewavutia sana watu wa Yehova, kwa sababu katika mufano huo, Yesu anazungumuzia mambo yenye itawapata wanadamu wakati unaokuja. Anaonyesha sababu gani watu fulani watapata uzima wa milele na wengine wataharibiwa milele. Ili kupata uzima wa milele, tunapaswa kuelewa kweli yenye Yesu anatufundisha kupitia mufano huo na kutenda kulingana na kweli hiyo. Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: Namna gani Yehova ametusaidia hatua kwa hatua kuelewa muzuri zaidi mufano huo? Sababu gani tunaweza kusema kwamba mufano huo unakazia kwamba ni lazima kufanya kazi ya kuhubiri? Ni nani wamepewa daraka la kuhubiri? Sababu gani huu ndio wakati wa kuwa waaminifu kwa ‘Mufalme’ na kwa wale wenye anaita “ndugu zangu”?

NAMNA TUMEELEWA MUZURI ZAIDI MUFANO WA KONDOO NA MBUZI

3, 4. (a) Ni mambo gani ya lazima tunapaswa kujua ili tuelewe mufano wa kondoo na mbuzi? (b) Katika mwaka wa 1881, namna gani gazeti Le Phare de la Tour de Sion lilifasiria mufano wa kondoo na mbuzi?

3 Ili tuelewe vizuri mufano wa kondoo na mbuzi, ni lazima tujue mambo ya lazima yenye kupatikana katika mufano huo: Ni nani wenye kuzungumuziwa katika mufano huo, hukumu itafanyika wakati gani, na sababu gani watu fulani wanahukumiwa kuwa kondoo ao mbuzi.

4 Katika mwaka wa 1881, gazeti Le Phare de la Tour de Sion, lilionyesha kwamba “Mwana wa binadamu” ambaye anaitwa pia ‘Mufalme,’ ni Yesu. Wanafunzi wa Biblia wa kwanza-kwanza walielewa kwamba maneno “ndugu zangu” yenye kupatikana katika tafsiri ya King James Version, inahusu wale wenye watatawala pamoja na Kristo, na pia wanadamu wote wenye watakuwa wamerudishwa kwenye ukamilifu duniani. Walifikiri kwamba kutenganisha kondoo na mbuzi kungefanyika wakati wa Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu Moja. Waliamini pia kwamba watu fulani wangehukumiwa kuwa kondoo kwa sababu waliishi kulingana na sheria ya Mungu yenye upendo.

5. Katika miaka ya 1920, namna gani tulielewa muzuri zaidi mufano wa kondoo na mbuzi?

5 Mwanzoni mwa miaka ya 1920, Yehova alisaidia watumishi wake waelewe muzuri zaidi mufano huo. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 10, 1923, lilihakikisha kwamba “Mwana wa binadamu” ni Yesu. Hata hivyo, lilitoa mafasirio yenye kuwa wazi na yenye kutegemea Maandiko ambayo yalionyesha kwamba wale wenye kuitwa ndugu za Kristo ni wale tu wenye watatawala pamoja naye mbinguni. Pia gazeti hilo likaonyesha kwamba kondoo ni wale wenye kuwa na tumaini la kuishi duniani na ambao watatawaliwa na Ufalme wa Kristo. Ni wakati gani Yesu atatenganisha kondoo na mbuzi? Gazeti hilo lilionyesha kwamba ndugu za Kristo watatawala pamoja naye mbinguni katika Utawala wa Miaka Elfu Moja. Kwa hiyo, hawatakuwa na lazima ya kusaidiwa ao kuachiliwa na wale wenye kuishi duniani. Ndiyo sababu tunasema kwamba Yesu atatenganisha kondoo na mbuzi mbele ya Utawala wa Miaka Elfu Moja kuanza. Sababu gani watu fulani watahukumiwa kuwa kondoo? Gazeti hilo lilionyesha kwamba watu fulani watahukumiwa kuwa kondoo, kwa sababu walimukubali Yesu kuwa Bwana wao na kwa sababu walikuwa na tumaini kwamba Ufalme utaleta hali nzuri zaidi duniani.

