Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | MASHAHIDI WA YEHOVA NI NANI?

Feza Zenye Kusaidia Kazi Yetu Iendelee Zinatoka Wapi?

Feza Zenye Kusaidia Kazi Yetu Iendelee Zinatoka Wapi?

Kila mwaka, tunachapisha na kugawanya mamilioni ya Biblia na vichapo vyenye kuzungumuzia Biblia. Tunajenga nafasi za kuchapishia vichapo na biro za inchi mbalimbali na tunaongoza kazi zenye kufanywa nafasi hizo. Maelfu ya makutaniko yanakusanyika katika nafasi za ibada zenye kupendeza lakini zisizopambwa sana, zenye kuitwa Majumba ya Ufalme. Feza za kufanya mambo hayo yote zinatoka wapi?

Kazi yetu yote inasaidiwa na michango ya kujipendea. (2 Wakorintho 9:7) Katika mwaka wa 1879, gazeti la pili la Munara wa Mulinzi lilisema hivi: “Tunaamini kwamba gazeti Munara wa Mulinzi linategemezwa na YEHOVA, na ikiwa ni hivyo, halitaomba-omba wala kuwalilia-lilia watu watoe feza ili kulitegemeza.” Hatujakuwa na mashaka juu maneno hayo.

Michango ya kujipendea inatumwa moja kwa moja kwenye biro za inchi mbalimbali ao inatiwa katika kisanduku cha michango chenye kuwa katika kila Jumba la Ufalme. Lakini, hatuombe sehemu ya kumi, hatukusanye sadaka, hatulipwe juu ya kazi tunafanya, na hatuuzishe vitabu vyetu. Hatulipwe ili kuhubiria watu, kufundisha katika kutaniko, ao kusaidia katika kujenga nafasi za ibada. Zaidi ya hilo, Yesu alisema hivi: ‘Mulipokea bure, mutoe bure.’ (Mathayo 10:8) Watu wote wenye kutumika kwenye biro za inchi mbalimbali na kwenye makao yetu makubwa, na hata wale wenye kufanyiza Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova, hawalipwe.

“Kama ilivyo juu ya kazi zote za Mashahidi wa Yehova, feza za kusaidia kazi ya dini iendelee zinatolewa kwa kujipendea, kila mumoja anaamua yeye mwenyewe atatoa ‘muchango’ wa ngapi na mara ngapi.”—Tribinali ya Ulaya ya Haki za Wanadamu, 2011

Tena, michango inatumiwa ili kusaidia wale wenye kupatwa na misiba. Wakristo wa kwanza walifurahi kutoa michango ili kusaidia wale wenye walikuwa na taabu. (Waroma 15:26) Sisi pia tunasaidia wale wenye kupatwa na misiba kwa kuwajengea tena nyumba zao na nafasi za ibada, na kwa kuwapatia chakula, mavazi, na matunzo.