Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | WATU WALIOKUFA—WANAWEZA KUISHI TENA?

Ni Nini Kinatokea Kisha Mutu Kufa?

Ni Nini Kinatokea Kisha Mutu Kufa?

“Niliwaza kuko nafasi tatu kwenye mutu anaweza kwenda kisha kufa: mbinguni, katika moto wa mateso, ao katika pirigatori. Nilijua kama sikukuwa mutu muzuri sana ili kwenda mbinguni ao mubaya sana ili kwenda katika moto wa mateso. Sikujua muzuri ni nini inafanyika katika pirigatori. Na nilikuwa sijasoma mambo hayo yote katika Biblia. Ni watu tu walikuwa wanasema hivyo.”—Lionel.

“Nilifundishwa kama watu wote wanaenda mbinguni kisha kufa, lakini sikuamini kabisa jambo hilo. Niliwaza kifo ni mwisho wa mambo yote na hakuna tumaini lolote kwa ajili ya watu waliokufa.”—Fernando.

Umekwisha kujiuliza hivi: ‘Ni nini kinatokea kabisa kisha mutu kufa? Watu waliokufa wenye tulikuwa tunapenda wanateseka nafasi fulani? Tutawaona tena siku moja? Ni nini kinaweza kutusaidia tusadiki kama tutawaona tena?’ Tafazali, ona mambo Biblia inafundisha. Kwanza, tuone Biblia inafananisha kifo na nini. Kisha, tutazungumuzia tumaini lenye Neno la Mungu, Biblia, linatoa.

Watu waliokufa wako katika hali gani?

JIBU LA BIBLIA: ‘Walio hai [wazima] wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe, wala hawana malipo tena, kwa maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Yote ambayo mukono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote, kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi, mahali unapokwenda.’ *Mhubiri 9:5, 10.

Kwa kifupi, Kaburi ni mahali watu wanaenda kisha kufa; ni hali ao nafasi ya mufano kwenye hakuna ufahamu ao kazi yoyote. Mwanaume muaminifu Ayubu alielewa kuwa Kaburi ni nini? Alipoteza mali yake yote na watoto wake wote siku moja, na kisha majipu (vidonda) yenye kuleta maumivu sana yalimuota kwenye mwili wote. Alimuomba Mungu hivi: “Ungenificha katika Kaburi, kwamba ungenificha.” (Ayubu 1:13-19; 2:7; 14:13) Ni wazi kuwa Ayubu alielewa kama Kaburi ni nafasi ya kupumzikia, lakini hakuelewa kama ni nafasi ya moto wa mateso kwenye maumivu yake yangekuwa mengi zaidi.

Kuko jambo lingine la kutusaidia tuelewe hali ya watu waliokufa. Tunaweza kuchunguza habari za Biblia juu ya watu munane wenye walifufuliwa.—Soma kisanduku “ Ufufuo Munane Wenye Kuzungumuziwa Katika Biblia.”

Kati ya wale watu munane wenye walifufuliwa, hakuna hata mumoja wao mwenye alisema kama alikuwa nafasi ya furaha ao ya mateso. Ikiwa watu hao walienda nafasi kama hiyo wakati walikufa, wangeambia watu juu ya jambo hilo. Na habari hiyo ingeandikwa katika Biblia ili watu wote waisome, haiko vile? Katika Maandiko, hakuna habari ya namna hiyo. Kwa kweli, watu hao munane hawakusema kitu juu ya habari hiyo. Sababu gani? Ni kwa sababu wakati walikuwa wamekufa, walikuwa katika hali ya kutojua kitu, kama vile katika usingizi muzito. Kwa kweli, wakati fulani Biblia inafananisha kifo na usingizi. Kwa mufano, wanaume waaminifu Daudi na Stefano ‘walilala usingizi katika kifo.’—Matendo 7:60; 13:36.

Basi, kuko tumaini gani kwa ajili ya watu waliokufa? Wanaweza kuamuka katika usingizi huo?

^ fu. 7 Katika Biblia TakatifuTafsiri ya Ulimwengu Mpya, neno “Kaburi” linatumiwa ili kutafsiri neno la Kiebrania “Sheoli” na neno la Kigiriki “Hadesi.” Biblia fulani zinatumia neno “kuzimu,” lakini Maandiko hayaonyeshe kuwa kuko nafasi kwenye roho za watu zinaendelea kuishi kisha watu kufa.