6. Katika miaka ya 1990, namna gani watumishi wa Yehova walielewa tena muzuri zaidi mufano wa kondoo na mbuzi?

6 Kwa sababu ya mafasirio hayo mapya, watumishi wa Yehova walifikiri kwamba katika siku za mwisho, watu wangehukumiwa kuwa kondoo ao mbuzi kulingana na namna wangeitikia ujumbe wa Ufalme. Hata hivyo, katikati ya miaka ya 1990, tulipata mafasirio mengine mapya kuhusu mufano huo. Habari mbili za kujifunza katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 1995, zilionyesha namna maneno ya Yesu katika Mathayo 24:29-31 (soma) inapatana na yale yenye kupatikana katika Mathayo 25:31, 32. (Soma.) * Walifikia uamuzi gani? Habari ya kwanza katika gazeti hilo ilisema hivi: “Kutenganisha kwa kondoo na mbuzi kutafanyika wakati unaokuja.” Ni wakati gani kabisa? “Ni kisha kuanza kwa ‘ziki’ yenye kuzungumuziwa katika Mathayo 24:29, 30 na Mwana wa binadamu ‘kufika katika utukufu wake.’ . . . Kisha ulimwengu huu wote muovu kufikia mwisho, Yesu atafanya mahakama (tribinali) na kutoa hukumu na kuitimiza.”

7. Namna gani tunaelewa leo mufano wa kondoo na mbuzi?

7 Leo, tunaelewa muzuri zaidi mufano wa kondoo na mbuzi. Kuhusu ulizo ni nani wenye kuzungumuziwa katika mufano huo, Yesu ndiye “Mwana wa binadamu,” ni kusema, Mufalme. Wale wenye Yesu anaita “ndugu zangu,” ni wanaume na wanawake wenye walitiwa mafuta kwa roho ili watawale pamoja na Kristo huko mbinguni. (Rom. 8:16, 17) “Kondoo” na “mbuzi,” wanafananisha watu wa mataifa yote. Watu hao hawakutiwa mafuta kwa roho takatifu. Hukumu itafanywa wakati gani? Hukumu hiyo itafanywa mbele ziki kubwa imalizike. Na sababu gani watu fulani watahukumiwa kuwa kondoo ao mbuzi? Watahukumiwa kulingana na namna watakuwa wamewatendea ndugu watiwa-mafuta wa Kristo ambao walikuwa wangali duniani. Kwa sababu mwisho wa ulimwengu huu unakaribia sana, tunashukuru sana kuona namna Yehova ametusaidia hatua kwa hatua kuelewa mufano wa kondoo na mbuzi, na mifano ingine yenye kupatikana katika Mathayo sura ya 24 na 25!

NAMNA GANI MUFANO HUO UNAKAZIA KAZI YA KUHUBIRI?

8, 9. Sababu gani kondoo wanaonwa kuwa ‘waadilifu’?

8 Katika mufano wa kondoo na mbuzi, Yesu hakuzungumuzia waziwazi kazi ya kuhubiri. Kwa hiyo, sababu gani tunaweza kusema kwamba mufano huo unaonyesha kwamba ni jambo la lazima kuhubiri?

9 Kwanza, ukumbuke kwamba wakati huo Yesu anafundisha kwa kutumia mufano. Ni wazi kwamba Yesu anazungumuzia kondoo na mbuzi wa mufano. Vilevile, Yesu anatumia maneno ya mufano wakati anasema kwamba kila mutu ambaye ni mufano wa kondoo anaombwa kulisha, kuvalisha, kutunza, ao kutembelea ndugu zake katika gereza. Lakini, anazungumuzia namna kondoo wa mufano wanapaswa kutendea ndugu zake. Anasema kwamba kondoo ni ‘waadilifu [wenye haki]’ kwa sababu wanatambua kwamba Kristo iko na kikundi cha ndugu zake watiwa-mafuta ambao wangali duniani, na kwa sababu wanategemeza kwa uaminifu watiwa-mafuta hao katika siku hizi za mwisho zenye hatari.—Mt. 10:40-42; 25:40, 46; 2 Tim. 3:1-5.

