Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | UNAPENDA KUJIFUNZA BIBLIA?

Programu ya Kujifunza Biblia na Watu Wote

Programu ya Kujifunza Biblia na Watu Wote

Mashahidi wa Yehova wanajulikana kwa sababu ya kazi yao ya kuhubiri waziwazi. Lakini unajua kama tuko pia na programu ya kujifunza Biblia na watu katika dunia yote?

Katika mwaka wa 2014, Mashahidi wa Yehova zaidi ya 8000000, katika inchi 240, waliongoza mafunzo ya Biblia karibu 9500000 kila mwezi. * Kwa kweli, hesabu ya watu wenye tunajifunza nao Biblia inapita hesabu ya wakaaji wa inchi moja-moja 140 hivi!

Ili kutimiza kazi hiyo ya kufundisha watu, Mashahidi wa Yehova wanachapisha kila mwaka karibu miliare moja na nusu ya Biblia, vitabu, magazeti, na vichapo vingine vya kusaidia watu kujifunza Biblia, katika luga 700 hivi! Kazi hiyo ya kuchapisha vichapo isiyoweza kulinganishwa inawezesha watu kujifunza Biblia katika luga yenye wanapenda.

MAJIBU YA MAULIZO YENYE WATU WANAULIZA SANA JUU YA PROGRAMU YETU YA KUJIFUNZA NA WATU BIBLIA

Funzo la Biblia linafanywa namna gani?

Tunachukua habari mbalimbali za Biblia na kisha tunachunguza maandiko yenye kuhusu habari hizo. Kwa mufano, Biblia inajibia maulizo kama haya: Mungu ni nani? Iko namna gani? Iko na jina? Anaishi wapi? Tunaweza kumukaribia? Haiko vyepesi kujua ni wapi tunaweza kutafuta majibu ya maulizo hayo katika Biblia.

Ili kusaidia watu wapate majibu ya maulizo hayo, kwa kawaida tunatumia kitabu chenye kurasa 224 kinachoitwa Biblia Inafundisha Kabisa Nini? * Kitabu hicho kilichapishwa ili kusaidia watu waelewe mafundisho ya musingi ya Biblia. Kinazungumuzia habari juu ya Mungu, Yesu Kristo, mateso ya wanadamu, ufufuo, sala, na habari zingine nyingi.

Funzo la Biblia linaweza kufanywa wapi na wakati gani?

Funzo la Biblia linaweza kufanywa mahali na wakati unapenda.

Funzo la Biblia linafanywa kwa muda gani?

Watu wengi wanapanga kujifunza Biblia kwa saa moja hivi kila juma. Lakini muda wa kujifunza unaweza kubadilika. Tutajifunza kwa muda unaopatana na programu yako. Watu fulani wanajifunza kwa dakika 10 ao 15 tu kila juma.

Inaomba kulipa feza ngapi ili kujifunza Biblia?

Hautalipa funzo na vichapo vya funzo. Hilo linapatana na agizo hili lenye Yesu alipatia wafuasi wake: ‘Mulipokea bure, mutoe bure.’—Mathayo 10:8.

Funzo la Biblia linachukua miezi ngapi?

Ni wewe utaamua ikiwa funzo litachukua miezi ngapi. Kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kina sura 19. Unaweza kujifunza sura fulani ao sura zote kwa mwendo unaokufaa.

Nitalazimika kuwa Shahidi wa Yehova?

Hapana. Kwa sababu tunaheshimu watu, tunajua kama kila mutu iko na haki ya kuchagua mambo ataamini. Lakini, watu wenye wamejifunza mafundisho ya musingi ya Biblia wanaweza kuchukua uamuzi wenye kutegemea mambo yenye wamejifunza.

Ninaweza kupata wapi habari zaidi?

Adresi yetu ya Internete jw.org inatoa habari za kweli juu ya mambo yenye Mashahidi wa Yehova wanaamini na juu ya kazi zao.

Ninaweza kuomba funzo la Biblia namna gani?

^ fu. 4 Kwa kawaida wanajifunza Biblia na mutu mumoja-mumoja ao na vikundi vidogo-vidogo vya watu.

^ fu. 9 Kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Vitabu zaidi ya milioni 230 vimechapishwa katika luga zaidi ya 260.