10. Namna gani kondoo wanaweza kusaidia ndugu za Kristo?

10 Pili, tuchunguze mambo yenye Yesu alikuwa anazungumuzia wakati alitoa mufano huo. Alikuwa anazungumuzia alama ya kuja kwake na ya mwisho wa ulimwengu huu muovu. (Mt. 24:3) Katika maneno ya kwanza-kwanza ya hotuba yake, Yesu alionyesha kwamba sehemu ya maana sana ya alama hiyo, ni kuhubiri habari njema ya Ufalme “katika dunia yote inayokaliwa.” (Mt. 24:14) Na mbele ya kuzungumuzia mufano wa kondoo na mbuzi, Yesu alizungumuzia mufano wa talanta. Kama vile tuliona katika habari yenye ilitangulia, Yesu alitoa mufano huo ili kukazia kwamba wafuasi wake waliotiwa mafuta kwa roho, ni kusema, “ndugu” zake, wanapaswa kuhubiri kwa bidii. Hata hivyo, kikundi kidogo cha watiwa-mafuta wenye wangekuwa duniani wakati wa kuwapo kwa Yesu, wangepaswa kufanya kazi kubwa sana, ni kusema, kuhubiria “mataifa yote” mbele mwisho ufike. Mufano wa kondoo na mbuzi unaonyesha kwamba watiwa-mafuta wangesaidiwa. Na njia kubwa zaidi ambayo wale wenye kuwa mufano wa kondoo wanatumia ili kusaidia ndugu za Kristo, ni kuwategemeza katika kazi ya kuhubiri. Ni mambo gani wanafanya ili kuwategemeza katika kazi hiyo? Wanatoa tu michango na kuwafariji, ao kuna mambo mengine yenye wanaombwa kufanya?

NI NANI WANAPASWA KUHUBIRI?

11. Tunaweza kujiuliza ulizo gani, na sababu gani?

11 Leo, Yesu iko na wanafunzi milioni 8 hivi; lakini wanafunzi wengi sana kati yao hawako watiwa-mafuta. Hawakupokea talanta zenye Yesu alipatia watumwa wake watiwa-mafuta. (Mt. 25:14-18) Sasa tunaweza kujiuliza hivi: ‘Je, Wakristo wenye hawako watiwa-mafuta wanapaswa kuhubiri pia?’ Tuchunguze sababu fulani zenye kuonyesha kwamba wao pia wanapaswa kuhubiri.

12. Maneno ya Yesu katika Mathayo 28:19, 20 inatufundisha nini?

12 Yesu aliamuru wanafunzi wake wote wahubiri. Kisha kufufuliwa, Yesu aliambia wafuasi wake wafanye wanafunzi, na kuwafundisha kushika “mambo yote” yenye aliamuru. Kati ya mambo yenye Yesu aliamuru kulikuwa daraka la kuhubiri. (Soma Mathayo 28:19, 20.) Kwa hiyo, wanafunzi wote wa Kristo wanapaswa kuhubiri, iwe watatawala mbinguni ao wataishi duniani.—Mdo. 10:42.

13. Maono ya mutume Yohana inaonyesha nini, na sababu gani?

13 Kitabu cha Ufunuo kinaonyesha kwamba Wakristo watiwa-mafuta na kondoo wengine wanapaswa kuhubiri. Katika maono, Yesu alimusaidia mutume Yohana aone “bibi-arusi,” ni kusema, watiwa-mafuta 144000 wenye watatawala pamoja na Kristo mbinguni. Watiwa-mafuta hao walikuwa wanaalika watu ‘wachukue maji ya uzima bure.’ (Ufu. 14:1, 3; 22:17) Maji hayo ni mipango yenye Yehova amekamata ili kukomboa wanadamu kutoka katika utumwa wa zambi na kifo kupitia zabihu ya ukombozi ya Kristo. (Mt. 20:28; Yoh. 3:16; 1 Yoh. 4:9, 10) Zabihu ya ukombozi ni sehemu ya maana sana ya ujumbe wenye tunahubiria watu, na Wakristo watiwa-mafuta ndio wenye kuwa kwenye mustari wa mbele katika kazi ya kusaidia watu wajifunze faida yenye zabihu hiyo inaweza kuwaletea. (1 Kor. 1:23) Lakini, katika maono hayo, mutume Yohana aliona watu wengine wenye hawako katika kikundi cha bibi-arusi. Wao pia wamepewa amri ya kusema, “Njoo!” Wanatii amri hiyo kwa kuendelea kualika watu wachukue maji ya uzima. Kikundi hicho cha pili ni wale wenye kuwa na tumaini la kuishi duniani. Kwa hiyo, maono hayo inaonyesha wazi kwamba wote wenye wanakubali mualiko wa kusema “njoo,” wako na daraka la kuhubiria wengine.

14. Kuongozwa na “sheria ya Kristo” kunamaanisha nini?

14 Wale wenye kuongozwa na “sheria ya Kristo” wanapaswa kuhubiri. (Gal. 6:2) Yehova anatumia kanuni zilezile kwa watumishi wake wote. Kwa mufano, aliwaambia Waisraeli hivi: ‘Sheria moja itakuwa kwa ajili ya mwenyeji na kwa ajili ya mukaaji mugeni anayekaa akiwa mugeni katikati yenu.’ (Kut. 12:49; Law. 24:22) Wakristo hawaongozwe na Sheria ya Musa. Lakini sisi wote, iwe tuko watiwa-mafuta ao hapana, tunaongozwa na “sheria ya Kristo.” Sheria hiyo ni mambo yote yenye Yesu alifundisha. Jambo la maana sana kati ya mambo yenye Yesu alifundisha wafuasi wake ni upendo. (Yoh. 13:35; Yak. 2:8) Kuhubiri habari njema ya Ufalme ndiyo njia moja kubwa ya kuonyesha kwamba tunapenda Mungu, Kristo, na majirani wetu.—Yoh. 15:10; Mdo. 1:8.

15. Sababu gani tunaweza kusema kwamba amri ya Yesu ya kuhubiri inahusu wafuasi wake wote?

15 Maneno yenye Yesu anawaambia wanafunzi wachache, yanaweza pia kuhusu wanafunzi wote. Kwa mufano, Yesu alifanya agano la Ufalme pamoja na wanafunzi 11 tu; lakini agano hilo linahusu Wakristo watiwa-mafuta 144000. (Lu. 22:29, 30; Ufu. 5:10; 7:4-8) Vilevile, kisha kufufuliwa, Yesu aliwatokea tu wafuasi wake wachache na akawapatia amri ya kuhubiri. (Mdo. 10:40-42; 1 Kor. 15:6) Lakini wanafunzi wake wote waaminifu wa wakati wa mitume walielewa kwamba amri hiyo iliwahusu pia, hata kama Yesu hakuwapatia amri hiyo moja kwa moja. (Mdo. 8:4; 1 Pet. 1:8) Leo pia, Yesu hazungumuze moja kwa moja na watu milioni 8 hivi wenye kufanya kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme. Lakini wote wanaelewa kwamba wanapaswa kuwa na imani katika Kristo, na kwamba wanapaswa kuonyesha imani hiyo kupitia kazi ya kuhubiri.—Yak. 2:18.

HUU NDIO WAKATI WA KUONYESHA UAMINIFU WETU

16-18. Ikiwa tunapenda tuhukumiwe kuwa kondoo wakati unaokuja, namna gani tunapaswa kutegemeza ndugu za Kristo, na sababu gani huu ndio wakati wa kufanya hivyo?

16 Shetani anaendelea kupiganisha sana mabaki ya ndugu watiwa-mafuta wa Kristo wenye kuwa duniani, na ataongeza mashambulio yake kwa sababu anajua kwamba anabakia tu na “kipindi kifupi cha wakati.” (Ufu. 12:9, 12, 17) Wakristo watiwa-mafuta wanavumilia majaribu hayo makali; lakini wanakuwa kwenye mustari wa mbele katika kazi kubwa zaidi ya kuhubiri habari njema. Bila shaka, Yesu iko pamoja nao, na anaendelea kuwaongoza.—Mt. 28:20.

17 Watu wenye wataonwa kuwa kondoo wanaendelea kuongezeka. Watu hao wanaona kuwa ni pendeleo kutegemeza ndugu za Kristo katika kazi ya kuhubiri na katika njia zingine. Kwa mufano, wanatoa michango na wanasaidia kujenga Majumba ya Ufalme, Majumba ya Mikusanyiko, na majengo ya tawi. Pia, wanatii kwa uaminifu wale wenye ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ ameweka ili kuwaongoza.—Mt. 24:45-47; Ebr. 13:17.

Wale wenye kuwa mufano wa kondoo wanategemeza ndugu za Kristo katika njia mbalimbali(Ona fungu la 17)

18 Hivi karibuni, malaika wataachilia zile pepo za uharibifu za ziki kubwa. Jambo hilo litatokea kisha ndugu za Kristo wenye kuwa duniani kutiwa muhuri kwa mara ya mwisho. (Ufu. 7:1-3) Wakristo watiwa-mafuta watapelekwa mbinguni mbele vita ya Har-magedoni ianze. (Mt. 13:41-43) Kwa hiyo, ikiwa tunapenda tuhukumiwe kuwa kondoo wakati unaokuja, huu ndio wakati wa kuwategemeza ndugu za Kristo kwa uaminifu.

^ fu. 6 Ili kupata maelezo zaidi juu ya mufano wa kondoo na mbuzi, soma habari zenye kichwa “Utasimamaje Mbele ya Kiti cha Hukumu?” na “Kuna Wakati Ujao Gani kwa Kondoo na Mbuzi?” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 1995.